Sare za Chama kwenye ziara za kiserikali

Sare za Chama kwenye ziara za kiserikali

Nanoli

JF-Expert Member
Joined
Oct 15, 2015
Posts
3,739
Reaction score
5,978
Hi guys..

Kuna mambo ya kinafki kwa viongozi wa serikali hasa wale wa juu sana...
Wanapotuambia wanafanya mikutano ya serikali na sio ya kichama, ninachojua mimi ni kwamba, Mkutano huo utahudhuriwa na wananchi wote bila kujali itakadi ya vyama vyao.

Sasa inakuaje kiongozi kama Rais, Waziri mkuu na wengine wanapofanya mikutano kama hii, hutawala jezi za Chama kimoja tu, hawaoni kama wanaleta manyanyaso na ubaguzi kwa vyama vingine kuwepo katika uwanja huo?

Jambo hili pia huchangia mfalme hujisikia kama vile anaongea na wanachama wa Chama kile pekee na kusahau wengine.

Wanachama hawa watashangilia kila baya na bovu atakaloongea mwenyekiti wao ili kukilinda Chama na kupalilia mbwembwe, misifa, kejeli na mipasho kwa vyama vingine.

Mikutano mingi inapewa jina la mikutano ya serikali huku agenda zinazoongelewa ni za kichama, na mkutano kiujumla ni wa kichama... Watu wanaona, na inaumiza sana, wao wanapovunja sheria zilizowekwa kinafki na wao wenyewe, Je huu sio uchwara?

Kama wanashindwa kusimamia kile walichokisema wao wenyewe, basi wawaache na wengine wafanye.

Ipigwe marufuku mikutano ya serikali kuvaa nguo za Chama,.. Zipo nguo za bendera ya Taifa, wavae hizo.
 
Ndugu wakuu nafatilia hotuba ya Rais kutoka Chato, cha kusikitisha zaidi, wakati wa kampeni ulishaisha, inakera sana kuona Rais anahutubia Taifa huku wengine wamevaa sare za chama...hivi hii ni haki kwa nini wanao wawakilisha wasiwape somo? Nawakilisha...
 
tuna nguo za uchaguzi ndo shine; vazi rasmi
 
Hakuna kitu kinanikela kama wanaccm kuvaa sare zao hata wakisikia anakuja RC kukagua mradi wa maji.

Sijui kama vyama vingine kama Chadema vinafanya huu ujinga.
Kama vinafanya viache utoto
 
Hii tabia ni mbaya sana na inakera

Sent from my itel it1408 using JamiiForums mobile app
 
Hakuna kitu kinanikela kama wanaccm kuvaa sare zao hata wakisikia anakuja RC kukagua mradi wa maji.

Sijui kama vyama vingine kama Chadema vinafanya huu ujinga.
Kama vinafanya viaje utoto
Kuna mambo ya chama na ya Kitaifa watu wanashindwa kutofautisha hivyo vitu viwili.

Sent from my GT-I9300 using JamiiForums mobile app
 
kwa mbunge wa chadema au ccm anakuwa kwenye mkutano wa hadhara asivae nguo za chama?
 
Hii ni serikali ya CCM. Subirini na nyie mtawale mtakuwa mnavaa zenu zile za pundamilia.
Serikali ipo chini ya CCM yaani Serikali ya CCM.
 
Hata marekan ipo hy

Sent from my HUAWEI SCL-U31 using JamiiForums mobile app
 
Ndoto Ya CCM sio kuongoza nchi. Ndoto ya CCM ni kuona hamna upinzani Tz.
Hizo ni ndoto zako. Siyo za CCM.
Soma katiba ya chama tawala cha CCM. Siyo kujiundia vijimaneno vya kijinga kijinga ili kujifariji.
Kama huna uwezo wa kupambana na CCM jiunge CCM.
Sasa unaaza kudanga watu. Ili iweje!?
Serikali ni ya CCM na nguo zitavaliwa kila sehemu okey.
 
mtoa mada umenena vema,wakati kodi za wananchi wote zinapotumika kwenye mikutano kama hii ,haileti maana yeyote,halafu tuna watu humu who are GT wanaposti uzi wa kutetereka kwa upinzani wakati wanayaona haya ,ccm wafanye kampeni wengine wasubiri hadi 2020!!
 
G4rpolitics kwani kuna kipengele kipi cha katiba na sheria kinachowakataza hao watu kuvaa hizo sare katika events za kiserikali?
 
Hizo ni ndoto zako. Siyo za CCM.
Soma katiba ya chama tawala cha CCM. Siyo kujiundia vijimaneno vya kijinga kijinga ili kujifariji.
Kama huna uwezo wa kupambana na CCM jiunge CCM.
Sasa unaaza kudanga watu. Ili iweje!?
Serikali ni ya CCM na nguo zitavaliwa kila sehemu okey.
Ulichoongea ndicho alichoongea Bujibuji. Kifupi, umekoleza point yake.
 
Hizi ndio ndoto za CCM, kila mtu ajiunge, je nani awe mpinzani wenu?
Sasa kuwa mpinzani ndio useme uongo!? Shindana kwa kuongea ukweli siyo kuongea uongo.
Katiba ya CCM haina unayoyasema. Shindana kwa sera siyo kuilisha maneno CCM.
Tangaza sera zako.
 
Back
Top Bottom