Samia na Kiti Cha Enzi Cha Sauti Zilizovunjika

Samia na Kiti Cha Enzi Cha Sauti Zilizovunjika

Pulchra Animo

Platinum Member
Joined
Jun 16, 2016
Posts
6,769
Reaction score
10,316
Ee Samia, uliyefunikwa kwa dhahabu iliyojaa damu, Ndoto gani mbaya zinazoishi ndani ya kimya chako? Chawa wako hukuimbia nyimbo za sifa kwa sauti tamu, Wapinzani hutekwa, huteswa na wengine hutoweka mitaani kama upepo.

Buti, gereza, kilio kilichozibwa—Gharama ya ukweli, bei yake—uongo. Lakini bado chawa wako huimba, Wakiimba nyimbo za sifa kuficha uovu ulio bayana.

Wewe hutawala kwa hofu, lakini hutamani fadhila, Mapenzi matupu kuficha aibu isiyo na kifani. Kwa kila sauti unayokandamiza kwa nguvu, Kivuli kitakutesa usiku bila usingizi wa kutosha.

Mitaa yatetemeka, kimya, imetulia, Lakini mifupa hukumbuka, majeraha hutiririka. Hakuna uongo unaweza kuifukia kweli—Hata ardhi italia kwa ajili yako kweli.

Basi cheza, Ee Malkia, kwa wakati wa kuazima, Wakati chawa wako wakikupamba kwa nyimbo zisizo na maana. Lakini mawimbi ya historia hayatakiepusha kiti cha enzi Kilichojengwa juu ya damu na mifupa yenye maumivu mengi.
 
Mungu na ajibu kwa haraka juu ya damu zisizo na hatia zilizomwagika juu ya ardhi na akisikie kilimo cha wajane na yatima wote.
 
Mungu anakwenda kuamua huu ugomvi soo,kikombe cha maovu yake kimekwisha jaa ba sasa kinafurika.
 
Hasahasa neno "chawa" linapoonekana.
Thamani ya chawa imepungua sana.
Mama kishatambua chawa hawawezi tena kumbakisha madarakani kwa sifa za uongo wanazo mpamba nazo, kwani waTanzania wamekwisha tambua ni hadaa na ulaghai.

Hatimae, Samia kaelekeza matumaini yake yote ya kumbakisha madarakani kwa kutegemea nguvu/mabavu; waTanzania wapende wasipende, yeye anabaki madarakani kwa gharama yoyote ile, hata ya kumwaga damu ya waTanzania.
Hili pekee ndilo tegemeo lake la kuendelea kuwa Rais wa nchi hii; siyo kupambwa pambwa kwa uongo mwingi na hao chawa.
Huoni hata humu JF wamebaki wale vichaa pekee? (Hardcore chawas)
 
Back
Top Bottom