JF Kwenu,
Sijui ni nani wanamshauri Mh. Rais kuhusu namna ya kuongea mbele ya hadhira ya Watanzania anapofanya ziara. Labda hashauriki.
Rais amefanya ziara nyingi toka alipoanza kazi baada ya mapumziko. Alianzia Chato, mikoa ya kanda ya ziwa Morogoro na sasa yuko Tanga.
Ukifuatilia hata wanaohudhuria mikutano, wengine wakiwamo viongozi wa CCM, huona ni mikutano ya chama na kwa hiyo huvaa sare. Inawezekana kuna wengi wanaotaka kumsikiliza rais lakini wakiona wenzao wana sare hughairi. Inakuwaje rais anayedai ni rais wa wote amwite katibu mkuu wa CCM, aje kuzungumza jukwaani kwenye ziara ya kiserikali?
Sent using
Jamii Forums mobile app