Satellite: Kwa nini isibaki angani?

Satellite: Kwa nini isibaki angani?

Kwa kuongezea ni kuwa ikishalipuliwa na kumegeka vipande vipande au kama ni ndogo basi huanza safari ya kuanguka.

Kila inavyosogea dunia, gravitation huongezeka na speed kuwa kubwa na hivyo kuongeza wind resistance ambayo nayo huongeza joto kwenye vipande au chombo hicho.

Ndiyo maana ile ndege ya NASA kwenye uvungu wake wanatumiwa mawe special yanayoweka kuhimili joto kubwa na yanapoteza joto hilo haraka. Unaweza kulichoma hadi likawa jekundu ila ukilitoa kwenye moto tu hapohapo waweza kuyashika mkononi bila muwa na gloves.
Ndege hii ya NASA ilikuwa wakati inashuka, joto mwenye tumbo lake lilizidi 1000*C. Hata chombo cha Warusi huwa kikitua kutoka spacestation huwa kama vile mimetoka kuchomwa moto na unaona kama masizi......

BF8BFA44-2D50-4983-8620-F4980801EC33_mw1024_n_s.jpg


https://www.youtube.com/watch?v=oZg3x7yy80o


https://www.youtube.com/watch?v=Pp9Yax8UNoM

Dah! Huu uzi niliuanzisha kitambo!
 
Umri wa setelaiti ni miaka 15 kwa zile ambazo hurushwa juu zaidi ya kilometa 36,000 toka uso wa dunia. Kwa zile ambazo hulizunguka jua kwenye umbali huo huwa na umri wa miaka 12.

Kitu gani huifanya setelaiti ifikie ukomo wa umri? Setelaiti zina kifaa kiitwacho propellant (fueli) ambacho huifanya setelaiti ibaki kwenye orbiti yake. Kifaa hiki hufa wakati vifaa vingine vingali vinafanya kazi.

Setelaiti zile za umbali mkubwa zinapofikia ukomo wa umri husogezwa mbali zaidi toka uso wa dunia; huenda hata 2000 km. Eneo hilo huitwa kaburi la setelaiti (satellite graveyard). Aidha, setelaiti nyingi hulipuka zinapofika huko. Vipande vya setelaiti iliyolipuka huweza kuleta madhara makubwa kwa setelaiti nzima. Hivyo, husogezwa mbali ili ikalipukie huko.

Setelaiti zinazozunguka dunia chini ya umbali wa km 36,000 zinapokufa hulipuka zikidondoka. Na kila mwaka takribani setelaiti 12 hufa na huondoka katika orbiti zake.

Mbona hatuoni zikidondoka? Zile zizungukazo umbali wa zaidi ya km 36,000 hupelekwa kwenye kaburi la satelaiti. Hata zikilipuka na kusambalatika, ili mabaki yake yafike kwenye uso wa dunia huchukua miaka na miaka. Huweza kuchukua kuanzia karne moja hadi milenium moja.

Kwa setelaiti za chini. Hizi zinapolipuka vipande vyake huweza kuchukua miaka 25 au zaidi kufika duniani. Na mara zote vipande hivyo havijaleta madhara yoyote hadi sasa kwa hapa duniani. Vipande vingi vimekuwa vikidondoka katika uso wa dunia.

Nani anazipeleka huko kaburini?
 
Back
Top Bottom