McLaren
JF-Expert Member
- Feb 19, 2025
- 889
- 2,863
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), Salum Mwalimu, akiwa katika Kata ya Guruka, Jimbo la Kigoma Kusini, mkoani Kigoma, ameahidi kuwa serikali yake itaweka nguvu katika kupambana na umaskini kwa kuanzisha viwanda vya kuongeza thamani ya mazao, kuboresha huduma za afya na kuimarisha sekta ya kilimo.
Amesema viwanda vitakavyojengwa vitasaidia kuzalisha ajira kwa vijana wa Kigoma na kuongeza kipato kwa wananchi wa maeneo ya vijijini.
Aidha amesisitiza kuwa afya bora ni msingi wa maendeleo, hivyo serikali ya CHAUMMA itahakikisha zahanati na vituo vya afya vinaboreshwa na vinapatikana karibu na wananchi
Amesema viwanda vitakavyojengwa vitasaidia kuzalisha ajira kwa vijana wa Kigoma na kuongeza kipato kwa wananchi wa maeneo ya vijijini.
Aidha amesisitiza kuwa afya bora ni msingi wa maendeleo, hivyo serikali ya CHAUMMA itahakikisha zahanati na vituo vya afya vinaboreshwa na vinapatikana karibu na wananchi