Sasa ni Zamu ya Wazanzibar...

Kuenzi maana yake nini,nani anawenziwa,na nani muwezeshi,Swali kama upande mmoja tayari mmoja amewenziwa.Kama zanzibar ni nchi kwani mwangagania muwenziwe na mwenzaji asiye taka kuwenzi kwani siye hatuoni radha ya kuwawenzi nyiee sasa mwataka nini bar?
 
Baada ya wananchi wa upande wa bara kutoa rais wa Jamhuri ya Nuungano mara 2 mfululizo ni vema sasa wanzetu wa Bara mkatuachia ndugu zenu wa Visiwani urais hapo mwaka 2015. Hii itasaidia kuenzi muungano wetu ulionzishwa na wale viongozi wetu mahiri mzee Karume na Mwalimu Nyerere.


ndugu yako nani au unamaanisha mgombea urais kupitia sisiemu na kafu atoke kwenu
 
Hiyo ni ndoto ya mchana kwenu Wazanzibar! Tatizo lenu ni ubinafsi ndo unawasumbua, ukifika wakati wa uchaguzi mathalani mwaka jana mnadai muungane eti kwa maslah ya zenj!? Mnafikiri sisi mazezeta tuwape nchi hv hv, mmesahau kuwa usaliti wenu umeua upinzan na demokrasia? Hiyo zam peanen huko huko zenj msituletee porojo hizo.
 
Mtoa mada ombi lako lipeleke ccm huku si mahala pake, taratibu kama hizo zinajadilika ccm. Lakin akina EL umesha wa-mark?
 
Hivi nyie wazanzibari,ni hiyo tu sababu mtakayompa EL au kuna nyingine?Kama ni hiyo,basi futeni kabisaa hii hoja yenu.Watu wanajiandaa karibu miaka 20 halafu nyie mnaleta porojo zenu eti tupokezane!
 
Ni zamu ya Lowassa kuwa rais hamtaki damu itamwagika
LICHA YA ADUI HATARI ITAKAYOIUA CCM KWA HARAKA ZAIDI NDANI KWA NDANI HIVI KARIBUNI, CHAMA HIKI KIKO MBIONI KUJITWISHA MIZIGO MIPYA KUMBEBA LOWASA NA HASA KUFANYA MAUAJI YA SAUTI PINZANI KISIRI KUSAFISHA NJIA

Kama uliwahi kufikiria kwamba CHADEMA ndicho adui mkubwa itakayoiua CCM basi kumbe kweli huelewi kabisa siasa za taifa hili zilivyo lakini hivi sasa kundi dogo ndani ya CCM linaloshikilia uhai wa chama hiki kiko mbioni 'KUSAFISHA NJIA KWA NAMNA YOYOTE ILE mmoja wao kushaka dola 2015.

Kwa wadadisi wa mambo, adui mkubwa zaidi na wa kutisha ajabu tayari yuko chumbani kwao CCM na hivi karibuni italipuka kuliko KINU CHA NYUKLIA CHA JAPAN na kutuma mionzi itakayoifuta kabisa CCM bukia chama cha upinzani namba 4 baada ya NCCR-Mageuzi hapa nchini.

Kwa kugusia tu kwa uchache; adui namba moja na hatasri mno hadi hivi, kwa haki kabisa kwa misingi ya kichama walichojiwekea, ni kwamba kule Wa-Tanzania Visiwani wanakiona CCM kama Chama kilichowasaliti kushika dola baada ya Mhe Benjamin Mkapa.

Hakika jambo hili la USALITI WA CCM KWA WATANZANIA VISIWANI ni tishio kubwa hivi sasa ambapo majina zaidi kutoka Bara yaendelea kutajwa KUMRITHI Mhe Kikwete ambaye naye kwanza hata hatima yake bado haiko wazi kwa umma wa Tanzania.Kwa jinsi mambo yalivyo nchini itakavyolipua Naona baada ya CCM kuwatapeli Wa-Tanzania Visiwani nafasi ya kugombea Urais, katika ule mpango wao maalum wa SIASA ZA KUKABIDHIANA UONGOZI WA NCHI KWA ZAMU KWA WATOTO WA WAKUBWA tu Bara na Visiwani.

Kitendo cha kikundi fulani kujipenyezea fedha haramu kupitia kwa akina Rostam Aziz na Edward Lowasa katika dakika za majeruhi kushawishi maamuzi kumtosa Mhe Salim Ahmed Salim (ambaye alipendwa sana bara na kuaminiwa mno na CCM-Mwalimu Nyerere) kule Dodoma, ndipo jini dume lenye vichwa viwili lilipozaliwa na kuleta salamu za maangamizi kwa hiki chama kilichowahi kupata umaarufu wa miaka mingi sana na kuaminiwa wa wengi nchini.

Miongoni mwa hizo salamu ni pamoja na (1) Wana-Mtandao badala ya Wana-CCM (ambao nao walikujakugawanyika mbele ya safari na kuwa (i) Wanamtandao Walaji (MAFISADI WA HIVI LEO) na Wanamtandao Waliwa ambao nao mahasibu yao mazito na yanayo nuka mno tutakuja kuyaelezea siku nyingine humu, (2) Wana-CCM Bara ambao lao ni kuwatumia baadhi ya Wana-CCM maswahiba kutoka Visiwani wakiwachezesha kama mchezo wa CHESS au DRAFT KISIASA ili kuzuia Wa-Tanzania wa kawaida Bara na Visiwani kuwa na maamuzi yoyote juu ya nani awaongoze isipokua tu maamuzi yote yatatoka siku zote kwa hii CCM Bara tu kwa sura zima ya Jamhuri yetu ya Muungano Tanzania.

Sasa kwa ujio wa CHADEMA na kuendelea kupendwa sana kwa chama hiki na azma yake ya KURUDISHA UONGOZI WA NCHI MIKONONI MWA WANANCHI WENYEWE kote Bara na Visiwani, na haya madai Moto Moto ya sisi Vijana kutaka Katiba Mpya na Tume Huru ya Uchaguzi kote ndani ya taifa letu tayari zimekua ni mwiba mchungu katika ngozi ya kikundi hiki cha WAJANJA WACHACHE Wana-CCM Bara ambao mpaka hivi sasa, kwa mujibu wa habari nyeti za ndani sana chumbani mwao, kila ramani ya kisiasa wanalolichora linagoma kabisa, fedha walizokwisha wekeza kwenye juhudi hizi zote Bara na Visiwani zakumbwa na hatari za wazi mno na migawanyiko kuongezeka kila kukicha kati yao.

Hata nako ndani ya kikundi hicho cha hao Wajanja wachache Wana-CCM kumeibuka nako Migawanyiko mikali ya KI-KANDA kwa namna ambayo hata juhudi gani zifanyike hakuwezekani kupatanishwa kitu hata wakafanya kazi kwa pamoja.

Kwa mujibu wa vyanzo vya ndani ya CCM katika ujumla wake, hali si shwari hata kidogo mle!! Wapo hata wale ambao, kwa ufinyu tu wa mawazo, wamefikia mahala wamependekeza MAJINA 15 ya baadhi ya watu mashuhuri na tishio kwa maslahi yao KUUAUA. Lini wauawe na kwa MTINDO GANI usioweza kuleta tafrani kwa kile wanachokiita 'Tishio la Nguvu ya Umma' kutokuweza kuwakumba.

Japo tatizo letu Wa-Tanzania tuliowengi ni mpaka tushikishwe jambo kiganjani ndio tuamini na wakati mwingine kugutuka kukiwa kumechelewa sana, miongoni mwa HAYO MAVUNO YA MIKONO YA KI-SHETANI tayari wameorodheshwa baadhi ya vinara wa kupinga madhambi ya CCM kwa njia mbali mbali nchini.

Kati ya watu wanaolengwa wamo (i) baadha ya viongozi tishio kwa kinyang'anyiro cha kiti cha urais 2015 waliomo ndani na nje ya hicho kikundi cha Rostam Aziz na Edward Lowasa. Pia, (ii) wapo baddhi ya viongozi wa serikali za wanafunzi nchini, (iii) baadha ya Wana-JF ambao wametajwa kama 'wakorofi na waharibifu', (iii) baadhi ya viongozi wa dini katika kanda fulani ambao wameelezewa kuwa na 'vinywa pana' na kuonekana kukisaidia CDM, (iv) wafanyabiashara wanaohofiwa kukifadhili CHADEMA hivi sasa na (v) na baadhi Wanataaluma wanaoonekana kujitolea kukisaidia CDM ki-mikakati ambayo hadi sasa yaelezewa KUKIDHOOFISHA MNO hiki chama tawala.

Sasa chama hiki chaonekana kubuni (1) mkakati mpya wa UONZOZI WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA kukabidhiwa kwa zamu ile ile ila safari hii ni NDANI KWA NDANI TANZANIA BARA na vile vile ni (2) kwa KUZINGATIA AMA URAFIKI, UJIRANI AU UDINI kufanya hivyo.

Hata hivyo nako mambo si yenyewe baada ya wale wafadhali wa Uarabuni (Libya, Misri na Iran) nazo kukumbwa na matatizo kibao, yale yanayoendelea na yale ambayo yatalipukia kwao miezi michache ijayo; kikundi hiki ndani ya CCM kimechanganyikiwa kupindukia kwani kwani ufadhili wao hauna uhakika tena huku wananchi tukiendelea kulishikilia bando DOWANS na mianya mingine itakayotumika kuchota kodi zetu kuyatekelezea haya yote.

Dawa ya yote haya wanayopangwa kutekelezwa kwa mikono ya giza ni (1) kuhakikisha kwamba kila mmoja wetu anageuka kuwa mlinzi wa mwenzie dhidi ya juhudi hizi hatari, (2) kusimama kidete kwa KUSISITIZA Katiba Mpya ya Wananchi na Tume Huru ya Uchaguzi kupitishwa Bungeni mwezi ujao, (3) kuendelea kuhakikisha kwamba UTEUZI WA JOHN MIMOSE CHEYO kushika tena ile kamati kule bungeni haiwi tena kichochoro tena cha Mafisadi kujichotea fedha kununulia kura na kutekelezea mambo machafu huku Cheyo akijifanya hajaona kitu kwenye vitabu vyetu!!
 
Mabadiliko ya katiba lazima yataje hilo jambo. Hata akitoka chama gani ni lazima awe mzenji. Urais kwa awamu.
 
Mkuu.
Unaikwepa ban...lakini unaingia katika mtego wa CCM..udini. Wakitokea wa "al jihad" na wao wakisema kinyume cha unachosema huoni tunaiingiza Nchi kule ambako hata wewe kwa kujua maafa yake hupendelei.

Nakumbuka ulipoanza mfumo wa vyama vingi ilikuwa ndio mwisho wa mzenj kuwa Rais wa Serikali ya Muungano...pia yale mabadiliko ya Katiba ya kumuondoa Rais wa Zanzibar kuwa makamo wa Rais ndio iliua Muungano. Kwa bahati mbaya kila "mtanzania" yumo ndani ya denial..tunaendeleza usanii.

La ajabu zaidi ni kauli za kuwa tuigeuze Zanzibar iwe mkoa au wilaya. Hatukuwa tunafanya review ya Muungano kila mwaka ndio sababu tumejikuta katika hali hii ya leo.Hatujui historia ya Muungano,hatuji tumeungana katika mambo yepi, hatuji nchi zilizoasisi muungano. hatujui hadhi ya muungano..sisi tumo tu kupiga kelele na mayowe.

Hizi kauli za kuwa "al jihad" wa bara au visiwani hawezi kuwa Kiongozi wetu ndio unafukia kaburi la nchi iitwayo Tanzania, tunairudisha "Tanzania bara" au jina lile maarufu la nchi anayoipigania bila aibu na bila kuchoka Rev. Mtikila. na hapo ndio huu "udini" tunaoupalilia na kuupigia matarumbeta ndio utatutafuna vizuri na hayataishia hapo.

Plziiiiiiiiiii, apo kwenye red sio mko au wilaya, iwe kata ili kiongozi mkuu awe afisa mtendaji tu,ndo hadhi yake na muungano ndo utaimarika-
 
Mabadiliko ya katiba lazima yataje hilo jambo. Hata akitoka chama gani ni lazima awe mzenji. Urais kwa awamu.

Katika marais sita wa zenj, ni mmoja tu ndo kutoka pemba, while katika marais wanne wa Tanzania mmoja ni kutoka zenj-so utaona ili mlingano ukamilike inabidi marais wawili zaidi toka tanganyika watawale ndo ije zamu ya zenj-provided rais ajaye zenj awe kutoka pemba. Kiherehere cha nn?
 
Plziiiiiiiiiii, apo kwenye red sio mko au wilaya, iwe kata ili kiongozi mkuu awe afisa mtendaji tu,ndo hadhi yake na muungano ndo utaimarika-
Mkuu.
Ningefurahi sana kama tutaacha ushabiki na kejeli katika kujadili hoja ambazo zinagusa mishipa ya fahamu ya taifa kama hii.

Mkuu, miungano mengine duniani..taja EAC, EU, SADC,..au nchi UK, nitajie Muungano wowote duniani ulioimarika kwa kuua au kufuta waanzilishi wake au kwa kuishusha hadhi nchi mbia wa Muungano.

Sisi tunafanya utani lakini utani huu unatupeleka pabaya.

Je unaelewa kuwa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ulikuwa wa mambo kumi na moja tu. EAC inashughulika na mambo ya pamoja mangapi?

Je unaelewa kuwa kuna nchi ndogo zaidi ya Zanzibar duniani?

Tuache utani, tufungue bongo zetu, tufikiri na tutafakari. Baada ya hapo watu wajadili je kuna umuhimu wa Muungano wa Tanzania wakati EAC ndio imo safarini inaziunganisha nchi za Afrika Mashariki?

Ndio sababu ya kupendekeza Mjadala wa Muungano na muundo wake utangulie ule wa Katiba ya Muungano. Kosa kubwa ambalo tunalifanya sote ni pale tunapoepuka kusema kuwa pia uwepo mjadala wa kuifufua katiba ya Tanganyika. Hili ndilo linaleleta kejeli na utani tunapojadili hoja za Katiba ya Muungano na Muungano wenyewe.
 
Zanzibar mna nchi yenu huru, mna rais na makamu wa rais wawili,baraza la mawaziri na isitoshe kuna makamu wa rais na mawaziri kutoka Zanzibar kwenye serikali ya muungano; bado hamtosheki tu!!Naisitoshe bado mnapewa vyeo vingi tu huku Tanganyika; kitu ambacho hakifanyiki kwa Mtanganyika kupewa mamlaka huko Zanzibar.Tanganyika ni nchi huru tumechoka kutawaliwa kijaja.
 
Zanzibar mna nchi yenu huru, mna rais na makamu wa rais wawili,baraza la mawaziri na isitoshe kuna makamu wa rais na mawaziri kutoka Zanzibar kwenye serikali ya muungano; bado hamtosheki tu!!Naisitoshe bado mnapewa vyeo vingi tu huku Tanganyika; kitu ambacho hakifanyiki kwa Mtanganyika kupewa mamlaka huko Zanzibar.Tanganyika ni nchi huru tumechoka kutawaliwa kijaja.
<br />
<br />
Kule ni serikali ya ZAnzibar ndio maana Watanganyika hamnahaki wala nafasi ktk serikali ya zanzibar. Hii huku ni serikali ya Muungano wa Tanzania Wazanzibar wana haki ya kushika nafafi yoyote, vinginevyo muiite serikali ya Tanganyika.
 
Mkuu.
Ningefurahi sana kama tutaacha ushabiki na kejeli katika kujadili hoja ambazo zinagusa mishipa ya fahamu ya taifa kama hii.

Mkuu, miungano mengine duniani..taja EAC, EU, SADC,..au nchi UK, nitajie Muungano wowote duniani ulioumikarika kwa kuua au kufuta waanzilishi wake au kuishusha hadhi nchi mbia wa Muungano.

Sisi tunafanya utani lakini utani huu unatupeleka pabaya.

Je unaelewa kuwa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ulikuwa wa mambo kumi na moja tu. EAC inashughulika na mambo ya pamoja mangapi?

Je unaelewa kuwa kuna nchi ndogo zaidi ya Zanzibar duniani?

Tuache utani, tufungue bongo zetu, tufikiri na tutafakari. Baada ya hapo watu wajadili je kuna umuhimu wa Muungano wa Tanzania wakati EAC ndio imo safarini inaziunganisha nchi za Afrika Mashariki?

Ndio sababu ya kupendekeza Mjadala wa Muungano na muundo wake utangulie ule wa Katiba ya Muungano. Kosa kubwa ambalo sote tunaliepuka ni kusema pia uwepo mjadala wa kuifufua katiba ya Tanganyika. Hili ndilo linaleleta kejeli na utani tunapojadili hoja za Katiba ya Muungano na Muungano wenyewe.

Acha ujuha wee nonda, unakumbuka juu ya relations na functions? yale mambo kumi na moja asilia ya muungano ndo kama kila kitu na hivyo yale 11 mengine yaliyoongezeka siyo mapya in such! so wote wanaodai nani kaongeza mambo ya muungano kutoka 11 ni watoto wa kuchambua na kuchanganua. Kama hutaki kuigeuza zenj wilaya na uigeuze Tanganyika Tarafa bac kama itapungua kitu
 
Zanzibar mna nchi yenu huru, mna rais na makamu wa rais wawili,baraza la mawaziri na isitoshe kuna makamu wa rais na mawaziri kutoka Zanzibar kwenye serikali ya muungano; bado hamtosheki tu!!Naisitoshe bado mnapewa vyeo vingi tu huku Tanganyika; kitu ambacho hakifanyiki kwa Mtanganyika kupewa mamlaka huko Zanzibar.Tanganyika ni nchi huru tumechoka kutawaliwa kijaja.

Wilaya ya Nyamagana ni kubwa(kieneo+wakazi) kuliko Zanzibar,inaongozwa na Mbunge Wenje.Zanzibar for what???? ondoeni urojorojo!!!
 
Baada ya wananchi wa upande wa bara kutoa rais wa Jamhuri ya Nuungano mara 2 mfululizo ni vema sasa wanzetu wa Bara mkatuachia ndugu zenu wa Visiwani urais hapo mwaka 2015. Hii itasaidia kuenzi muungano wetu ulionzishwa na wale viongozi wetu mahiri mzee Karume na Mwalimu Nyerere.

Tupe kifungu cha katiba
 
Acha ujuha wee nonda, unakumbuka juu ya relations na functions? yale mambo kumi na moja asilia ya muungano ndo kama kila kitu na hivyo yale 11 mengine yaliyoongezeka siyo mapya in such! so wote wanaodai nani kaongeza mambo ya muungano kutoka 11 ni watoto wa kuchambua na kuchanganua. Kama hutaki kuigeuza zenj wilaya na uigeuze Tanganyika Tarafa bac kama itapungua kitu
Mkuu Mipangomingi.
Nikushukuru kwa dhati kabisa kwa ushauri wako.
Mkuu. Challenge ambayo ipo ya Muungano leo ni matokeo ya watu kama wewe waliokuwa na mipangomingi na usiri mkubwa katika kufanikisha mipango hiyo.

Mkuu hakuna katika dunia hii muungano unaolingana na huu wa Tanganyika na Zanzibar. Lakini hakuna muungano unaozifuta nchi waanzilishi wa Muungano huo. Na ndio sababu baada ya miaka 47 hakuna nchi nyengine iliyotaka kujiunga nasi na hata kama ingejiunga sijui tungebadilisha jina tena? Kuna Member aliwahi kusema Comoro wanataka kujiunga nasi..nikamuuliza jee jina la nchi litakuwa Tanzancomia? na utaifa mpya utakuwa utanzancomia?

Kwa hiyo lilikuwa ni kosa kubwa kujaribu kuifuta Tanganyika..unaijua "Tanzania bara"? lakini ni kosa pia kujaribu kuifuta Zanzibar au kuimeza Zanzibar. Katika sehemu moja pia nimewahi kuonesha kuwa Tanganyika ipo na Taasisi zake nyengine zinaonekana wazi. Sio wizara zote kuwa ni za Muungano. mfumo wa mahakama wa Tanzania bara. sasa mkuu ujuha unakujaje hapa?

Mimi sijazungumzia kuongezeka kwa mambo ya Muungano kuwa ni batili au ubabe au vyenginevyo. ninachosema Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ulikuwa wa mambo kumi na moja. Sasa mkuu, mambo kumi na moja vipi yanaunda nchi moja?
kwa hiyo ni wazi zilikuwepo mamlaka tatu za kisheria. Mamlaka ya Tanganyika, Mamlaka ya Zanzibar na mamlaka ya Muungano.

Kama kuna ujuha katika hili basi ni "ujuha" wetu sote. Kwa sababu hatuujui Muungano wetu, asili yake wala hadhi yake. Sishangai kwa hili kwani wakati wa Utawala wa Mwalimu kuudadisi muungano ilikuwa ni uhaini.

Asante sana kwa ushauri huu "Acha ujuha wee nonda". Nitajitahidi kuutekeleza ushauri wako.
 
Baada ya wananchi wa upande wa bara kutoa rais wa Jamhuri ya Nuungano mara 2 mfululizo ni vema sasa wanzetu wa Bara mkatuachia ndugu zenu wa Visiwani urais hapo mwaka 2015. Hii itasaidia kuenzi muungano wetu ulionzishwa na wale viongozi wetu mahiri mzee Karume na Mwalimu Nyerere.
Hakuna kitu kama hicho na sisi mtuachie Mtoto wa Mkulima aje awe raisi huko visiwani kwani hata siku moja hajatoka raisi toka bara aheri nyie Mwinyi amewahi kuwa raisi huku kwa miaka kumi
 
Mkuu Mipangomingi.
Nikushukuru kwa dhati kabisa ushauri wako.
Mkuu. Challenge ambayo ipo ya Muungano leo ni matokeo ya watu kama wewe waliokuwa na mipangomingi na usiri mkubwa katika kufanikisha mipango hiyo.

Mkuu hakuna katika dunia hii muungano unaolingana na huu wa Tanganyika na Zanzibar. Lakini hakuna muungano unaozifuta nchi waanzilishi wa Muungano huo.

Kwa hiyo lilikuwa ni kosa kubwa kujaribubu kuifuta Tanganyika lakini ni kosa pia kujaribu kuifuta Zanzibar au kuimeza Zanzibar. Katika sehemu moja pia nimewahi kuonesha kuwa Tanganyika ipo na Taasisi zake nyengine zinaonekana wazi. Sio wizara zote kuwa ni za Muungano. mfumo wa mahakama wa Tanzania bara. sasa mkuu ujuha unakujaje hapa?

Mimi sijazungumzia kuongezeka kwa mambo ya Muungano kuwa ni batili au ubabe au vyenginevyo. ninachosema Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ulikuwa wa mambo kumi na moja. Sasa mkuu, mambo kumi na moja vipi yanaunda nchi moja?
kwa hiyo ni wazi zilikuwepo mamlaka tatu za kisheria. Mamlaka ya Tanganyika, Mamlaka ya Zanzibar na mamlaka ya Muungano.

Kama kuna ujuha katika hili basi ni "ujuha" wetu sote. Kwa sababu hatuujui Muungano wetu, asili yake wala hadhi yake. Sishangai kwa hili kwani wakati wa Utawala wa Mwalimu kuudadisi muungano ilikuwa ni uhaini.

Asante sana kwa ushauri huu "Acha ujuha wee nonda". Nitajitahidi kuutekeleza ushauri wako.
nadhani Nyerere na wale wafuasi wa fikra zake wanastahili lawama kwa kuifuta TANGANYIKA na kushindwa kuimeza ZANZIBAR.
 
Mna nchi yenu na rais wenu, sasa mnataka nini? mbona mna tamaa sana nyie?
Hao ni sawa na ngamia wa jangwani aliyeomba aiingize kichwa tu kwenye hema ili ajinusuru na mvua ,baadaye mwenye hema akajashutukia keshatolewa nje,hapa bara wamejaa na vidaladala vyao lakini thubutu nawewe upeleke chai maharage huko kwao utafanyiwa mtima nyongo mpaka utakoma
 
Back
Top Bottom