Sam Mahela wa ITV na kipindi cha upande mmoja

Sam Mahela wa ITV na kipindi cha upande mmoja

Tairi bovu

JF-Expert Member
Joined
Sep 28, 2017
Posts
3,063
Reaction score
2,987
Mahela kipindi chako kinakosa mvuto. wanangalia wachache.

Mosi, unauliza mambo ambayo ni ama huyajui au umedangishwa. Maswali mengi uliyomuliza jafo ilifaa umulize Mtendaji wa Kata au Mek (Mratibu wa elimu kata)

Pili, kipindi kinakosa mvuto kwa kuwa kuna fanani/ msimuliaji tu na hadhira hairuhusiwi kuliza maswali.

Tatu, maswali unayouliza siyo fikirishi yanampa muulizwaji nafasi ya kuelezea hisia badala ya actual facts. Mfano wewe unasemaje? Hupaswi kumuliza waziri hivyo kwakuwa hujamwalika kama mtu binafsi umeialika wizara.

Nne, unatumia vibaya gesture? Kuongeza chunvi yale unayoyaongea.huwapi watazamaji uhuru wa kuamua juu ya unachohoji.

Nakifananisha kipindi hiki na mazungumzo baada ya habari, bwana Juma Ngondai alikuwa ananiacha na maswali mengi sana pasi na majibu lakini sasa najua alikuwa anadanganya, kutisha na kuogofya watu.

Mahela boresha kipindi, ruhusu simu toka kwa walaji
 
Wewe nae una uvumilivu, ulikaa dk zote 45 ukitegemea labda mtangazaji atabadilika lakini wapi. Mm huwa nikisikiliza mada ya siku hiyo tu na aina ya mgeni aliyealikwa najua kabisa hapo ni bora nilale mapema, ni kama ninamaliza LUKU yangu tu.

Maswali yanayoulizwa majibu yake ni obvious hata mwendawazimu anaweza kujibu kwa usahihi. Mfano niliwahi kusikia swali la kipima joto “ je mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi, hatua kali zichukuliwe kwa wanaobainika kutenda unyama huo”? Hilo ni swali kweli? mm nikikaa sebuleni kuangalia TV hadi watoto wangu huwa nahisi kama hawafurahi, maana nikishika remote muda wote mm ni kuhamisha channel tu, huwa sivumilii kusikiliza mambo ya ajabu ajabu, hata siasa wakishaleta za upande ule tu nahamisha. Kuna siku walificha remote, kila ninayemuuliza anasema hajaiona na hiyo TV waliwasha wao. Nikajiongeza tu kuwa hawa watoto wamegundua nitaanza kuhamisha hamisha, nikaamua kuingia tu chumbani kwangu na kujivinjari na jf, instagram na tweeter

Usiikaribie dhambi kwa kigezo kwamba umeokoka, unaweza kuteleza shetani hajawahi kufa, muda wote anatafuta watu awameze.
 
Itv walishapoteza sifa zao za super brand.. now wachache wanaangalia pia mambo yao yamekuwa ndo yale yale sikuhiz si wabunifu.. soon itakuwa tv station ya kawaida tu..
 
  • Thanks
Reactions: BAK
mahela .
kipindi chako kinakosa mvuto. wanangalia wachache.
mosi, unauliza mambo ambayo ni ama huyajui au umedangishwa.maswali mengi uliyomuliza jafo ilifaa umulize mtendaji wa kata au Mek (mratibu wa elimu kata)
pili, kipindi kinakosa mvuto kwa kuwa kuna fanani/ msimuliaji tu. na hadhira hairuhusiwi kuliza maswali.
tatu, maswali unayouliza siyo fikirishi .yanampa muulizwaji nafasi ya kuelezea hisia badala ya actual facts. mfano wewe unasemaje? hupaswi kumuliza wazir hivyo kwakuwa hujamwalika.kama mtu bnafsi. umeialika wizara.
nne, unatumia vibaya gesture? kuongeza chunvi yale unayoyaongea.huwapi watazamaji uhuru wa kuamua juu ya unachohoji.
nakifananisha kipindi hiki na mazungumzo baada ya habari. bwana juma ngondai. alikuwa ananiacha na maswali mengi sana pasi na majibu.lakini sasa najua alikuwa anadanganya, kutisha na kuogofya watu.
mahela boresha kipindi.ruhusu simu toka kwa walaji
Una muda wa mchezo sana..kwangu mm marufuku clouds FM, clouds TV, radio one, TBC, ITV. Ni marufuku kwangu..!! Habari naangalia azam two ..nikitaka mpira dstv, nikitaka yanga azam anatosha..nikitaka mziki MTV base, Chanel e ya majizo basi..!! Wanafki hawana nafsi kwangu.

Tena habari nyingi now nazipata jf zikiwa hazijaeditiwa. Miziki YouTube.

ebu angalia mtangazaji anavyomuhoji Rais wa France..mahela kujipendekeza tu..tatzo hatobadilika ataona km tunamchukia.



Kidogo charles hilary/nurdin suleman/ivona na Muhuza wanaweza kumweka mtu kitimoto na kumchapa maswali ya maana.. Poor ITV..
 
Hicho kipindi kina dakika nyingi lakini ni kama kipindi cha propaganda za ccm/serekali. Kipindi ambacho hakina kupiga simu na kuuliza maswali kisha mjadala wa mtu mmoja huwa nakipuuza. Hofu imeikumba ITV toka awamu hii iingie madarakani, ni kama imenyooshewa kidole na mkulu. Hapa tusubiri muda wa huyu jamaa uishe, huenda ikarudi katika ubora wake.
 
Hicho kipindi kina dakika nyingi lakini ni kama kipindi cha propaganda za ccm/serekali. Kipindi ambacho hakina kupiga simu na kuuliza maswali kisha mjadala wa mtu mmoja huwa nakipuuza. Hofu imeikumba ITV toka awamu hii iingie madarakani, ni kama imenyooshewa kidole na mkulu. Hapa tusubiri muda wa huyu jamaa uishe, huenda ikarudi katika ubora wake.
Tindo unaweza kuwa na kipindi ambacho watu hawapigi simu lakini kama host ni mzuri kinanoga tu. Huyu Mahela wengine tulisema muda mrefu kwamba anabore na anaingia katikati ya kipindi. Ni mtangazaji wa ajabu sana wakati mwingine yeye anajigeuza kuwa ndiye mwalikwa anajijibu maswali yake. Anauliza maswali ya hovyo hovyo kabisa. Labda naye anavizia fursa kama za akina Buhohela za kutokea kwenye Dakika 45 kwenda idara ya Mawasiliano Ikulu!
 
Hicho kipindi kina dakika nyingi lakini ni kama kipindi cha propaganda za ccm/serekali. Kipindi ambacho hakina kupiga simu na kuuliza maswali kisha mjadala wa mtu mmoja huwa nakipuuza. Hofu imeikumba ITV toka awamu hii iingie madarakani, ni kama imenyooshewa kidole na mkulu. Hapa tusubiri muda wa huyu jamaa uishe, huenda ikarudi katika ubora wake.
Mkuu unamaanisha nini kusema muda wake uishe? 2020? Mbona kuna dalili anaweza kuondoka mwenyewe baada ya zoezi la 26/4?
 
Nguzo Mia hata familia yako inakuonà baba mlegezo kufunga mkanda chini ya matako!¡!!!!!
 
Hicho kipindi kina dakika nyingi lakini ni kama kipindi cha propaganda za ccm/serekali. Kipindi ambacho hakina kupiga simu na kuuliza maswali kisha mjadala wa mtu mmoja huwa nakipuuza. Hofu imeikumba ITV toka awamu hii iingie madarakani, ni kama imenyooshewa kidole na mkulu. Hapa tusubiri muda wa huyu jamaa uishe, huenda ikarudi katika ubora wake.
Sio lazima kupiga simu maana hata wapiga simu huwa wanapangwa waulize nini. ilitakiwa kipindi kina uliza maswali bila kumpa mgeni kutoa ngonjera kuiga sio kubaya hivi hawaoni BBC Hardtalk, unapigwa maswali kama boxing unawekwa corner hakuna hadithi.
 
Back
Top Bottom