Safarini NGENDE

Safarini NGENDE

SIMBA mtoto

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2011
Posts
204
Reaction score
100
Natarajia kusafiri kwenda Newala, kusudi la safari yangu ni kufika kijiji cha Ngende kutafuta bahati ya kimaisha.
Taarifa za awali nilizozipata ni za kutisha sana, na hatari yake ni kubwa sana hadi ufike kwenye hicho kijiji.

Taarifa zinasema jaribio la kwanza ni muda utakaotumia hadi ufike kijijini na kutoka hicho kijiji ufike kwenye shimo wanakokaa hao waungwana, kuna umbali wa kilomita 12 lakini ukiwa ngangari sana itakuchukua siku tano kufika shimoni.

Jaribio la kwanza ni jinsi ya kuwapita simba luwala waliotapakaa njiani, jaribio la pili ni kumpata mwenyeji wa kukubali kukupeleka huko ukimpata dau lake ni kubwa na hatakufikisha atarudia njiani, jaribio la tatu baada ya kuwapita simba ni majoka ya kutisha utakayokutana nayo, ukiwapita hayo majoka utauona mlima mkubwa mbele yako na chini yake ndipo lilipo lango la kuingilia shimoni.

Taarifa zinasema, mara tu unapokaribia lango, huwa anajitokeza mwanamama mmoja mrefu sana, naye ana jicho moja, wanasema huyo mama ni mzee sana, lakini ana maguvu ya kumnyanyua tembo na kumtupa chini na ni mkali ajabu. Wanasema unaweza kukaa hapo mlangoni siku moja hadi mbili ukihojiwa na kufanyizwa kazi za usafi, kisha unapewa mashariti ya kuingia shimoni....

Jamani naenda Ngende, nimepigika kimaisha, maisha bora kwa kila mtu yamenipitia mbali, naenda Ngende, walioenda na kurudi na mafanikio nipeni maujanja wa kwenda Ngende.


images
images
 
kwa hiyo umeshindwa kabisa kutafuta maisha kwa nji halali?mpaka uende huko?mimi nakushauri usiende huko,utaikosa pepo.
 
walioenda kwenye ushirikina hawaongei hadharani eidha utaona mafainikio ya ajabu (ya mapepo) ama utaishia kukaa kimya kwa kujutia ujinga wako, mwisho ngende haipo newala umebugi
 
Duh...!! Kumbe utajiri unapatikana huko?
 
Utajiri wa Ngende ni ushirikina ambao ukikiuka masharti yake lazima ufe!
 
Hii ni paukwa......


Palitokea........ kajenga nyumba kaa!

Jibu lake......... Ngende wote matajiri?
 
Kuna njia rahis yakufika hata bila kupitia kwenye Simba na Majoka, ni PM mm nausafiri rahisi sana ila naomba kabla hatujaonana nitafutie 5L ya damu kutoka kwa mtoto asiezid miezi 3. Fanya haraka wanaofanya booking ni wengi sana.

Sent from my BlackBerry 9360 using JamiiForums
 
Back
Top Bottom