888I
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 445
- 553
Huwa naliona gazeti Wamachinga likijinasibu na kauli mbiu yake: “Sauti ya Wanyonge.”
Lakini mara nyingi kurasa zake za mbele zimepambwa na sura za viongozi wakubwa wa kisiasa, watu wenye nafasi kubwa serikalini, pamoja na mabwenyenye wenye ushawishi wa kifedha na kiserikali.
Sasa najiuliza: wanyonge gani hasa wanapewa sauti katika gazeti hili?
Je, ni wale mama lishe, machinga mitaani, bodaboda, wakulima na wavuvi wanaotaabika na gharama za maisha?
Au “wanyonge” hawa wanaozungumziwa ni hao wanasiasa waliopo madarakani na matajiri wenye nafasi ya kupiga picha ukurasa wa mbele?
Ikiwa kweli gazeti lina kauli mbiu ya “sauti ya wanyonge,” kwa nini mara chache sana tunaona simulizi za wananchi wa kawaida, changamoto zao, na kilio chao kikipata nafasi kubwa ukurasavwa mbele?
Au labda tafsiri ya “wanyonge” katika uandishi huu imebadilishwa — kwamba mwenye nguvu akijipa taswira ya “mnyonge,” basi ndiye anayepewa kipaumbele?
Lakini mara nyingi kurasa zake za mbele zimepambwa na sura za viongozi wakubwa wa kisiasa, watu wenye nafasi kubwa serikalini, pamoja na mabwenyenye wenye ushawishi wa kifedha na kiserikali.
Sasa najiuliza: wanyonge gani hasa wanapewa sauti katika gazeti hili?
Je, ni wale mama lishe, machinga mitaani, bodaboda, wakulima na wavuvi wanaotaabika na gharama za maisha?
Au “wanyonge” hawa wanaozungumziwa ni hao wanasiasa waliopo madarakani na matajiri wenye nafasi ya kupiga picha ukurasa wa mbele?
Ikiwa kweli gazeti lina kauli mbiu ya “sauti ya wanyonge,” kwa nini mara chache sana tunaona simulizi za wananchi wa kawaida, changamoto zao, na kilio chao kikipata nafasi kubwa ukurasavwa mbele?
Au labda tafsiri ya “wanyonge” katika uandishi huu imebadilishwa — kwamba mwenye nguvu akijipa taswira ya “mnyonge,” basi ndiye anayepewa kipaumbele?