Bado sijajua sababu ni nini ila ningependelea kufahamu ni kwanini ukiwa unakaribia mkoani mara ukitokea mwanza maeneo ya usukumani ukiwa unaingia mkoa wa mara unakutana na tangazo limeandikwa sijui kama manisipaa au serikali limeandikwaaaa.
"SASA UNAINGIA MKOA MARA"
lakini ukienda mikoa mingine unasikia karibu mwanza,karibu kagera,karibu shinyanga na mikoa mingine yote ni karibu lakini ukiingia mkoani mara
"SASA UNAINGIA MKOANI MARA" ni kwanini tunasema sasa unaingia kwa wale wanaofahamu historia ya mkoa wa mara mpka panaandikwa sasa hebu tusaidiane kupeana info ni kwanini