Mibunge yote ambayo huwa inapata bahati ya Kuwa mawaziri kutokea Mkoa wa Mara,huwa ni hovyo!
1.STEVEN MASATU WASIRA
Huyu yeye amekuwa Mbunge wa Bunda Miaka ya kutosha,Aliwahi Kuwa Waziri wa Kilimo & Maji
Tulitegemea watu wa Mara hakikishe anasaidiana na wadau wa maendeleo,wawekezaji na kuibana serikali ili kufufua viwanda vilivyokufa Ili watu na Vijana wa Mkoa wa Mara wapate Ajira,Ajabu viwanda vyote vya kuchakata Pamba (Jineri),Viwanda vya Samaki,Viwanda vya nguo (Mutex) amevikuta kama vilivyo na kaondoka kaviacha kama vilivyo!
Akiwa Waziri wa maji,Bunda haikuwahi Kuwa na maji hadi Leo,angalau kipindi Cha Esther Bulaya akiwa Mbunge watu wa Bunda waliopata maji ijapokuwa nayo yanatoka mara moja Kwa mwezi na wakati ziwa liko umbali WA km 5 tu !
Kazi ya WASIRA muda wote imekuwa kuisema CHADEMA kuliko kuwasemea watu wa Mara ambao wamezungukwa na Utajiri usiowanufaisha !
2.KANGI LUGOLA KANGI
Huyu yeye alikuwa ni Mbunge wa Jimbo la Mwibara,Mwibara ni Jimbo ambalo liko ndani ya wilaya ya Bunda,lakini pamoja na fursa hiyo ya uwaziri aliyoipata,Mwibara Iko ziwani kabisa lakini wananchi wake wanayaangalia maji Kwa macho tu !
Alichotumwa na wananchi hakukifanya ila akafanya asichotumwa na wananchi,Alikuwa mjuzi wa kukata viuno stejini huku waliopaswa kukata viuno wakimshangaa !,Haikuchukua muda Magufuli naye akamla kichwa,nadhani aliona hamna shughuli !
3.SOSPETER MUHONGO
Huyu yeye amekuwa Mbunge wa Musoma vijijini Kwa kipindi Cha miaka takribani 10,Pia Kwa kipindi hicho amekuwa Waziri ,Ajabu ni kwamba,ukienda Musoma vijijini Kuna Nuka shida,Jimbo la Musoma Vijijini ni Jimbo ambalo linazungukwa na ziwa lakini watu wake hawana maji safi na salama,Kuna migodi lakini wananchi wanauishi umasikini Kwa Vitendo,barabara kutoka Musoma mjini kuelekea Musoma Vijijini (Majita road) ni vumbi mwanzo mwisho !
4.JUMANNE SAGINI ABDALLAH
Huyu yeye hakuna alichofanya hapo Butiama zaidi ya kulembua uso,Aliyekuwa Mbunge wa Butiama ambaye Sasa ni Marehemu (Nimrod Mkono) amefanya mambo makubwa sana hapo Butiama enzi zake ukilinganisha na Hawa ambao wamepewa na uwaziri kabisa,Nimrod alikuwa Mbunge wa kawaida tu lakini aliibadili Butiama kuliko huyo SAGINI !
Mkoa wa Mara una bahati ya kupata mawaziri lakini tatizo hawaelewi wanachopaswa kufanya !
Mkoa wa Mara umezungukwa na mbuga maarufu ya Serengeti ,ajabu ni kwamba,watu wa Arusha na Viunga vyake ndio wanaonufaika na Serengeti kuliko Wana Mara wenye mbuga yao!
Kutoka Arusha to Serengeti ni umbali wa km 383
Kutoka Musoma Mjini to Serengeti Via Butiama ni km 129 (Kupitia gate la Natta/fort ikoma)
Kutoka Musoma mjini to Serengeti Via Bunda ni Km 87 (Ndabaka gate)
Musoma Kuna uwanja wa ndege ambao umekuwa ukitumika miaka yote,Ajabu ni Kuwa hao mawaziri mizigo wao kukaa chini na wadau wa utalii kushirikiana na wafanya biashara Ili Kuja na mkakati wa pamoja wa kukuza utalii ndani ya Mkoa wa Mara,wameshindwa!
Mtu kama WASIRA hajawahi kusikika mahali popote akiuongelea Mkoa wa Mara na kuzieleza fursa za kiuwekezaji!
Kazi yake kubwa ukimsikia ni kuiongelea CHADEMA tu na kuipiga Vijembe !,Anasahau kazi anayopaswa kuifanya Kwa ajili ya Wana Mara!