Companero
Platinum Member
- Jul 12, 2008
- 5,604
- 1,704
Mada hii inahusu uhusiano kati ya Sataranji na Siasa. Sataranji ni mchezo ambao hutumia fikra nyingi na mipango mingi tarajali kumshinda mpinzani. Katika mchezo huu, ambao vinara wake walikuwa ni Mafia a Sicily, Italia na Warusi kama Gary Kasparov, mtu husoma mchezo wa mpinzani na kutambua njia anuwai ambazo mpinzani huyo aweza kusogeza kete. Lakini mtu haishii kuzisoma tu hizo njia mbalimbali, bali pia hupanga njia anuwai za namna ya kucheza kwa kutegemea na jinsi mpinzani atakavyosogeza kete yake. Hivyo hivyo ndivyo ilivyo katika medani ya siasa zilizokubuhu. Kinara katika medani hii katika siku za hivi karibuni ni Rais Barack Hussein Obama ambaye alitumia mbinu ya Kisataranji kumgalagalaza Hillary Clinton katika uchaguzi wa awali wa Mgombea Urais kwa tiketi cha Chama cha Democrats. Hata Rais wa sasa nchini aliucheza kimahiri mchezo huo 1995-2005 ndio maana magwiji wa siasa walishindwa tena kumchomoa kama ilivyotokea 1995.
Hapa nchini itakuwa vigumu sana kudai kuwa mbinu hii haitumiki ipasavyo hasa ukizingatia kuwa kuna mitandao lukuki ndani ya chama tawala. Ndio maana ni kujidanganya kudhani Sisiemu imeshtukizwa na kupitishwa kwa Dakta Slaa kuwa mgombea wa Urais kwa tiketi ya Chadema. Hivyo, cha kujiuliza ni, je, chama tawala kilipanga nini mara baada ya kusoma dalili za nyakati na kuona uwezekano wa mtu huyu mwenye ushawishi mkubwa ndani na nje ya Sisiemu kupitishwa. Ikumbukwe huyu alikuwa ni Mwanasisiemu ambaye alikigalagaza chama chake hicho cha zamani baada ya kugoma kumpitisha kugombea jimbo la Karatu japo alikuwa anakubalika zaidi kwa maoni ya wanasisiemu wa jimbo hilo.
Sataranji ina siri nzito - Slaa akiicheza vizuri basi anaweza kuisambaratisha 'Ngome ya Sicily' 2010!