Salamu za Shukrani kwa Wanachama wa JamiiForums

Salamu za Shukrani kwa Wanachama wa JamiiForums

JamiiForums

JF Official Account
Joined
Nov 9, 2006
Posts
6,240
Reaction score
5,658
Kufuatia zuio lililotolewa Septemba 6, 2025 na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ikisitisha leseni ya utoaji maudhui nchini humo kupitia Jukwaa la JamiiForums kwa siku 90, member wa JF, Mshana Jr alianzisha uzi (https://www.jamiiforums.com/threads/tusimame-na-jf-yetu-kipindi-hiki-kigumu.2387883/) kuhamasisha wanachama na wapenzi wa JF kuungana nasi katika kipindi hiki.

Mpaka kufikia leo Septemba 27, 2025 tumepokea kiasi cha Tsh. 233,603.00/-

Tunatoa shukrani zetu za dhati kwa kila aliyejitoa kuungana nasi kwa salamu za pole, kuchangia na hata kuwa nasi kwa njia ya maombi wakati huu JamiiForums imezuiwa kutoa huduma zake nchini Tanzania.

Tunathamini sana umoja na mshikamano mliotuonyesha na mnaoendelea kutuonyesha🙏.
 
Of course let say members 15k wangedonate 500 jf ingepata 7.5M

hili zoezi linatakiwa kurudiwa kwa uzito kidogo.
Zoezi lilifanyika kienyeji sana. Watu waliomba ufafanuzi wakaishia kubezwa na kutukanwa (cc. The Icebreaker). Mello au mods ye yote angejitokeza na kutoa ufafanuzi mbona watu wangechanga tu? Mtu kujifanya anajua kila kitu yeye ndo yeye kwenye mambo yanayohusu charity is a big no.

Zoezi lirudiwe!
 
Zoezi lilifanyika kienyeji sana. Watu waliomba ufafanuzi wakaishia kubezwa na kutukanwa (cc. The Icebreaker). Mello au mods ye yote angejitokeza na kutoa ufafanuzi mbona watu wangechanga tu? Mtu kujifanya anajua kila kitu yeye ndo yeye kwenye mambo yanayohusu charity is a big no.

Zoezi lirudiwe!
Wangetoka front
kama jinsi wamelete huu uzi wa shukrani angalao ingeleta mantiki kwa kiasi flani
 
Pongezi sana kwa Mshana. Ila hayo makusanyo yanaashiria watu hawana imani na Mshana. Pia ni wazi kuwa kwenye jambo muhimu watu huingia mitini.

Kwenye uzi wa Mshana(ambaye umempa pongezi kwenye uzi huu wa shukurani) ulimpa dislike kwenye post yake

Kitaalamu sijajua ni nini hii
Screenshot_20250927-103529_Samsung Internet.jpg
 
Back
Top Bottom