Tetesi: Salim Abdallah ‘Try Again’ katika jaribio la kumng’oa Mo Dewj Simba!

Nguvu ya Yanga ipo kwa mashabiki na wapenzi wa timu, nguvu ya Simba ipo kwa boss. Miaka michache ya nyuma Yanga ktk dhiki alipambana akabaki top 2, ule upepo angepita Simba angekuwa 4 au 5 huko.

Ni kweli SSB ataleta ushindani mkubwa sana ila bado atakutana na kigingi cha wananchi kwa uzito.
Mkuu, SSB akikabidhiwa Simba pale akafanya uwekezaji wa maana zikiwemo sajili makini itakuwa balaa.

Sasa hivi Yanga tunatamba sababu ya uwekezaji aliofanya GSM ikiwemo uongozi makini, ukiviondosha hivyo Yanga sio lolote.
 
Taarifa hizi nilizisikia miezi miwili iliyopita, kile kikao kilifanya kinyume na maagizo ya serikali ambayo yalitaka Simba irekebishe katiba yake maana hii iliyopo imempa mo madaraka makubwa.
Katikat kile kikao Kuna fujo zilitokea, Ila waandishi walipewa bahasha hawakuripoti.
Ukiona waandishi wanaanza kusema ukweli kuhusu utapeli wa mo ujue Kuna nguvu kubwa nyuma yake maana mo ni mjanjajanja anajua namna ya kucheza na waandishi.
Mchakato mpya ukianzishwa tu Mo hana chake pale Simba, hizo janjajanja mwisho wake ni huo mchakato.
 
Taarifa hizi nilizisikia miezi miwili iliyopita, kile kikao kilifanya kinyume na maagizo ya serikali ambayo yalitaka Simba irekebishe katiba yake maana hii iliyopo imempa mo madaraka makubwa.
Katikat kile kikao Kuna fujo zilitokea, Ila waandishi walipewa bahasha hawakuripoti.
Ukiona waandishi wanaanza kusema ukweli kuhusu utapeli wa mo ujue Kuna nguvu kubwa nyuma yake maana mo ni mjanjajanja anajua namna ya kucheza na waandishi.
Washabiki wa simba ndo wajinga
Kipindi kile mzee kilimon alipiga sana kelele ila akaonekana ni mamluki na anayeitakia simba mabaya

Na washabiki wa simba hawakutaka kusikia chochote sababu walikua katika mafanikio
Taratibu za asilimia 49 za wawekezaji wanatakiwa kuwa watatu na sio mmoja tokea mwanzon ilikua inajulikana ila kwa sababu simba walikua kwenye mafanikio hukuwaambia kitu

Hata swala la uwanja wa bunju kuitwa mo arena lililamikiwa na mzee kilomon ila alioneka mamluki
Ila ukweli ni kwamba yule mzee aliona mbali sana

Sasa leo mnaimba nyimbo zile zile mzee kilomoni aliyeziimba miaka sita nyuma na akaonekana hamnazo
 
Washabiki wa simba ndo wajinga
Kipindi kile mzee kilimon alipiga sana kelele ila akaonekana ni mamluki na anayeitakia simba mabaya

Na washabiki wa simba hawakutaka kusikia chochote sababu walikua katika mafanikio
Taratibu za asilimia 49 za wawekezaji wanatakiwa kuwa watatu na sio mmoja tokea mwanzon lilikua linajulikana ila kwa sababu simba walikua kwenye mafanikio hukuwaambia kitu

Hata swala la uwanja wa bunju kuitwa mo arena lililamikiwa na mzee kilomon ila alioneka mamluki
Ila ukweli ni kwamba yule mzee aliona mbali sana

Sasa leo mnaimba nyimbo zile zile mzee kilomoni aliyeziimba miaka sita nyuma na akaonekana hamnazo
Mzee Kilomoni anatakiwa kujengewa sanamu ya heshima pale Simba.

Hivi unafikiri mpaka kufikia mtifuano ule Mo alishampa ofa kubwa kiasi gani lakini akaendelea na msimamo wake huku akizishikilia hati?
Kama kuna shabiki mzalendo pale Simba ni Mzee Kilomoni.
 
......sijajua ni ipi nafasi ya mashabiki na wanachama hai wa simba katika kuamua mustakabali wa timu, au wamnachukuliwa kama mazuzu tu means hawana impact, baada ya Ferguson kuondoka na timu kuyumba familia ya Glazer imekuwa kwenye pressure kubwa, na jitihada zao kupambania timu zinaonekana licha ya kwamba bahati haipo upande wao.....
.......mashabiki hawawazi kupata pesa wanataka timu bora, Sasa hiyo battle onaonekana wazi hailengi kusaidia timu na ndo maana ni 'pesa against power' na sio matamanio ya mashabiki, hivyo basi kwa kuwa pesa=power basi yeyote atakaeshinda hapa usitegemee atakaa ashughulikie changamoto za simba sc, hili litapita na matatizo yatabaki palepale.......
 
Hii imekaa sawa
Mmiliki wa Azam ni mtoto
Miliki wa simba muwekezaji ni baba (kama atakuwa) sizani kama kuna shida

Ni kama umiliki wa timu za taasisi
Timu za jkt
Timu za jwtz huko daraja la kwanza zimejaa
Timu za polisi zipo polisi dom, polisi moro, polisi dsm
Magereza pia wanazo mikoani kama magereza musoma

Timu za halmashauri kama ilivyokuwa timu za kurugenzi (wakurugenzi wa halmashauri)

Timu za ujenzi

Timu za shirika moja la relic Yani reli kigoma, reli morogoro

Nazani kwetu ni kawaida

Pia ndg kumiliki timu ni jambo la kawaida, pale Congo dr kuna Katumbi na ndg yake wana miliki timu na zipo Ligi kuu

Salzburg RB, RB reipzig na RB zingine ni mifano ya umiliki wa taasisi moja au shabihishi
Hii imekaa sawa kama mtoto ndo mmiliki
 
......sijajua ni ipi nafasi ya mashabiki na wanachama hai wa simba katika kuamua mustakabali wa timu, au wamnachukuliwa kama mazuzu tu means hawana impact, baada ya Ferguson kuondoka na timu kuyumba familia ya Glazer imekuwa kwenye pressure kubwa, na jitihada zao kupambania timu zinaonekana licha ya kwamba bahati haipo upande wao.....
.......mashabiki hawawazi kupata pesa wanataka timu bora, Sasa hiyo battle onaonekana wazi hailengi kusaidia timu na ndo maana ni 'pesa against power' na sio matamanio ya mashabiki, hivyo basi kwa kuwa pesa=power basi yeyote atakaeshinda hapa usitegemee atakaa ashughulikie changamoto za simba sc, hili litapita na matatizo yatabaki palepale.......
Sasa Mkuu, Kama Mangungu ambaye ndiye Mwenyekiti wa Simba akiwakilisha wanachama hana sauti katika vikao, yeye kazi yake ni kufungua na kufunga vikao unategemea nini?
 
Sasa Mkuu, Kama Mangungu ambaye ndiye Mwenyekiti wa Simba akiwakilisha wanachama hana sauti katika vikao, yeye kazi yake ni kufungua na kufunga vikao unategemea nini?
........huko kukosa kwake sauti ndo kunaongeza tatizo au kuzua maswali zaidi, ina maana hisa za wanachama zinaweza kuwa hewa au tunaweza kuquestion upatikanaji wake kama mwenyekiti, lakini ukiachana na Ngungu boy je wanachama by themselves wanaweza kufanya kitu eg kugomea kwenda uwanjani au hata kutishia kurudisha kadi au kususia jezi za msimu mpya etc, inasemekana mashabiki wa upande wa pili hawanaga mzaha timu ikiwa down,.....
 
Hapana Mkuu, hii sio propaganda ni habari ya ukweli kabisa.
Na huyo mtu ambaye ni chanzo changu ni mwanachama hai wa Simba mwenye access na taarifa za ‘ndani’ huko kwenye klabu yao.
Mulikuwa wapi na Ulimpa nini hadi akupenyezee habari nyeti kama hizo?

".............Delila kwa Samson............"
 
View attachment 2966280

Moto unawaka SSC! Ni vita kubwa!
Klabu ya Simba ipo katika kipindi kigumu cha vita inayozidi kukomaa kila uchwao baina ya Mwenyekiti wa bodi ya Wakurugenzi ya Simba Salim Abdallah Muhene ‘Try Again’ dhidi ya ‘Rais wa heshima’ wa Simba Mohamed ‘Mo’ Dewj.

Wawili hao walianza kukosa maelewano baada ya Mo Dewj kuhamisha makazi yake nchini ambapo taarifa za uhakika ni kwamba anaishi Dubai hadi hivi sasa.

Baada ya Mo Dewj kuhamisha makazi uwekezaji wake Simba ulisuasua, ikitaarifiwa kumuachia mzigo mkubwa wa uendeahaji timu Try Again ambao ulimuelemea!

Try Again alijitahidi kadiri ya uwezo wake baada ya ‘tajiri’ kujitenga ‘kiaiana’, akihaha huku na huko kutafuta namna ya kuinusuru Klabu ya Simba ambayo kwa msimu wa tatu mfululizo imekuwa na matokeo ya kusuasua. Jitihada zake hizo zikizaa matunda kwa kiasi kisichoendana na kipindi ambacho muwekezaji alikuwa ameshikilia usukani.

Try Again adhamiria mapinduzi, amlenga Said Salim Bakhressa!
Baada ya Try again ‘kususiwa’ timu na muwekezaji Mo Dewj, Try Again aliona uwezekano wa kupindua meza, na kama ilivyo ada ya wafanyabiashara wakubwa kuwa na jicho angavu la udhia, S.S Bakhressa hakusita kupenyeza rupia!

Vita kubwa iliyopo hivi sasa ni Try Again aliyeko kwenye mikakati thabiti ya kumpindua Mo Dewj kama muwekezaji kisha nafasi hiyo apewe muwekezaji asiye na ‘mbambamba’ S.S. Bakhressa, huku Mo Dewj nae akiwa katika mipango ya kujidhatiti kushikilia nafasi yake hiyo adhimu ambayo huitumia mara nyingi kama kielelezo cha mali zake (SSC)

Serikali yakoleza vita!
Hivi karibuni, Serikali imetoa agizo la kuanzishwa upya kwa mchakato wa undeshwaji wa kisasa kwa klabu ya Simba. Kama mtakumbuka vyema mchakato huo ulioanza miaka kadhaa nyuma, haukuwahi kukamilika.

Serikali imetoa agizo hilo baada ya kujidhihirisha kuwa mchakato wa awali ulikuwa na makosa mengi, hivyo ulikuwa batili ukikosa uhalali.

Agizo hilo limekuwa chachu kwa Try Again na timu yake, kwani endapo ukifanikiwa kuanza kuna uwezekano mkubwa wa S.S. Bakhressa na wawekezaji wengine kujitokeza na kushika hatamu katika hisa, huku ikielezwa kwamba Mo Dewj atarudishiwa fedha zake alizolipia katika mchakato huo uliohuishwa ambako alijitwalia hisa 49% za umiliki wa klabu ya Simba.

Mo Dewj atupa shilingi mechi ya Yanga!
Hii ni tahadhari kwa Klabu ya Yanga, Hersi na wenzio kama hamjaipata nawapa hii…

Mo Dewj amejipanga kuitumia mechi ya tarehe 20/04/2024 dhidi ya Yanga kama turufu yake ndani ya Simba.

Mo Dewj ambaye inaarifiwa ametenga fungu ‘nono’ kuhakikisha Simba inashinda mechi hiyo, amejipanga sawia na mkakati wake huo ambao tayari ameshaanza utekelezaji.

Mkakati huu wa Mo ni kwamba endapo Simba ikishinda mechi hiyo, atafanikiwa kurudisha imani na mapenzi kwa mashabiki, hivyo kutumia hilo kama zengwe la kuwang’oa Try Again na Mangungu pale Simba.

Kila mmoja ana mpango kazi!
Try Again ambaye hapo awali alitumia ‘janja janja’ kuwang’oa aliyekuwa CEO wa Klabu bibie Barbara na Rweyemamu ambaye alikuwa meneja wa timu kwa ‘kuwachonganisha’ na muewekezaji Mo Dewj, anahaha kulinda maslahi yake kwani endapo Mo Dewj akishinda vita hii (Kwa Simba kushinda dhidi ya Yanga) amepanga kuwarejesha Barbara, Rweyemamu ambaye hivi sasa yupo Kikosi B na aliyekuwa Mkurugenzi wa bodi ya wawekezaji ambaye alijiengua Nkwabi.

Try Again ambaye wameungana na Mangungu kumuhujumu Mo Dewj, nao hawako nyuma. Wanatumia turufu yao ya ‘ujanja wa mjini’ kuhakikisha Mo Dewj anang’oka Simba kwa namna yoyote!

Inaarifiwa hata agizo la kuanza upya kwa mchakato wa uendeshaji wa kisasa wa timu umechagizwa na ‘connection’ za Try Again pamoja na S.S.B na mpaka hivi sasa mpango wao ‘umetiki’.

Je, nani ataibuka mshindi katika vita hii? Ni ‘watoto wa mjini’ Salim Abdallah, Try again au tajiri Mo Dewj?

Ni mimi na chanzo changu nyeti,

Nifah.
Kuna wakati nilikuwa nikitamani kuona threads za michezo zikiwa zinaandikwa kwa weledi namna hii, bila kujaza unazi na ushabiki.

Hongera sana Nifah, umelipa heshima jukwaa na michezo. Umeandika vizuri sana na kufafanua kwa kina hadi nikasahau kama wewe ni Yanga.

Ni kweli Simba tuko kwenye tatizo la kiuongozi na sioni namna nzuri ya utatuzi, kando ya mbinu nyingi za kukomoana na kuonesha umwamba.

Ova
 
........huko kukosa kwake sauti ndo kunaongeza tatizo au kuzua maswali zaidi, ina maana hisa za wanachama zinaweza kuwa hewa au tunaweza kuquestion upatikanaji wake kama mwenyekiti, lakini ukiachana na Ngungu boy je wanachama by themselves wanaweza kufanya kitu eg kugomea kwenda uwanjani au hata kutishia kurudisha kadi au kususia jezi za msimu mpya etc, inasemekana mashabiki wa upande wa pili hawanaga mzaha timu ikiwa down,.....
Hicho ndicho kilichofanya serikali iagize kurudiwa upya kwa mchakato baada ya kuonekana Mo amejitwalia madaraka makubwa Simba kuliko wanachama ambao ndio wenye hisa nyingi.

Sisi Yanga huwa hatuna mchezo, si unakumbuka kilichomleta Mzee Mpili town kutokea Ikwiriri ni nini? Alikuja kukiwasha baada ya kuona kuna watu wanafanya mchezo timu haisongi mbele ilhali GSM anaweka pesa.
 
Mulikuwa wapi na Ulimpa nini hadi akupenyezee habari nyeti kama hizo?

".............Delila kwa Samson............"
We ni mgeni kwenye habari ninazozileta hapa? Mbona kanipenyezea nyingi tu?

Nimempa moyo wangu.
 
Kuna wakati nilikuwa nikitamani kuona threads za michezo zikiwa zinaandikwa kwa weledi namna hii, bila kujaza unazi na ushabiki.

Hongera sana Nifah, umelipa heshima jukwaa na michezo. Umeandika vizuri sana na kufafanua kwa kina hadi nikasahau kama wewe ni Yanga.

Ni kweli Simba tuko kwenye tatizo la kiuongozi na sioni namna nzuri ya utatuzi, kando ya mbinu nyingi za kukomoana na kuonesha umwamba.

Ova
Mwandishi bora ni yule anayeficha mapenzi yake binafsi katika maandishi yake. Nimejifunza haya kutoka kwa mwalimu bora, bado najifunza vingi kutoka kwenye kapu lake lisokwisha maarifa.

Asante b… hii kutoka kwako ni zaidi ya pongezi.
Nashukuru.
 
Washabiki wa simba ndo wajinga
Kipindi kile mzee kilimon alipiga sana kelele ila akaonekana ni mamluki na anayeitakia simba mabaya

Na washabiki wa simba hawakutaka kusikia chochote sababu walikua katika mafanikio
Taratibu za asilimia 49 za wawekezaji wanatakiwa kuwa watatu na sio mmoja tokea mwanzon ilikua inajulikana ila kwa sababu simba walikua kwenye mafanikio hukuwaambia kitu

Hata swala la uwanja wa bunju kuitwa mo arena lililamikiwa na mzee kilomon ila alioneka mamluki
Ila ukweli ni kwamba yule mzee aliona mbali sana

Sasa leo mnaimba nyimbo zile zile mzee kilomoni aliyeziimba miaka sita nyuma na akaonekana hamnazo
Mbona unakwepa kujadili hoja iliyopo, unaweza kufungua uzi mwingine wa hoja yako.
 
Back
Top Bottom