Junius
JF-Expert Member
- Mar 11, 2009
- 3,181
- 139
Rais Sassou Ngueso.
Rais Denis Sassou-Nguesso ataendelea kuwa madarakani kwa kipindi cha miaka mingine saba baada ya kunyakua ushindi mkubwa katika uchaguzi ambao ulisusiwa na vyama vya upinzani ambavyo viliishutumu serikali kwa kujilimbikizia kura.
Tume ya uchaguzi ilisema Bwana Sassou-Nguesso alikuwa amepata zaidi ya asilimia 78 ya kura na mpinzani wake wa karibu akiwa na chini ya asilimia 10.
Wafuasi wa upinzani wapatao elfu mbili walijaribu kuandamana kwenye mitaa ya mji mkuu Brazzavile lakini wakasambaratishwa na polisi waliowatimua na gesi za kutoa machozi.
Polisi walimwandama mwandishi wa BBC mjini Brazzavile, Thomas Fessy na mwenzake wa kituo cha televisheni cha Ufaransa na kuwanyanganya vifaa vyao vya kazi.
Fessy alisema maandamano hayo yalikuwa salama lakini polisi waliwashambulia na kuwatawanya kwa gesi za kutoa machozi.
Licha ya malalamiko ya upinzani, kiongozi wa kundi la waangalizi wa Umoja wa Afrika, Dieudonne Kumbo Yaya aliiambia BBC kwamba hawakushuhudia kisa chochote cha udanganya katika upigaji kura uliomalizika Jumapili iliyopita.
SOURCE: BBC(SWAHILI SERVICE)