Mafyangula
JF-Expert Member
- Jan 16, 2025
- 505
- 887
Hapo kwanza nichekee! Samia kumbuka kuna familia hawajui wapi walipo ndugu zao, wametekwa
=============
Mgombea wa nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema katika eneo la furaha na uhuru kwa Watanzania, serikali yake ya awamu ya sita imefanya vizuri, akiahidi kuendelea kutia bidii zaidi katika kuwafanya Watanzania kuwa na uhuru na furaha.
Dkt. Samia ametoa kauli hiyo leo Alhamisi Oktoba 23, 2025 wakati wa Mkutano wake wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu kwenye Viwanja vya Tanesco Buza, Wilayani Temeke Mkoani Dar Es Salaam
"Kama unakaa pazuri, unakula vizuri, afya nzuri, maji unayapata, umeme unauona, unapopata kuwasha tv unawasha maana yake furaha ipo tu, ukitaka haki yako unaipata, michezo unacheza kwahiyo kwa eneo la furaha tumefanya vizuri na tunajipanga kufanya vizuri zaidi." Amesema Dkt. Samia.
=============
Mgombea wa nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema katika eneo la furaha na uhuru kwa Watanzania, serikali yake ya awamu ya sita imefanya vizuri, akiahidi kuendelea kutia bidii zaidi katika kuwafanya Watanzania kuwa na uhuru na furaha.
Dkt. Samia ametoa kauli hiyo leo Alhamisi Oktoba 23, 2025 wakati wa Mkutano wake wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu kwenye Viwanja vya Tanesco Buza, Wilayani Temeke Mkoani Dar Es Salaam
"Kama unakaa pazuri, unakula vizuri, afya nzuri, maji unayapata, umeme unauona, unapopata kuwasha tv unawasha maana yake furaha ipo tu, ukitaka haki yako unaipata, michezo unacheza kwahiyo kwa eneo la furaha tumefanya vizuri na tunajipanga kufanya vizuri zaidi." Amesema Dkt. Samia.