Just Pray
JF-Expert Member
- Nov 7, 2023
- 2,142
- 4,777
Sakata la kupingwa kwa mtiania wa urais wa ACT Wazalendo, Luhaga Mpina limefika Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, huku chama hicho kikitakiwa kutoa maelezo kwa ofisi hiyo kesho Jumatano Agosti 20, 2025.
Mzizi wa hilo, ni barua iliyoandikwa na Katibu Mwenezi wa ACT Wazalendo Mkoa wa Dar es Salaam, Monalisa Ndala akipinga kupitishwa kwa Mpina kuwa mgombea urais, kwa kile alichosema ni kinyume na kifungu cha 16(1)4)I cha kanuni za kudumu za uendeshaji chama toleo la mwaka 2015.
Kwa mujibu wa kanuni hiyo, mwanachama anayewania nafasi ya urais kupitia chama hicho, anapaswa kuwa mwanachama wa zaidi ya siku saba.
Alipotafutwa kuzungumzia hilo, Naibu Katibu wa Mawasiliano, Uenezi na Mahusiano kwa Umma wa ACT Wazalendo, Shangwe Ayo amesema hayuko tayari kulizungumzia hilo.
Awali, alitafutwa katibu mkuu wa chama hicho, Ado Shaibu, simu yake iliita bila majimbu. Vivyo hivyo kwa Makamu Mwenyekiti wa chama hicho bara, Issihaka Mchinjita.
Mpina alijiunga na chama hicho Agosti 5 na Agosti 6, 2025 akapitishwa na mkutano mkuu uliofanyika ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam kuwa mtiania wa urais wa chama hicho.
Tayari Mpina amekabidhiwa fomu ya kuomba kuteuliwa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) na anaendelea kutafuta wadhamini wasiopungua 200 kila mkoa katika mikoa 10 ikiwemo miwili ya Zanzibar.
Chanzo, Mwananchi
Mzizi wa hilo, ni barua iliyoandikwa na Katibu Mwenezi wa ACT Wazalendo Mkoa wa Dar es Salaam, Monalisa Ndala akipinga kupitishwa kwa Mpina kuwa mgombea urais, kwa kile alichosema ni kinyume na kifungu cha 16(1)4)I cha kanuni za kudumu za uendeshaji chama toleo la mwaka 2015.
Kwa mujibu wa kanuni hiyo, mwanachama anayewania nafasi ya urais kupitia chama hicho, anapaswa kuwa mwanachama wa zaidi ya siku saba.
Alipotafutwa kuzungumzia hilo, Naibu Katibu wa Mawasiliano, Uenezi na Mahusiano kwa Umma wa ACT Wazalendo, Shangwe Ayo amesema hayuko tayari kulizungumzia hilo.
Awali, alitafutwa katibu mkuu wa chama hicho, Ado Shaibu, simu yake iliita bila majimbu. Vivyo hivyo kwa Makamu Mwenyekiti wa chama hicho bara, Issihaka Mchinjita.
Mpina alijiunga na chama hicho Agosti 5 na Agosti 6, 2025 akapitishwa na mkutano mkuu uliofanyika ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam kuwa mtiania wa urais wa chama hicho.
Tayari Mpina amekabidhiwa fomu ya kuomba kuteuliwa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) na anaendelea kutafuta wadhamini wasiopungua 200 kila mkoa katika mikoa 10 ikiwemo miwili ya Zanzibar.
Chanzo, Mwananchi