Habarindiyohiyo
JF-Expert Member
- Aug 11, 2008
- 263
- 13
MFANYABIASHARA maarufu nchini Jaffar Sabodo amehoji matumizi katika taasisi ya Mwalimu Nyerere na kuitaka itoe mchanganuo wa Sh1bilioni alizoichangia taasisi hiyo mwaka jana.
Katika tangazo lake alilotoa jana kupitia vyombo vya habari, Sabodo alitaka kueleza namna ilivyotumia Sh 1bilioni aliyotoa wakati wa mchezo wa bahati nasibu ulioendeshwa na taasisi hiyo.
Pia ameitaka ieleze mafanikio yake tangu ilipoanzishwa.
Katika tangazo hilo alilotoa kuulezea utawala wa rais Jakaya Kikwete miaka minne tangu aingie madarakani, Sabodo ameitaka taasisi hiyo kueleza matumizi ya taasisi hiyo kwanza kabla ya kumshutumu rais Kikwete.
âKupitia mchezo wa bahati nasibu ulionzishwa na taasisi ya Mwalimu Nyerere nilichangia Sh1 bilioni lakini kutokana na mapungufu makubwa ya mfuko huo imeshindwa hata kufikisha Sh200 milioni kwa kuuza bidhaa mbalimbali katika bahati nasibu hiyo," alisema Sabodo katika taarifa hiyo na kuongeza:
"Mbali na mimi, watu wengi pia wamechangia katika mfuko huo. Fedha zote walizochangiwa zipo wapi?, waseme walichofanya, waseme walichopoteza?".
Maelezo ya Sabado yanafuatia kuwepo na ongezeko kubwa la watu kutoka ndani ya CCM ambao wamejitokeza hadharani na kumkosoa Rais Kikwete kuwa anashindwa kufanya maamuzi magumu, hasa dhidi ya mafisadi huku wengine wakikiona chama hicho kikipoteza mwelekeo na kuachana na wakulima na wafanyakazi.
Miongoni mwa watu hao ni mawaziri wa zamani, Mussa Nkangaa na Matheo Qares ambaye alidiriki kusema kuwa iwapo Kikwete atashindwa kufanya maamuzi magumu ifikapo 2010, basi CCM isimteue kugombea urais. Kikwete alijibu kuwa hashangazwi na maneno ya watu hao, lakini akasema kuwa atakaa na wenzake, ambao hakuwataja, kuandaa majibu.
Katika tangazo hilo Sabodo anaona kuwa sasa ni wakati wa taasisi hiyo kueleza imetoa mchango gani kwa watanzania.
âAidha, wao waeleze walichofanya wakati walipokuwa katika nafasi nyeti za utawala, na si kuulaumu utawala wa sasaâ. Imesema taarifa hiyo
Sabodo, mmoja wa watu muhimu katika historia ya nchin hii, anaona kwamba Rais Kikwete atakubukwa na taifa la Tanzania kama atafanya mapinduzi ya kweli katika kilimo. âHivyo ninamshauri rais kuunda Shirikisho la Umoja kama walivyofanya nchini Sweden. Namuomba muheshimiwa Kikwete ainge mfano kama wa aliyekuwa rais wa Marekani Goerge Washington na Nehru wa India ambao walifanya mapinduzi ya kweli ya kilimo katika nchi zao.â
Akizungumza na Mwananchi jana kwa njia ya simu, mkurungezi wa taasisi ya Mwalimu Nyerere, Joseph Butiku alisema; â Nenda kwa huyo huyo Sabodo akupe Clarification (maelezo) zaidi ya hayo aliyosema. Mimi siwezi kujibu kitu ambacho sikijui, sina la zaidi akakata simu.â
Pia kupitia tangazo hilo Sabodo anadai
Edwin Mtei ambaye alikuwa ni gavana na pia Waziri wa Fedha ndiye aliyemshauri hayati Mwalimu Julius Nyerere kupunguza thamani ya fedha kwa asilimia 20 lakini Mwalimu alipingana na ushauri huo. Wakati huo thamani ya fedha ya Tanzania ilikuwa kati ya Sh 14 na 15 kwa dola moja ya kimarekani.
âNa kuanzia hapo ndio thamani ya fedha ya Tanzania ilianza kushuka,âilisema taarifa hiyo.
âNi bora nimpende mtu ambaye si mwaminifu lakini anatimiza wajibu wake kwa kufanya mambo mazuri na yenye manufaa kuliko kumpenda mwaminifu ambaye hawezi kutimiza wajibu,â
Sabodo alisema mwalimu alikuwa ni mtu muelewa, mwenye kujali na aliyetumia maisha yake kwa ajili ya kuwatumikia watu na wala hakuwa mchumi.
Kama rais Kikwete ataweka mpango madhubuti wa kuhakikisha thamani ya fedha ya Tanzania inakuwa, uchumi utakuwa kwa kasi. Mfano ni nchi za Mauritius, Singapore na Thailand. Kulinda na kukutza thamani ya fedha ndio inayohitajika sasa na si vinginevyo.
Katika tangazo lake alilotoa jana kupitia vyombo vya habari, Sabodo alitaka kueleza namna ilivyotumia Sh 1bilioni aliyotoa wakati wa mchezo wa bahati nasibu ulioendeshwa na taasisi hiyo.
Pia ameitaka ieleze mafanikio yake tangu ilipoanzishwa.
Katika tangazo hilo alilotoa kuulezea utawala wa rais Jakaya Kikwete miaka minne tangu aingie madarakani, Sabodo ameitaka taasisi hiyo kueleza matumizi ya taasisi hiyo kwanza kabla ya kumshutumu rais Kikwete.
âKupitia mchezo wa bahati nasibu ulionzishwa na taasisi ya Mwalimu Nyerere nilichangia Sh1 bilioni lakini kutokana na mapungufu makubwa ya mfuko huo imeshindwa hata kufikisha Sh200 milioni kwa kuuza bidhaa mbalimbali katika bahati nasibu hiyo," alisema Sabodo katika taarifa hiyo na kuongeza:
"Mbali na mimi, watu wengi pia wamechangia katika mfuko huo. Fedha zote walizochangiwa zipo wapi?, waseme walichofanya, waseme walichopoteza?".
Maelezo ya Sabado yanafuatia kuwepo na ongezeko kubwa la watu kutoka ndani ya CCM ambao wamejitokeza hadharani na kumkosoa Rais Kikwete kuwa anashindwa kufanya maamuzi magumu, hasa dhidi ya mafisadi huku wengine wakikiona chama hicho kikipoteza mwelekeo na kuachana na wakulima na wafanyakazi.
Miongoni mwa watu hao ni mawaziri wa zamani, Mussa Nkangaa na Matheo Qares ambaye alidiriki kusema kuwa iwapo Kikwete atashindwa kufanya maamuzi magumu ifikapo 2010, basi CCM isimteue kugombea urais. Kikwete alijibu kuwa hashangazwi na maneno ya watu hao, lakini akasema kuwa atakaa na wenzake, ambao hakuwataja, kuandaa majibu.
Katika tangazo hilo Sabodo anaona kuwa sasa ni wakati wa taasisi hiyo kueleza imetoa mchango gani kwa watanzania.
âAidha, wao waeleze walichofanya wakati walipokuwa katika nafasi nyeti za utawala, na si kuulaumu utawala wa sasaâ. Imesema taarifa hiyo
Sabodo, mmoja wa watu muhimu katika historia ya nchin hii, anaona kwamba Rais Kikwete atakubukwa na taifa la Tanzania kama atafanya mapinduzi ya kweli katika kilimo. âHivyo ninamshauri rais kuunda Shirikisho la Umoja kama walivyofanya nchini Sweden. Namuomba muheshimiwa Kikwete ainge mfano kama wa aliyekuwa rais wa Marekani Goerge Washington na Nehru wa India ambao walifanya mapinduzi ya kweli ya kilimo katika nchi zao.â
Akizungumza na Mwananchi jana kwa njia ya simu, mkurungezi wa taasisi ya Mwalimu Nyerere, Joseph Butiku alisema; â Nenda kwa huyo huyo Sabodo akupe Clarification (maelezo) zaidi ya hayo aliyosema. Mimi siwezi kujibu kitu ambacho sikijui, sina la zaidi akakata simu.â
Pia kupitia tangazo hilo Sabodo anadai
Edwin Mtei ambaye alikuwa ni gavana na pia Waziri wa Fedha ndiye aliyemshauri hayati Mwalimu Julius Nyerere kupunguza thamani ya fedha kwa asilimia 20 lakini Mwalimu alipingana na ushauri huo. Wakati huo thamani ya fedha ya Tanzania ilikuwa kati ya Sh 14 na 15 kwa dola moja ya kimarekani.
âNa kuanzia hapo ndio thamani ya fedha ya Tanzania ilianza kushuka,âilisema taarifa hiyo.
âNi bora nimpende mtu ambaye si mwaminifu lakini anatimiza wajibu wake kwa kufanya mambo mazuri na yenye manufaa kuliko kumpenda mwaminifu ambaye hawezi kutimiza wajibu,â
Sabodo alisema mwalimu alikuwa ni mtu muelewa, mwenye kujali na aliyetumia maisha yake kwa ajili ya kuwatumikia watu na wala hakuwa mchumi.
Kama rais Kikwete ataweka mpango madhubuti wa kuhakikisha thamani ya fedha ya Tanzania inakuwa, uchumi utakuwa kwa kasi. Mfano ni nchi za Mauritius, Singapore na Thailand. Kulinda na kukutza thamani ya fedha ndio inayohitajika sasa na si vinginevyo.