Sautisol ft. Ali Kiba - Unconditionally Bae

Sautisol ft. Ali Kiba - Unconditionally Bae

Ahlan Wasahlan brothers and sisters!

Acheni tuwe wakweli, binafsi nimeanza kumfuatilia Huyu Msanii Muda mrefu lakini zaidi sana Na Kwa undani Ni kuanzia 2007 mpaka Leo.

Kwa kifupi Ni Msanii mzuri mwenye uwezo wa kucheza vizuri Na sauti Yake, sijui Kama hua anatunga mwenyewe Au anatungiwa hizo nyimbo zake Ila Kwa kiasi kikubwa anajitahidi.

Ila Sasa kuna huu wimbo wa kuitwa Unconditionally bae, Alikiba ameshirikishwa, Kwa jinsi ninamvyomjua Na uwezo wake katika huu wimbo hajafanya kazi yeyote, Yaani kaimba vibaya!

Imagine anasema "jina langu Ali Sasa lazima Nile" Sasa hii maana Yake Nini? Alikosa Kabisa cha kuandika hapo? Au Ndio mambo ya mizani? Huo wimbo Ni mzuri sana Anzia vionjo vyake Ktk beat mpaka mpangilio wa sauti za hao wenye wimbo wao lakini Huyu Msanii wetu kapooza sana katika nafasi Yake ingawa upande wa video kafanya vizuri.

Hivyo Kwa maoni yangu Ni kwamba Alikiba KAHARIBU wimbo wa watu, Hebu piga picha ule wimbo wangeimba wenyewe tu Sauti Sol, ungependeza sana!

Ushauri wangu; Next time Alikiba akipata nafasi ajitahidi kuimba serious Na mistari yenye mashiko, unapoleta utani Ktk issue serious haujiangushi wewe tu, unatuangusha mpaka sisi Watanzania wenzio.

NB: Hayo Ni maoni yangu Mimi binafsi Mgibeon, sina team yeyeto ya kushabikia hapa bongo zaidi ya Young Africans Sports Club! Kila mtu anasikio lake la kusikilizia uzuri Na ubaya wa wimbo, hivyo hala hala Na matusi jamani, tafadhari sana!
Hahahahaaaaaaa maoni yako Mzee ungekuwa fair ungezungumzia na zile sauti zilizopanda za I beliiiiiiiiiiieve.... Ningejua umeskiza na umehukumu kwa haki ila kusema hakuna jamaa alichofanya kwenye wimbo ule ni kumuonea Mzee... Ali katisha sana mule haswa kwenye I belieeeeeeeeeve..
 
Sasa Ndio Nini hicho Mkuu? Huo Ndio ule utani niliosema mwanzoni, issue serious analeta maskhara! Fikiria jinsi alivyo ghani katika nyimbo Kama Njiwa, mapenzi yanarun Dunia, Mackmuga Na hata ule waliimba Na kina R.kelly linganisha Na huu utaona!
Kuna harufu ya utimu Fulani hapa japo hutaki kuweka wazi
 
Kuna harufu ya utimu Fulani hapa japo hutaki kuweka wazi
Me sina utimu Mkuu! Frankly speaking nawakubali wasanii wanaofanya vizuri including Kiba mwenyewe, shida ya Kiba amepanic, Mwambieni tampolise!
 
Me sina utimu Mkuu! Frankly speaking nawakubali wasanii wanaofanya vizuri including Kiba mwenyewe, shida ya Kiba amepanic, Mwambieni tampolise!
Katika hiyo nyimbo umemuonea mkuu... Hiyo nyimbo jamaa kaitendea haki from audio to video Mzee.
 
Duh kweli watz ni wachawi kama huu wimbo ni mbaya basi jide hakukosea pale aliposema chizi lazima ashushwe mirembe na safari iendeleee, Uncondationally bae ndio habar ya Africa kwa sasa, I beliveeeee. Pop it in
 
Sauti Sol (Kenya) and Alikiba (Tanzania) release UNCONDITIONALLY BAE, a danceable love ballad. In the song, Sauti Sol and Alikiba sing about the difficulty of finding love in the modern day world. The music video is poised to unite fans across East Africa and Africa at large, through dance and its strong message.
#SautiSolAlikiba
#UnconditionallyBae

Shot in Kenya’s beautiful North Coast of Mombasa at the English Point Marina, the official video of UNCONDITIONALLY BAE has been shot by the super talented South African video director Justin Campos of Gorilla Films.



Sources: Ghafla.co.ke || Sauti Sol || YouTube



Good music
 
Kiba acha aitwe mfalme... Funga kazi. Ile sauti ya kupanda ikageuzwa ikashuka.. Achaaaa kabisa!!! Naiweka Ringtone
 
Wimbo wa saut sol na Ali kiba ndani ya radio ya uswiss

nimetumiwa tu na Mshikaji anayeishi uswiss. Angalia hapo kwenye baadhi ya nyimbo zilizopigwa leo. Kiba yupo kwenye 14:--
 

Attachments

  • ImageUploadedByJamiiForums1459967974.669265.jpg
    ImageUploadedByJamiiForums1459967974.669265.jpg
    63.2 KB · Views: 76

Similar Discussions

Back
Top Bottom