denooJ
JF-Expert Member
- Mar 31, 2020
- 18,511
- 68,141
Ripoti mbalimbali toka viunga vya jiji la Liverpool zinabainisha mshambuliaji wao raia wa Senegal, Sadio Mane, ataondoka dirisha hili la kiangazi.
Habari hizo zinadai kwamba, Bayern Munich wamekuwa na makubaliano ya muda kumtaka Mane, na wakakubaliana wasubiri kwanza mpaka fainali ya UEFA iliyochezwa usiku wa jana ipite, ambapo Liverpool walifungwa 1-0 na Real Madrid ya Hispania.
Inajulikana wazi sababu za,Bayern kumtaka Mane ni kwa ajili ya kuziba pengo la mshambuliaji wao wa Poland, Robert Lewandoski, ambaye anataka kutimkia FC Barcelona ya Hispania majira haya ya kiangazi.
Kinachosubiriwa sasa ni kuona kama Liverpool FC, watakuwa tayari kumpoteza Mane aliyebakiza mwaka mmoja kwenye mkataba wake unaoisha 2023, huku wakiwa bado hawajampata mbadala wake.
Swali la kujiuliza ni je; moto wa Liverpool utaendelea kuwepo bila Sadio Mane pale mbele akishirikiana na Mo Salah?
Habari hizo zinadai kwamba, Bayern Munich wamekuwa na makubaliano ya muda kumtaka Mane, na wakakubaliana wasubiri kwanza mpaka fainali ya UEFA iliyochezwa usiku wa jana ipite, ambapo Liverpool walifungwa 1-0 na Real Madrid ya Hispania.
Inajulikana wazi sababu za,Bayern kumtaka Mane ni kwa ajili ya kuziba pengo la mshambuliaji wao wa Poland, Robert Lewandoski, ambaye anataka kutimkia FC Barcelona ya Hispania majira haya ya kiangazi.
Kinachosubiriwa sasa ni kuona kama Liverpool FC, watakuwa tayari kumpoteza Mane aliyebakiza mwaka mmoja kwenye mkataba wake unaoisha 2023, huku wakiwa bado hawajampata mbadala wake.
Swali la kujiuliza ni je; moto wa Liverpool utaendelea kuwepo bila Sadio Mane pale mbele akishirikiana na Mo Salah?