GE2025 Samia: Vyombo vyetu vya ulinzi na usalama, vimejipanga vyema, na tumevijengea uwezo wa kutosha

GE2025 Samia: Vyombo vyetu vya ulinzi na usalama, vimejipanga vyema, na tumevijengea uwezo wa kutosha

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Mafyangula

JF-Expert Member
Joined
Jan 16, 2025
Posts
505
Reaction score
887
Bi mkubwa anaendelea kuwatisha watanzania ambao wapo tayari kutetea nchi yao.

Ila hivi vitisho vina mwisho wake kwa wale wote wanajiona ni bora zaidi kuliko watanzania wengine.

==========

"Vyombo vyetu vya ulinzi na usalama ndani ya Taifa hili vimejipanga vyema, tumevijengea uwezo wa kutosha, vimejipanga vyema na tupo salama wakati wote. Iwe wakati wa uchaguzi, iwe hakuna uchaguzi, tupo salama.

"Hivi vitisho vidogo vidogo wanavyovifanya waulizeni. Sisi tupo salama wakati wote, na niwatoe hofu wananchi kwamba tokeni, kapigeni kura, tupo salama," Dk. Samia Suluhu Hassan, Mgombea urais kupitia CCM akizungumza na wananchi wa Ilala mkoani Dar es Salaam leo Oktoba 22, 2025.

 
20251022_222900.jpg
 
Hahaha swali hili hawezi kulijibu hata mbele ya Yuda
ila tatizo, wenye kuhoji maswali kama haya, nao wanapotea na kutoonekana tena. au tafsiri ya UTU katika namna yao, ni kuhakikisha watu wanaishi kwa hofu, mashaka na kudhulumiwa haki ya kuishi ? Najua mama yetu msikivu, anaweza tufafanulie hii
 
Bi mkubwa anaendelea kuwatisha watanzania ambao wapo tayari kutetea nchi yao.

Ila hivi vitisho vina mwisho wake kwa wale wote wanajiona ni bora zaidi kuliko watanzania wengine.
Hivi mfano wakiua raia 1,000 wasio na hatia wataendelea kuua tu? Kisa wameandamana? Swali fikirishi
 
ila tatizo, wenye kuhoji maswali kama haya, nao wanapotea na kutoonekana tena. au tafsiri ya UTU katika namna yao, ni kuhakikisha watu wanaishi kwa hofu, mashaka na kudhulumiwa haki ya kuishi ? Najua mama yetu msikivu, anaweza tufafanulie hii
Utu maana yake ni Utulivu km ulikua hujui nimekufumbua sio Utu ule unaoujua wewe Utu ni kifupi cha Utulivu

Kazi na Utulivu
 
Utu maana yake ni Utulivu km ulikua hujui nimekufumbua sio Utu ule unaoujua wewe Utu ni kifupi cha Utulivu
Mkuu wangu, mbona hata huo utulivu haupo huku kijijini kwetu, ni heka heka tu.. Na leo magari yao ya matisho wameyazagaza uswahili..
 
Mkuu wangu, mbona hata huo utulivu haupo huku kijijini kwetu, ni heka heka tu.. Na leo magari yao ya matisho wameyazagaza uswahili..
Ndio Utulivu wanaouzungumzia huo wewe ulifikiri Utulivu upi?
 
Tumevijengea uwezo wa kutosha:

Tumevipa Silaha za kuulia masikini bila huruma.
Tumevihakikishia ulinzi kisheria.
Tumevipa Pesa na ahadi nzito.
Tumevihakikishia Ulinzi na Usalama familia zao.

Wizi ukikunogea kuacha shida sana
 
Back
Top Bottom