Samwel Sitta, chui ktk kundi la kondoo.

SS hashobokei uwaziri kama ambavyo ungefikiria. Ashakuwa na hivyo vyeo toka miaka ya sabini. Ni miongoni mwa watu wachache wanaoipenda Tz na vyote vya asili na pia ni miongoni mwa wanachama wachache sana wanaotaka kuinusuru sisiemu.
 
JK alidhani kumuingiza Samwel Sitta katika serikali yake labda itakuwa ni njia mojawapo ya kuponya majeraha na mpasuko ndani ya chama chake. Lakini mambo yameenda tofauti. Samwel Sitta amekuwa akiikosoa serikali na maamuzi ya serikali hivyo kwenda kinyume na dhana nzima ya Uwajibikaji wa pamoja(Collective Responsibility). Majuzi na hata leo amepingana na uamuzi wa serikali wa kuilipa DOWANS. Ikumbukwe kuwa ni yeye aliyeifikisha CCM hapa ilipo.

Rais JK, mfukuze Sitta. Atakudhuru na ataiangusha serikali. Mbona wenzake akina Mwakyembe wametulia na wanachapa kazi? Sitta hakufai. Wanasema waswahili. ukimchekea nyani, utavuna mabua. Ana chuki baada ya kuukosa uspika.


We KAUMZA ni fisadi, wewe ni funza wa ufisadi, ukifika hatua ya kua nzi ukaruka na kutua juu ya ugali...utachafua sana hali ya hewa....unatetea ujinga...nawe mjinga....
 
Huo utakuwa ni uwajibikaji wa pamoja ktk kundi la vipofu, hata kuhujumu rasiliamali za Taifa? Kumb akina SS wako wengi ndani ya Sisiemu ila hawaongei!
 
Sita alitolewa usipika kwa maelezo kuwa , mwaka huu ni wa wanawake!!
Kapewa uwaziri ili asiseme machafu ya serikali!!!!
Kapewa wizara ya afrika mashariki ili asipate mda wa kuhudhuria bunge!!!
Sasa umefika wakati mwakyembe na mh sitta wamevunja viapo wa uwaziri na kikwete anatakiwa kuwafukuza kama alivyofanya mwinyi kwa mrema!!!
Je, kikwete ana uwezo wa kumufukuza ???
Kikwete angemurejesha sitta kuwa spika ingekuwa salama kwake !!!!
Kikwete hawezi kuchukua miezi sita sasa ni lazima apangue baraza la mawaziri!!
 
''You are always clear'' with the lack of clarity! Acha kuwa mvivu wa kufikiri , na usipende kuwa hodari wa umbea! Sitta anajaribu kuwa na mawazo huru yasiyo fungwa na uwaziri! Si lazima ukiwa waziri ushabikie usiri haramu! Je unamkumbuka bi clare short wa uingereza wakati wa sakata la radar ya tz?



Bi Clare alijiuzuru kwa kuwa alikuwa hakubaliani na serikali yake juu ya Radar. Ktk nchi zinazofuata mfumo wa kiutawala wa kibunge(parliamentary system), lazima ukubaliane na maamuzi ya serikali yako(Collective responsibility/uwajibikaji wa pamoja) na kama huwezi, unatakiwa ujiuzuru. Sitta ana nafasi ya kujiuzuru uwaziri ili aweze kuikosoa vizuri serikali
 
Back
Top Bottom