DuaZaMama
JF-Expert Member
- Jun 2, 2025
- 1,882
- 4,129
Mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameahidi kuimarisha zaidi huduma za kijamii katika Jimbo la Chamwino ikiwa ni pamoja na afya, maji na barabara.
Akizungumza Agosti 31, 2025, katika mkutano wa kampeni uliofanyika Chamwino, mkoani Dodoma, Dkt. Samia amesema serikali ya CCM ina dhamira ya kuhakikisha wananchi wa jimbo hilo, ambalo pia ndilo lina Ikulu ya Rais, hawakabiliwi na changamoto za huduma za msingi.
“Niwaahidi kuwa tutakuja kuongeza vituo vya afya, vituo vya afya 10 na zahanati nyingine tano. Jimbo la Rais halitakiwi kuwa na shida yoyote ile, kwahiyo tutakuja kuongeza,” amesema Dkt. Samia na kuongeza,
“Ninajua tuna shida ya maji, mgombea ubunge hapa amesema mradi mkubwa upo, ninataka niwahakikishie tutahakikisha Chamwino yote inapata maji kwa karibu zaidi.”
Aidha, ameahidi kuendeleza ujenzi wa miundombinu ya barabara, akisema serikali itajenga kilomita 10 za barabara za kiwango cha lami na kuimarisha barabara za changarawe katika maeneo mbalimbali ya jimbo hilo.
Akizungumza Agosti 31, 2025, katika mkutano wa kampeni uliofanyika Chamwino, mkoani Dodoma, Dkt. Samia amesema serikali ya CCM ina dhamira ya kuhakikisha wananchi wa jimbo hilo, ambalo pia ndilo lina Ikulu ya Rais, hawakabiliwi na changamoto za huduma za msingi.
“Niwaahidi kuwa tutakuja kuongeza vituo vya afya, vituo vya afya 10 na zahanati nyingine tano. Jimbo la Rais halitakiwi kuwa na shida yoyote ile, kwahiyo tutakuja kuongeza,” amesema Dkt. Samia na kuongeza,
“Ninajua tuna shida ya maji, mgombea ubunge hapa amesema mradi mkubwa upo, ninataka niwahakikishie tutahakikisha Chamwino yote inapata maji kwa karibu zaidi.”
Aidha, ameahidi kuendeleza ujenzi wa miundombinu ya barabara, akisema serikali itajenga kilomita 10 za barabara za kiwango cha lami na kuimarisha barabara za changarawe katika maeneo mbalimbali ya jimbo hilo.