EvNich
Senior Member
- Mar 29, 2014
- 135
- 37
Mzee Arfi mwenyewe kwa muda wote aliokuwa Madarakani hajawahi kusema katiba ni mbovu.Amekuja kuiona mbovu baada ya kufukuzwa kiaina Umakamu Mwenyekiti.Mtu kama huyu anatumika na wala hastahili kueleweshwa chochote kwa hiyo unamwonea bure Nicholas.
Mimi nikiona nalalamikiwa na watu zaidi ya watatu siwezi kuthubutu kusema wao ndio wana makosa na mimi ni sahihi, kwani wamezaliwa na mama mmoja? pengine tatizo linaanzia kwangu na sikubali kushindwa. Haya mambo yakiendelea hivi ni kila mtu atashindwa kukitetea chama chenyewe. Na ukiona watu wanajitahidi kukikosoa ni kwa vile kilifikia hatua nzuri na hawataki kurudi kuanza mwanzo na kingine. Ila hata tufanye nini kuna kinachoendelea kule juu ambapo walio wengi chini hawaridhiki na wanashindwa kuchukua uamuzi, kwa vile hawajui hatima yao. Kadri wanavyopungua waliochanganya Imani zao na Makabila yao ndani ya kilichowahi kusemwa ni chama cha Kabila fulani na Imani fulani, ndivyo ambavyo na Usemi huu utazidi kukamilika. Hofu yangu ni kama mambo yataendelea hivi ya kulazimishana tusishangae Chama hiki kikatumika kama Kikundi kitakachopingana na Serikali hapo baadaye. Tunaposema hivi ni kwa vile tunaijali nchi na wao tunapenda wawe wawazi na wakajirekebisha.