Undava King
JF-Expert Member
- Aug 11, 2017
- 3,205
- 5,332
'Leo ntazungumzia mada tata kidogo ya kifo maana kamwe hata mwanasayansi hawezi thibitisha undani wake si kwa sababu haiwezekani la hasha hakuna aliye tiyari kutangulia na madamu ukienda huko ndo basi tena atukuoni daima'
"..Ila msiwe na mashaka ntawapa facts ambazo mtazithibitisha siku mkikubali kuongoza njia kadri ya mlivyoamini, nilifanikiwa kwenda huko ila kama wengine sikukubali kuondoka mazima bali nilikataa kutokurudi hivyo sikufika huko niliupenda ugali wangu hata nikalazimisha matokeo chanya nikarudi.."
Unapoongelea kufa kila mtu aliye-hai anafahamu ni nini kimemaanishwa ila siri juu ya experience ya kufa na nini kinamkumba mwanadamu au kiumbe baada ya kufa imebaki kuwa siri kubwa isiyoweza elezwa kwa muktadha wa kawaida leo najitoa kimasomaso kuyafumbua macho ya wote wenye fikra chanya na nyumbulifu kwa maana si mchoyo ningeamua kuiuza siri hii ningeliuza kwa fedha nyingi kupitia vitabu na majarida bali nipo hapa kuwapa bure kile nijuacho.."
Kifo uanza na dalili kwa muhusika, siku ya tukio itategemea na muhusika(mtarajiwa marehemu) yupo mahala gani yaweza kuwa kalala,anatembea,anasafiri au yupo ofisini nakadhalika.
Cha kwanza kunakuwapo na msukumo wa nguvu katika fikra na mwito fulani anaohisi muhusika siku hiyo mfano kujihisi mzito kwenda mahali,kama ni mgonjwa kutojisikia kuomba tena au kumeza dawa au kutumaini zaidi na badala yake kujisikia nafuu ghafla nakuitaji kuongea maneno yafaraja au siri halizotunza moyoni muda mrefu kwa wale awapendao zaidi(usia) n.k,,
Kukatazwa lakini asikii kutofanya jambo yaani siku hiyo ni lazima afanye tu alichokusudia,,kujikwaa kwaa,kupaliwa,kujing'ata,kutojisikia vizuri siku hiyo kama kuna jambo aliendi sawa,mtu kuota kuwa utakufa au kuongelea kifo chako kiutani, au kufanya jambo ila unahisi ni kama leo ndo mwisho na haitojirudia tena,moyo kuuma au mapigo yamoyo kukuenda mbio pasipo kawaida n.k
Kama utakufa ukiwa katika hali ya utulivu na amani yaani pengine umelala au wakati unaugulia kitandani na siyo kifo cha mazingira magumu au cha ghafla, basi utaanza na tukio la kuona kuwa muda wa kuaga umewadia hapa ndoto na fikra halisi uungana pamoja kuwa kitu kimoja hivyo wahisi unawaona waliokizunguka kitanda chako(wanakuuguza) pasipo kuwa macho kuwa wapo katika ndoto yako na ni lucid,
hapo utamwagizia yule utakayekumwona aletwe uongee nae kwa maana ya kumuaga maana kuna kitu kinakwambia wakati umewadia tazama hata macho yako sasa umeyafumbua lakini yameshafumbwa,
hapo ndipo unapoianza safari ndefu sana yakuondoka katika dunia hii yumkini utaniuliza naelekea wapi sasa? vizuri! utaelekea kule tu ulipopeleka mboga, je ninamaana gani kusema hivyo?
Kama wewe ni muumini wa dini za dunia hii na waamini katika imani zake basi tambua kuwa waabudu (..........) hivyo utarudi katika (......…..) za imani yako, usiniulize kwa wale wasiyo waamini kuwa wao wataelekea wapi kwa maana hata mimi sijuhi...
kwa kuwa kifo si jambo dogo ni hatua kubwa kutoka duniani kwenda umbali mrefu usio wa damu na nyama utaanza kwanza kwa kuyaona maji mithili ya tope jeusi ukianza kuyakanyaga nakuondoka ukiacha footprints(wajanja wenye siri hii ukuonesha kwenye muvi na miziki kama burudani)
kila kitu uonekana kikikupisha kwa kurudi nyuma kwa kasi hapa unaanza kuhisi kichefuchefu,hali yakuitaji kunywa maji ili usikabwe kwa kuhisi hewa inapungua na tazama mbele yako nuru uondolewa na kiza tupu uzidi kutanda(waliohai ukuona ukipumua kwa shida nakujinyonganyonga)
Hapo sasa tiyari hauko duniani bali wapambania kubaki au kuondoka kuna nguvu mithili ya usumaku ukuvuta kwa nguvu kuelekea usipoweza paelewa mara moja kuwa ni wapi hapa utakuwa unajitambua kuwa upo mwenyewe na upo kwenye giza totoro ukisikia milio ya mivumo ya pepo na viumbe vya anga hakika inatisha(kitandani pale watakuona katika uso ukiweweseka)
Fikra zitakutuma u-focus mbele na safari yako na usisite kwenda kwa kuwa nguvu zinazidi kukuvuta uende natazama pindi utakaporuhusu roho itizame mbele utaona pale imani yako uliyokuwa ukiitumainia ukiwa duniani ilipo,
Yakuwa ni mbali mno mara haielezeki na bado sharti lazima uende hivyo woga hapa huwa hauzuiliki utataka kurudi nyuma(ndiyo maana wengine uchoma mahiti kabisaa kuepuka tatizo hili au kuna visa vya mtu kurejesha uhai na kugonga jeneza tiyari anazikwa n.k japo ni nadra sana kupingana na nguvu hizi mpaka kurudi tena)na kwa bahati mbaya nafasi hiyo huna tena(mara zote wanadamu wote wakifikia hapa ukunja sura kwa maumivu au taamaki yakuondoka kuifata njia hii isiyo na mwisho)
Ni sawa na hadithi yako ya ndoto ukiwa mtoto unapoota kudumbukia kwenye shimo jeusi refuu sana hivyo ile experience ujirudia tena wakati huu isipokuwa hapa uwezi shituka tena kutoka katika usingizi huu bali nguvu za usumaku-sumaku zitakuzidia ujanja nakukuvutia katika anga tupu kuendelea na safari kuelekea kwenye destination ambayo ni display pekee unayoiona mbele yako kama tumaini nje ya giza hili totoro..."
sasa je, huko unakoelekea utafanikiwa kufika au utaendelea kusafiri daima? hilo sijuhi maana nshakwambia nilikomea njiani kwa kutetea pumzi yangu.."
NB: Mahali nilipoweka (........) ina maana sijataka iwe ni sehemu ya mjadala au kuzua taharuki kwa maana hiyo pia ni siri kuu iliyolindwa kwa miaka maelfu kwa maelfu kwa nia nzuri mimi ni nani hata niizungumzie? hivyo naomba nisiulizwe juu ya hilo.
"..Ila msiwe na mashaka ntawapa facts ambazo mtazithibitisha siku mkikubali kuongoza njia kadri ya mlivyoamini, nilifanikiwa kwenda huko ila kama wengine sikukubali kuondoka mazima bali nilikataa kutokurudi hivyo sikufika huko niliupenda ugali wangu hata nikalazimisha matokeo chanya nikarudi.."
Unapoongelea kufa kila mtu aliye-hai anafahamu ni nini kimemaanishwa ila siri juu ya experience ya kufa na nini kinamkumba mwanadamu au kiumbe baada ya kufa imebaki kuwa siri kubwa isiyoweza elezwa kwa muktadha wa kawaida leo najitoa kimasomaso kuyafumbua macho ya wote wenye fikra chanya na nyumbulifu kwa maana si mchoyo ningeamua kuiuza siri hii ningeliuza kwa fedha nyingi kupitia vitabu na majarida bali nipo hapa kuwapa bure kile nijuacho.."
Kifo uanza na dalili kwa muhusika, siku ya tukio itategemea na muhusika(mtarajiwa marehemu) yupo mahala gani yaweza kuwa kalala,anatembea,anasafiri au yupo ofisini nakadhalika.
Cha kwanza kunakuwapo na msukumo wa nguvu katika fikra na mwito fulani anaohisi muhusika siku hiyo mfano kujihisi mzito kwenda mahali,kama ni mgonjwa kutojisikia kuomba tena au kumeza dawa au kutumaini zaidi na badala yake kujisikia nafuu ghafla nakuitaji kuongea maneno yafaraja au siri halizotunza moyoni muda mrefu kwa wale awapendao zaidi(usia) n.k,,
Kukatazwa lakini asikii kutofanya jambo yaani siku hiyo ni lazima afanye tu alichokusudia,,kujikwaa kwaa,kupaliwa,kujing'ata,kutojisikia vizuri siku hiyo kama kuna jambo aliendi sawa,mtu kuota kuwa utakufa au kuongelea kifo chako kiutani, au kufanya jambo ila unahisi ni kama leo ndo mwisho na haitojirudia tena,moyo kuuma au mapigo yamoyo kukuenda mbio pasipo kawaida n.k
Kama utakufa ukiwa katika hali ya utulivu na amani yaani pengine umelala au wakati unaugulia kitandani na siyo kifo cha mazingira magumu au cha ghafla, basi utaanza na tukio la kuona kuwa muda wa kuaga umewadia hapa ndoto na fikra halisi uungana pamoja kuwa kitu kimoja hivyo wahisi unawaona waliokizunguka kitanda chako(wanakuuguza) pasipo kuwa macho kuwa wapo katika ndoto yako na ni lucid,
hapo utamwagizia yule utakayekumwona aletwe uongee nae kwa maana ya kumuaga maana kuna kitu kinakwambia wakati umewadia tazama hata macho yako sasa umeyafumbua lakini yameshafumbwa,
hapo ndipo unapoianza safari ndefu sana yakuondoka katika dunia hii yumkini utaniuliza naelekea wapi sasa? vizuri! utaelekea kule tu ulipopeleka mboga, je ninamaana gani kusema hivyo?
Kama wewe ni muumini wa dini za dunia hii na waamini katika imani zake basi tambua kuwa waabudu (..........) hivyo utarudi katika (......…..) za imani yako, usiniulize kwa wale wasiyo waamini kuwa wao wataelekea wapi kwa maana hata mimi sijuhi...
kwa kuwa kifo si jambo dogo ni hatua kubwa kutoka duniani kwenda umbali mrefu usio wa damu na nyama utaanza kwanza kwa kuyaona maji mithili ya tope jeusi ukianza kuyakanyaga nakuondoka ukiacha footprints(wajanja wenye siri hii ukuonesha kwenye muvi na miziki kama burudani)
kila kitu uonekana kikikupisha kwa kurudi nyuma kwa kasi hapa unaanza kuhisi kichefuchefu,hali yakuitaji kunywa maji ili usikabwe kwa kuhisi hewa inapungua na tazama mbele yako nuru uondolewa na kiza tupu uzidi kutanda(waliohai ukuona ukipumua kwa shida nakujinyonganyonga)
Hapo sasa tiyari hauko duniani bali wapambania kubaki au kuondoka kuna nguvu mithili ya usumaku ukuvuta kwa nguvu kuelekea usipoweza paelewa mara moja kuwa ni wapi hapa utakuwa unajitambua kuwa upo mwenyewe na upo kwenye giza totoro ukisikia milio ya mivumo ya pepo na viumbe vya anga hakika inatisha(kitandani pale watakuona katika uso ukiweweseka)
Fikra zitakutuma u-focus mbele na safari yako na usisite kwenda kwa kuwa nguvu zinazidi kukuvuta uende natazama pindi utakaporuhusu roho itizame mbele utaona pale imani yako uliyokuwa ukiitumainia ukiwa duniani ilipo,
Yakuwa ni mbali mno mara haielezeki na bado sharti lazima uende hivyo woga hapa huwa hauzuiliki utataka kurudi nyuma(ndiyo maana wengine uchoma mahiti kabisaa kuepuka tatizo hili au kuna visa vya mtu kurejesha uhai na kugonga jeneza tiyari anazikwa n.k japo ni nadra sana kupingana na nguvu hizi mpaka kurudi tena)na kwa bahati mbaya nafasi hiyo huna tena(mara zote wanadamu wote wakifikia hapa ukunja sura kwa maumivu au taamaki yakuondoka kuifata njia hii isiyo na mwisho)
Ni sawa na hadithi yako ya ndoto ukiwa mtoto unapoota kudumbukia kwenye shimo jeusi refuu sana hivyo ile experience ujirudia tena wakati huu isipokuwa hapa uwezi shituka tena kutoka katika usingizi huu bali nguvu za usumaku-sumaku zitakuzidia ujanja nakukuvutia katika anga tupu kuendelea na safari kuelekea kwenye destination ambayo ni display pekee unayoiona mbele yako kama tumaini nje ya giza hili totoro..."
sasa je, huko unakoelekea utafanikiwa kufika au utaendelea kusafiri daima? hilo sijuhi maana nshakwambia nilikomea njiani kwa kutetea pumzi yangu.."
NB: Mahali nilipoweka (........) ina maana sijataka iwe ni sehemu ya mjadala au kuzua taharuki kwa maana hiyo pia ni siri kuu iliyolindwa kwa miaka maelfu kwa maelfu kwa nia nzuri mimi ni nani hata niizungumzie? hivyo naomba nisiulizwe juu ya hilo.