GE2025 Samia asisitiza katiba mpya itakamilika awamu ya sita

GE2025 Samia asisitiza katiba mpya itakamilika awamu ya sita

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

tonicimmobility

JF-Expert Member
Joined
Jun 17, 2025
Posts
493
Reaction score
1,038
Mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa mchakato wakupata Katiba mpya utakaika katika kipindi cha awamu ya sita.

Soma pia: Samia: Tutaendeleza mchakato wa Katiba Mpya kama ilivyo katika ilani yetu ya CCM



“Pamoja na hayo CCM inatambua kwamba zaidi mshikamano wa Watanzania kwa kukamilisha mchakato wa Katiba mpya kama ilivyoelekezwa kwenye Ilani yetu ya 2025-2030, haya ni matakwa ya makundi mbalimbali ya Watanzania kwa nyakati tofauti, tulijaribu wakati wa awamu ya nne mchakato haukukamilika, awamu ya sita tunaenda kuendeleza mchakato huo,” amesema Samia.

Samia amebainisha hayo leo, Ijumaa Oktoba 10, 2025, katika mkutano wa kampeni uliofanyika Uwanja wa Mwenge, Wilaya ya Butiama mkoani Mara na kuongeza kuwa hawatakubali nchi iyumbe kwa kisingizio chochote kile.
 
Kwenye tume huru ya uchaguzi ametuletea kiini macho! Hakuna mtu mwenye akili timamu anaweza kumuamini kirahisi tu. Hiyo Katiba mpya ataibadilisha jina tu, ila maudhui yake yote yatakuwa ni yale yale ya Katiba mbovu ya mwaka 1977!

Na katika hili, wananchi hatuko tayari kuendelea kuburuzwa na pia kuchezewa akili na wanasiasa wachache wabinafsi ndani ya nchi yetu.
 
Kwenye tume huru ya uchaguzi ametuletea kiini macho! Hakuna mtu mwenye akili timamu anaweza kumuamini kirahisi tu. Hiyo Katiba mpya ataibadilisha jina tu, ila maudhui yake yote yatakuwa ni yale yale ya Katiba mbovu ya mwaka 1977!

Na katika hili, wananchi hatuko tayari kuendelea kuburuzwa na pia kuchezewa akili na wanasiasa wachache wabinafsi ndani ya nchi yetu.
Nilimuuliza mwanaccm, hii mnayosema katiba mpya itakua na jipya gani ikiwa mmeshateka na kuua, mmefunga wapinzani mmebaki wenyewe, alafu ndio mtakuja na katiba bora?

Pale dodoma january mlipitishana kinguvu ndio leo mtaleta katiba bora? Hakunijibu
 
Hata ikija katiba mpya bado hakutakua na jipya. Uondoe ushindani, ufunge jela wapinzani wako, uteke na kuua, alafu usuburi katiba mpya ndio kuja kuwa nzuri ili kuleta haki?
Katiba ni yetu sisi Wananchi na sisi ndio tunatakiwa tuwe wakali pale Katiba inapokiukwa bila kujali itikadi na uvyama wetu.
 
CCM hawajawahi kuwa serious kwenye masuala yoyote yale yasiyo na maslahi kwenye chama chao. Kwa hiyo hata hiyo Katiba wanayo jifanya kuipigia promo, itakuwa ni maigizo tu kama haya maigizo tunayo yashuhudia kwenye tume yao "huru" ya uchaguzi.
 
Mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa mchakato wakupata Katiba mpya utakaika katika kipindi cha awamu ya sita.

Soma pia: Samia: Tutaendeleza mchakato wa Katiba Mpya kama ilivyo katika ilani yetu ya CCM

View attachment 3486629

“Pamoja na hayo CCM inatambua kwamba zaidi mshikamano wa Watanzania kwa kukamilisha mchakato wa Katiba mpya kama ilivyoelekezwa kwenye Ilani yetu ya 2025-2030, haya ni matakwa ya makundi mbalimbali ya Watanzania kwa nyakati tofauti, tulijaribu wakati wa awamu ya nne mchakato haukukamilika, awamu ya sita tunaenda kuendeleza mchakato huo,” amesema Samia.

Samia amebainisha hayo leo, Ijumaa Oktoba 10, 2025, katika mkutano wa kampeni uliofanyika Uwanja wa Mwenge, Wilaya ya Butiama mkoani Mara na kuongeza kuwa hawatakubali nchi iyumbe kwa kisingizio chochote kile.
Katiba ya CCM nani anaitaka? Katiba ya Mafisadi nani anaitaka?

CCM hawawezi kutuba Katiba bora kamwe? Nani wa kutupa Katiba bora? Hawa wanaojinufaisha kwa Ufisadi??
 
Mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa mchakato wakupata Katiba mpya utakaika katika kipindi cha awamu ya sita.

Soma pia: Samia: Tutaendeleza mchakato wa Katiba Mpya kama ilivyo katika ilani yetu ya CCM

View attachment 3486629

“Pamoja na hayo CCM inatambua kwamba zaidi mshikamano wa Watanzania kwa kukamilisha mchakato wa Katiba mpya kama ilivyoelekezwa kwenye Ilani yetu ya 2025-2030, haya ni matakwa ya makundi mbalimbali ya Watanzania kwa nyakati tofauti, tulijaribu wakati wa awamu ya nne mchakato haukukamilika, awamu ya sita tunaenda kuendeleza mchakato huo,” amesema Samia.

Samia amebainisha hayo leo, Ijumaa Oktoba 10, 2025, katika mkutano wa kampeni uliofanyika Uwanja wa Mwenge, Wilaya ya Butiama mkoani Mara na kuongeza kuwa hawatakubali nchi iyumbe kwa kisingizio chochote kile.
Never......never labda JK akinyongwa....au Afe kibudu....ila aliwepo na remote anayo yeye hakuna kitu unafikiii
 
Miaka 4 ilitosha kupata katiba mpya hakuwa na nia maana katiba mpya pia ilikuwa ni kaburi la chama chake .

Kenya walipata katiba ndani ya mwaka 1 na miezi nane tu baada ya machafuko ya 2007/08 na mchakato wa katiba ulianza Novembeer 2009 na August 27 , 2010 walipata Katiba mpya .

Hivyo hakuna lolote jipya kutoka kwa Samia na CCM , kwa miaka 4 hiyo angeweza kufanya mapitio ya rasimu ya jaji Warioba na wangeweka mabadilio mapya kadhaa ila vyote alishindwa.
 
Hakuna CCM wa kukupa hata Katiba ya Warioba wewe.

Na mali za Umma wanazoiba na kujinufaisha na familia zao wakupe Katiba mpya iliyo bora ili iwaahughulikie?

Hawa dawa pekee kwao ni kuwaondoa madarakani hiyo Oktoba 29
Ngoja tuone 29/10
 
Katiba ni yetu sisi Wananchi na sisi ndio tunatakiwa tuwe wakali pale Katiba inapokiukwa bila kujali itikadi na uvyama wetu.
Katiba haiwezi kuwa yetu, Bali ni yao
Katiba imekiukwa sana huo ukali wa wananchi upo wapi?
Watu mnnashindwa kuelewa kuwa na katiba ni jambo moja na kuifuata ni Jambo lingine. Unafikiri katiba ya sasa inaruhusu watu kutekwa na kuuwawa?
Hii tu iliyopo hakuna anayeifuata
 
Katiba haiwezi kuwa yetu, Bali ni yao
Katiba imekiukwa sana huo ukali wa wananchi upo wapi?
Watu mnnashindwa kuelewa kuwa na katiba ni jambo moja na kuifuata ni Jambo lingine. Unafikiri katiba ya sasa inaruhusu watu kutekwa na kuuwawa?
Hii tu iliyopo hakuna anayeifuata
Wananchi wanatakiwa wapewe elimu ili waelewe Katiba ya nchi lakini hivi sasa wananchi waliowengi hawana uelewa wa Katiba yao ndio maana inakiukwa inakanyagwa na wao wanachojali ni Simba na Yanga.
 
Back
Top Bottom