Next hit atagonga 1M within a dayWazee wa kuboost views!
Unaliwa weweKanichambua kama karanga mama. Chambua kama karangaaa
Good morning mabibi na mabwana. Inatia moyo sana kuona msanii kutoka bongo land anaweka rekodi na kuivunja mwenyewe. Mpaka sasa hakuna msanii yeyote barani afrika ambaye Video zake zinatizamwa na watu wengi ndani ya muda mfupi kama Mondi Platnumz.
Sio kuwa tunajivunia Viewers ila tunajivunia Mziki wetu kutoboa zaidi Anga za kimataifa.
Japo kuna watu wachache walioanza kuleta chokochoko na kutaka wimbo huu mpya ufungiwe kwa madai ya kutokuwa na maadili ila wengi wetu tunampongeza kwa ubunifu na kumsaidia Bi Saida karoli kurudi tena masikioni mwa watu. Binafsi baada ya kusikia wimbo huu niliamua Kudownload na wimbo wa Saida karoli ili nione kama ameutendea haki wimbo huo.
Hongera Diamond platnumz na tunatarajia leo Tutahit 1M viewers ikiwa ni siku ya pili baada ya Salome Kufufuliwa.
Ujumbe wa leo " WENYE WIVU WAJINYONGE"
[HASHTAG]#mckonjetv[/HASHTAG]
Na sababu ya Kuliwa ni ipi kwa mfano.?Unaliwa wewe
Hii iko njiani.
Hapa ni suala la mtazamo tu lakini uhalisia ni kwamba hii inaonyesha ubora wa Saida dhidi ya diamond.Sio kuwa tunajivunia Viewers ila tunajivunia Mziki wetu kutoboa zaidi Anga za kimataifa.
Japo kuna watu wachache walioanza kuleta chokochoko na kutaka wimbo huu mpya ufungiwe kwa madai ya kutokuwa na maadili ila wengi wetu tunampongeza kwa ubunifu na kumsaidia Bi Saida karoli kurudi tena masikioni mwa watu. Binafsi baada ya kusikia wimbo huu niliamua Kudownload na wimbo wa Saida karoli ili nione kama ameutendea haki wimbo huo.
We bashaNa sababu ya Kuliwa ni ipi kwa mfano.?
Toka zakoIla dunia haiko fair kabisa, eti anayegawa haki ya wimbo ni Felician Mutta na si Saida Karoli, yaani kwa maana nyingine Siada Karoli huo wimbo hana haki nao haumuhusu daah, kweli shule ni muhimu
Tunamheshimu Saida kutokana na uwezo wake lakini watu wakiwa na mawazo kama yako basi wanaweza kusema unaporudia wimbo wa zamani ni kwamba unaona aliyefanya kuna mahali kaukosea na wewe unaweza kuufanya vizuri zaidi kuliko original version. Lakini kwa watu wanaofahamu hawawezi kusema hivyo kwa sababu kurudia ngoma au hata movie ya zamani (remake) ni mambo ya kawaida kwenye tasnia ya muziki na filamu!Hapa ni suala la mtazamo tu lakini uhalisia ni kwamba hii inaonyesha ubora wa Saida dhidi ya diamond.
Tatizo letu kubwa ni kwamba tunaangalia mafanikio kwa vigezo vya nani anamiliki nini (possession) badala ya traits halisi, Na sio ajabu kukuta vijana wametoa nyimbo mbili tu na wanamiliki used cars na nyumba alafu tunajiaminisha eti 'kijana kafanikiwa' na ukimwambia mtu huyo huyo kuwa hakuna mwanamuziki wa kizazi hiki aliyefikia hata robo ya Dr. Remmy (kwa mfano) anakucheka!
Pamoja na dhuluma alizofanyiwa Saida anaendelea kuwa juu tangu nyakati zake na ahitaji promo za kitoto, muda utadhihirisha ukweli huu.
Ni kweli una lugha kali lakini uzuri ni kwamba, ukielewa mitusi iliyomo mle basi fahamu ushakuwa mtu mzima vinginevyo utaishia kudhani anazungumziwa ngongoti mwanadamu kumbe ngongoti mlingoti ukiwa unasoma network 101%!! Tena Raymond ndo kazidi kumwaga mitusi sema the kid is so smart... huwezi kujua kwamba sehemu kubwa ya mashairi yake ya verse ya kwanza ni mitusi tupu!!Una lugha kali sana.
Na hii dabate itaendelee kwa muda mrefu lakini mwisho sote tutajua kuwa Saida ndiye alikuwa na kipaji na ndio maana huyu Muta hajamtoa msanii mwingine baada ya hapo ...kama kweli ni 'professional promoter'!?Felician Mutta alikuwa gaidi kwenye sanaa, we acha tu! Siku nasikia Saida maisha yake ni ya kawaida sana; sikutaka kuamini! Nyomi la pale Taifa lilikuwa linajirudia kila sekunde... huyo ndo Mzee Mutta bhana!! Aka-take advantage ya ushamba wa Saida kumnyonya hadi rojo za kwenye mifupa!!!