Saudi Arabia yatoa msaada MOI

Saudi Arabia yatoa msaada MOI

KAUMZA

JF-Expert Member
Joined
Aug 31, 2010
Posts
699
Reaction score
240
Serikali ya Kifalme ya Saudi Arabia (Walinzi wa misikiti mitukufu ya Makka na Madina) imetoa vifaa mbalimbali kwa Taasisi ya mifupa ya MOI ya hospitali ya Taifa ya Muhimbili, kwa ajili ya kuwahudumia watoto wanaozaliwa wakiwa na vichwa vikubwa (vichwa maji). Tunashukuru kwa msaada. Huo ni uislam.
 
watakuwa wanaleta udini hawa. wapeleke huko sudan.

.......

Jamaa hili pweza kweli udini kwa kusaidia vingetoka marekani sio udini au itali sasa hv kila kitu udini kweli umesahaulishwa kufanya harakat zenye maana.
 
Hii niliona ITV jana kwenye taarifa ya nabari. Kilichonishangaza ni mtangazaji kusema kuwa sasa watoto wenye matatizo ya vichwa vikubwa wataweza kutibiwa nchini kwa kuwa Muhimbili wamepata msaada wa vyombo vyenye thamani ya kama dola laki moja na kitu.

Kushangazwa kwangu kunaaanzia kwa kujiuliza kuwa kweli serikali ya Tanzania ilikuwa imeshindwa kupata dola hizo na kununua vyombo hivyo?

Ina maana hawa watoto walikuwa wanakufa kwa kukosa vyombo vya upasuaji/matibabu vya dola laki moja? Kwa mawazo yangu, serikali inatumia zaidi ya hizo fedha kwenye mambo mengine yasiyo muhimu.

Ni jambo la aibu kuwa kwa sababu tumepokea msaada huo, watoto wetu hawatakufa tena. Pale ambapo tuna uwezo wa kujitegemea tufanye hivyo, ama sivyo tutakuwa tunadharauliwa siku zote!
 
Hii niliona ITV jana kwenye taarifa ya nabari. Kilichonishangaza ni mtangazaji kusema kuwa sasa watoto wenye matatizo ya vichwa vikubwa wataweza kutibiwa nchini kwa kuwa Muhimbili wamepata msaada wa vyombo vyenye thamani ya kama dola laki moja na kitu. Kushangazwa kwangu kunaaanzia kwa kujiuliza kuwa kweli serikali ya Tanzania ilikuwa imeshindwa kupata dola hizo na kununua vyombo hivyo? Ina maana hawa watoto walikuwa wanakufa kwa kukosa vyombo vya upasuaji/matibabu vya dola laki moja? Kwa mawazo yangu, serikali inatumia zaidi ya hizo fedha kwenye mambo mengine yasiyo muhimu. Ni jambo la aibu kuwa kwa sababu tumepokea msaada huo, watoto wetu hawatakufa tena. Pale ambapo tuna uwezo wa kujitegemea tufanye hivyo, ama sivyo tutakuwa tunadharauliwa siku zote!

Huwaga hatuna tabia ya kujitegemea kwahiyo tutaendelea kutegemea misaada mpaka dunia ifike mwisho
 
watakuwa wanaleta udini hawa. wapeleke huko sudan.

Watu kama nyinyi ndio mnaongoza kwa kuiangusha nchi kwa ubaguzi.Na pengine huna mchango wowote kwa Taifa.Tunawashukuru sana kwa msaada wao na mwenyezi mungu azidi kuwapa moyo wa huruma.
 
Hii niliona ITV jana kwenye taarifa ya nabari. Kilichonishangaza ni mtangazaji kusema kuwa sasa watoto wenye matatizo ya vichwa vikubwa wataweza kutibiwa nchini kwa kuwa Muhimbili wamepata msaada wa vyombo vyenye thamani ya kama dola laki moja na kitu.

Kushangazwa kwangu kunaaanzia kwa kujiuliza kuwa kweli serikali ya Tanzania ilikuwa imeshindwa kupata dola hizo na kununua vyombo hivyo?

Ina maana hawa watoto walikuwa wanakufa kwa kukosa vyombo vya upasuaji/matibabu vya dola laki moja? Kwa mawazo yangu, serikali inatumia zaidi ya hizo fedha kwenye mambo mengine yasiyo muhimu.

Ni jambo la aibu kuwa kwa sababu tumepokea msaada huo, watoto wetu hawatakufa tena. Pale ambapo tuna uwezo wa kujitegemea tufanye hivyo, ama sivyo tutakuwa tunadharauliwa siku zote!

Kwa hili nakubaliana nawe!! Tunafurahia ujio wa vifaa vya $150,000 kuwa sasa vifo vitapungua. Tunashindwa kwenda mbele zaidi na kujiuliza haya:
a) Je ni kweli hatuna uwezo wa kupata hizo $150,000 katika hazina yetu wenyewe??
b) Je kuokoa maisha ya watoto si swala la msingi kuliko kutumia mabilioni kufanya sherehe za kiserikali?
c) Je mgeni anapataje kujua matatizo yetu ya ndani na kuyatatua kabla yetu kwa fedha za aibu kiasi hiki??

Kwa walio na wajibu wa kifamilia, utajisikiaje mgeni akikutembelea lakini baada ya siku kadhaa siku moja akaja na kilo ya nyama, sukari, unga wa ngano nk?? Na sababu ni kuwa hitu hivo havipatikani nyumbani kwako!!

Taifa linafikia low point kiasi hiki kweli?? Tupate misaada ya kujengewa barabara kwa mamilioni ya dola, kweli na hata $150,000???
 
Jamaa hili pweza kweli udini kwa kusaidia vingetoka marekani sio udini au itali sasa hv kila kitu udini kweli umesahaulishwa kufanya harakat zenye maana.[/QUOTE
tumezoea vya kutoka kwa wazungu. ila sina uhakika kuhusu ushoga kama tutakuwa tayari kama taifa. hivyo vya kwa waarabu vina majini.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom