Safari ya kurudi mwezini November 2024

Safari ya kurudi mwezini November 2024

Mzawa_G

JF-Expert Member
Joined
Feb 27, 2014
Posts
669
Reaction score
1,479
Shirika la uchunguzi wa mambo mbalimbali ya anga za mbali duniani ambalo linapatikana nchini Marekani NASA hatimaye siku ya jana wameweza kutangaza majina manne ya wanaanga watakao hudumu kwenye mission ya kurudi mwezini Artemis II

Ilikuwa ni jambo la furaha kwa wanaanga hao maana ilikuwa ni kundi kubwa la wanaanga 30 hivyo ni furaha kwa wanaanga hao wanne kuona majina yao yamechaguliwa kwenye mission hiyo kubwa ya kihistoria

[emoji3581] Gregory Reid Wiseman _ huyu atakuwa ndio mission commander au kiongozi mkubwa wa mission nzima na ndio atakuwa anapokea taarifa zote na commands zote kutoka duniani na ni mwanaanga wa NASA

[emoji3581] Victor J Clover _ huyu atakuwa kama ndio Pilot wa Chombo kizima cha kuelekea huko mwezini mambo ya manuevering yote kuelekea kwenye trajetories zinazohitajika zitafanywa na jamaa ambaye anamuonekano wa rangi nyeusi
Moja ya rekodi iliyombeba ni ameendesha vyombo mbalimbali vya anga kama ndege kwa jumla ya masaa 3,000
Mwanaanga wa Marekani kutoka NASA .

[emoji3581] Christina Koch _ Atakuwa kama Mission specialist wa safari nzima huku akiwa ana rekodi matukio na kufanya chunguzi nyingi za katika safari nzima , kumbuka mwanadada huyu amesomea mambo ya umeme , kiufupi ni electrical engineer , Mwananga wa NASA

[emoji3581]Jeremy Hansen _ Mwanaanga wa shirika la anga la Canada CSA , huyu atakuwa kama Mission specialist ambapo pia atasaidiana na mwanadada Christina Koch kufanya analysis mbalimbali katika safari nzima na kufanya tafiti fupi kuhusu waliyoyaona safarini

Safari itafanyika Mwezi wa 11 Mwakani 2024 kwa sasa mafunzo mazito yataendelea kwa wanaanga hawa katika harakati za kufahamu chombo watakachoenda nacho huko katika moja wapo ya maumbo yanayopatikana angani ambapo sisi tumeipa jina la mwezi

Kumbuka safari za mwezini ni moja ya safari ambazo ni ngumu sana kwa chombo hata kwa wanaanga sababu ni lazima kuwe na chombo imara kitakachowalinda wanaanga dhidi ya extremely radiations mbalimbali kutoka katika Jua letu

Go NASA go Artemis II to the Moon

[emoji419]Moudyswema
[emoji419]Tanzaniascienceyetu
[emoji419]AstronomyKiswahili
FB_IMG_1680812238878.jpg
 
Shirika la uchunguzi wa mambo mbalimbali ya anga za mbali duniani ambalo linapatikana nchini Marekani NASA hatimaye siku ya jana wameweza kutangaza majina manne ya wanaanga watakao hudumu kwenye mission ya kurudi mwezini Artemis II

Ilikuwa ni jambo la furaha kwa wanaanga hao maana ilikuwa ni kundi kubwa la wanaanga 30 hivyo ni furaha kwa wanaanga hao wanne kuona majina yao yamechaguliwa kwenye mission hiyo kubwa ya kihistoria

[emoji3581] Gregory Reid Wiseman _ huyu atakuwa ndio mission commander au kiongozi mkubwa wa mission nzima na ndio atakuwa anapokea taarifa zote na commands zote kutoka duniani na ni mwanaanga wa NASA

[emoji3581] Victor J Clover _ huyu atakuwa kama ndio Pilot wa Chombo kizima cha kuelekea huko mwezini mambo ya manuevering yote kuelekea kwenye trajetories zinazohitajika zitafanywa na jamaa ambaye anamuonekano wa rangi nyeusi
Moja ya rekodi iliyombeba ni ameendesha vyombo mbalimbali vya anga kama ndege kwa jumla ya masaa 3,000
Mwanaanga wa Marekani kutoka NASA .

[emoji3581] Christina Koch _ Atakuwa kama Mission specialist wa safari nzima huku akiwa ana rekodi matukio na kufanya chunguzi nyingi za katika safari nzima , kumbuka mwanadada huyu amesomea mambo ya umeme , kiufupi ni electrical engineer , Mwananga wa NASA

[emoji3581]Jeremy Hansen _ Mwanaanga wa shirika la anga la Canada CSA , huyu atakuwa kama Mission specialist ambapo pia atasaidiana na mwanadada Christina Koch kufanya analysis mbalimbali katika safari nzima na kufanya tafiti fupi kuhusu waliyoyaona safarini

Safari itafanyika Mwezi wa 11 Mwakani 2024 kwa sasa mafunzo mazito yataendelea kwa wanaanga hawa katika harakati za kufahamu chombo watakachoenda nacho huko katika moja wapo ya maumbo yanayopatikana angani ambapo sisi tumeipa jina la mwezi

Kumbuka safari za mwezini ni moja ya safari ambazo ni ngumu sana kwa chombo hata kwa wanaanga sababu ni lazima kuwe na chombo imara kitakachowalinda wanaanga dhidi ya extremely radiations mbalimbali kutoka katika Jua letu

Go NASA go Artemis II to the Moon

[emoji419]Moudyswema
[emoji419]Tanzaniascienceyetu
[emoji419]AstronomyKiswahiliView attachment 2578981
Kwenda anga za mbali hususan kwenye mwezi ni Moja kati ya safari ngumu na hatari kuwahi kufanywa na mwadamu. Hizi picha wanazopiga za dizain hii kabla ya kuondoka duniani Huwa zinahamasisha na pia kuhuzunisha sana .. maana hubaki kama kumbukumbu ya kipekee just In case things goes wrong out there.
 
I can't wait to see this..

At last wengi wetu hatukuwepo kwahiyo ilionekana ni uongo tu, acha tuone hili
 
Tuliokuwepo enzi za Apollo 11 tutafurahi kulishuhudia tena tukio la binadamu kutua mwezini!
 
Sijui iliishaje ishaje hii,maana hawakuleta mrejesho waliyoyaona njiani kuelekea mwezini🤣🤣,wazungu bana wanadhani kwenda Mwezini ni sawa na kuja Afrika😔
 
Sijui iliishaje ishaje hii,maana hawakuleta mrejesho waliyoyaona njiani kuelekea mwezini🤣🤣,wazungu bana wanadhani kwenda Mwezini ni sawa na kuja Afrika😔
ni kwamba huamini kama walienda ?
 
ni kwamba huamini kama walienda ?
Kiukweli mi siamini mkuu,hakuna binadamu aliyewahi kufika kwenye mwezi Wala kwenye jua,huko mars wameishia kupabatiza jina tuu😎!
Vifaa vyao ndiyo wanavituma huko na huwaletea taarifa za huko wao wakiwa duniani.
Huko juu ni tafarani mkuu,ushawahi kuuangalia mwezi Kwa umakini??hakika ni dubwana linalotisha mnooo!
 
Kiukweli mi siamini mkuu,hakuna binadamu aliyewahi kufika kwenye mwezi Wala kwenye jua,huko mars wameishia kupabatiza jina tuu😎!
Vifaa vyao ndiyo wanavituma huko na huwaletea taarifa za huko wao wakiwa duniani.
Huko juu ni tafarani mkuu,ushawahi kuuangalia mwezi Kwa umakini??hakika ni dubwana linalotisha mnooo!
Mzee kwenye mwezi wameenda hao jamaa. Ila huko mars hawajafika zaidi ya kutuma vyombo vya utafiti. Hivi unajua kuna chombo kinaitwa voyager 2, kilichorushwa miaka ya 70 kwenye anga za mbali na bado hakijawahi rudi duniani tena? Huenda mwanadamu akaenda mars lakini huenda tusishuhudie sisi labda kizazi kijacho cha miaka 100 ijayo.
 
Back
Top Bottom