PAYE
JF-Expert Member
- Jun 19, 2025
- 354
- 395
gombea wa nafasi ya urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Samia Suluhu Hassan, ameahidi kuwa ikiwa wananchi watampa ridhaa miaka mitano ijayo, Serikali yake itajenga maghala ya kuhifadhia mazao pamoja na soko la kisasa Wilayani Mbogwe mkoani Geita, ili kusisimua biashara na kilimo.
Samia ameyasema hayo leo Jumapili Oktoba 12, 2025 kwenye Mji mdogo wa Masumbwe wakati aliposimama kusalimia na kuomba kura kwa wananchi wa eneo hilo, akiwa njiani kutokea mkoani Shinyanga kuendelea na kampeni zake.
Ameahidi pia kuanza ujenzi wa barabara ya Masumbwe-Kasosobe, kuelekea makao makuu ya wilaya hiyo, barabara yenye urefu wa kilomita 45 na itakayojengwa kwa kiwango cha lami, ili kuondoa adha ya usafiri na kurahisisha shughuli za usafiri na usafirishaji katika wilaya hiyo.
Samia ameyasema hayo leo Jumapili Oktoba 12, 2025 kwenye Mji mdogo wa Masumbwe wakati aliposimama kusalimia na kuomba kura kwa wananchi wa eneo hilo, akiwa njiani kutokea mkoani Shinyanga kuendelea na kampeni zake.
Ameahidi pia kuanza ujenzi wa barabara ya Masumbwe-Kasosobe, kuelekea makao makuu ya wilaya hiyo, barabara yenye urefu wa kilomita 45 na itakayojengwa kwa kiwango cha lami, ili kuondoa adha ya usafiri na kurahisisha shughuli za usafiri na usafirishaji katika wilaya hiyo.