Sababu za Tanzania kushindwa mjadala wa Makinikia

.

Wacha niseme kwanza mimi sina chama na wala sina mrengo wowote kisiasa. Ila, nachukia ufisadi!

Hili suala la CCM walifanya hivi au vile nafikiri tunaliongelea kijumla jumla sana.

CCM ni moja lakini ndani yake kuna makundi. Kuna CCM ya Azimio la Arusha na kuna CCM ya Azimio la Zanzibar.

Hapa naongelea wanachama, siyo chama!

Wale wanaoamini Azimio la Zanzibar, walisaini hiyo mikataba lakini kuna wengi wanaoamini katika utu na miiko ya uongozi ambao walipinga jitihada zile za kusaini mikataba ya kitapeli. Kwa hiyo ni vizuri tuwe waangalifu tunapo zungumzia hili suala bila kusahau kiini cha tatizo.

Nitaishia hapa.
Hata kama CCM hao hao walikosea wanapojirekebisha kuna ubaya gani? Yaani tuwachukie kwa kuwa wameamua kujirekebisha? Ni jambo zuri kukubali makosa na kurekebisha, haiondoi nafasi ya wapinzani wapiga kelele.
 
Duu!! kuna watu wanaomba kwenye hii issue tusifanikiwe kabisa aisee Magu una kazi sana kuijenga nchi yako uipendayo..
 
Unajua 'tax evasion' ni kitu gani? Na madhara yake?
Chini ya serikali ya CCM, tax evasion siyo ishu! Tax evaders uwa wanaombwa walipe kodi walizokwepa, kisha wanasemehewa. Kama vile wezi wanavyoombwa warudishe fedha za wizi kama condition ya msamaha. Haya yote yanafanyika nje ya Mahakama!!!
[HASHTAG]#magufuliisaphony[/HASHTAG]
 
Hata kama CCM hao hao walikosea wanapojirekebisha kuna ubaya gani? Yaani tuwachukie kwa kuwa wameamua kujirekebisha? Ni jambo zuri kukubali makosa na kurekebisha, haiondoi nafasi ya wapinzani wapiga kelele.
.
Mtu mzima akikosea siyo lazima aseme 'samahani', unaweza tuu ukaona mambo yamebadilika basi, we juwa ndo kujirekebisha huko.

Binafsi sikatai upinzani kupiga kelele, lakini kelele ziwe za msingi, sio kelele tuu ilimradi usikike.

Kipindi Slaa katibu mkuu, nilikuwa nafurahia makelele yake kwa CCM, kwasababu walikuwa wanafanya mambo ya hovyo. Nilikuwa nasikitika mno kuona Mnyika akipelekwa pelekwa central bila sababu ya msingi. Lakini sasa kuna sababu gani ya msingi kupiga makelele?
 
Ulitakiwa kuwauliza uliowaazimisha ubongo wakupatie facts wakati walipokua wanazunguka nchi nzima kusema ccm ya kikwete ni mafisadi pamoja na Lowasa na leo wanasema kikwete ni rais bora. Na hii ndiyo sababu yangu ya kuandika kama nilivyoandika na kweli ninyi watu wa ukawa na rafiki zenu ccm mna matatizo ya akili. Mnatakiwa kusaidiwa na dawa yenu imepatikana inaitwa Dr Pombe John joseph Makomea ya kufuri. Mtamchukia ninyi na wenzenu wezi 2a ccm lakini Pombe ipo hapa mpaka 2025. Na jinsi nionavyo itakua kata mti panda mti maana kutakuja pombe mwingine nawashauri mhame nchi kama Mange Kimambi maana hakuna kupumua.
Ukiwachukua Sizonje na JK, wote wabovu ila afadhali JK

Sent using Jamii Forums mobile app
 
WAZUNGU mliwaleta nyie mnaojipaka rangi ya "uzalendo", kwa mikataba yenu feki. Mkawaundia (kwa dharura) sheria za kuwalinda. Ili kuwaondoa nako itatumika mikataba hiyohiyo mlioweka kwa 10% mlizokula. Hapo ndipo "UZALENDO" wenu ulipotufikisha.

Sent using Jamii Forums mobile app
Not under this administration... Kama wanaamini wanaweza kuyachimba kwa mikataba hiyo hiyo feki wajaribu sasa....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Chini ya serikali ya CCM, tax evasion siyo ishu! Tax evaders uwa wanaombwa walipe kodi walizokwepa, kisha wanasemehewa. Kama vile wezi wanavyoombwa warudishe fedha za wizi kama condition ya msamaha. Haya yote yanafanyika nje ya Mahakama!!!
[HASHTAG]#magufuliisaphony[/HASHTAG]

Hiyo ilikuwa kipindi kile, wewe ulitegemea hata siku moja kuona Manji akioteshwa ndevu kiasi ile?
 
Wakati tunaingia mkataba na Barrick/Acacia
1. CHADEMA ndio waliopiga makofi na kuoitisha sheria ya madini
2. CHAdEMA ndio waliotoa wanasheria kuandaa na kuridhia mikataba hiyo.
3. CHADEMA ndio waliotoa Mwanansheria mkuu wa serikali ili kuridhia na kumshauri rais kuhusiana na mikataba hiyo
4. CHADEMA ndio waliochagua Wakala wa Madini ambaye aliidhinisha kontena zilizo na makinikia bila kujua thamani halisi ya kilichomo humo ndani
5.CHADEMA ndio walitoa Waziri wa Nishati na Madini ambaye aliendelea kuona uozo ukifanyika
6.CHADEMA ndio walikuwa wanaongoza TRA ambayo ilishindwa kukusanya kodi stahiki kwa miaka zaidi ya 19.
7. CHADEMA ndio walikuwa wanaongoza Kitengo cha usajili wa makampuni na kuacha Barrick/ Acacia kufanya biashara bila kusajiliwa.

CHADEMA mmetufikisha hapa, tuache chama kitakatifu CCM kisafishe nchi yetu.

ON A SERIOUS NOTE : CCM MNAPASWA KUWAOMBA RADHI WATANZANIA
 
Hiyo ilikuwa kipindi kile, wewe ulitegemea hata siku moja kuona Manji akioteshwa ndevu kiasi ile?

Kipindi hiki nazungumzia. Wakwepaji kodi Bandarini walisamehewa kinyume na sheria. Leo ndiyo wachangiaji na washirika wakubwa wa Daud Bashite, mhaini aliye mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam.

Kosa la Manji ni lipi kwani? Sijasikia kama amefikishwa Mahakamani kwa tax evasion ama wizi!! Ebu nielezee. Ninachokiona ni matumizi mabaya ya madaraka. Kichaa kapewa rungu, basi anakomoa kila mtu asiyempenda. Ana tofauti gani na Bwana Dhaifu aliyefunga watu jela maisha kisa ugomvi wao binafsi juu ya wanawake?

Kwa kelele zake juu ya wakwepa kodi, nilitaraji mahakama ya ufisadi ingekuwa imeelemewa na kesi. Ila ajabu, ati mahakama inakosa wateja.

[HASHTAG]#magufuliisaphony[/HASHTAG]
 
Tumuunge mkono Rais wetu, akifanikiwa tutafaidika wote, hivi hatutaki Tanzania iwe kama Oman Qater au Sauth Africa? Nasie tunahitaji siku moja twende morroco tukatoe ahadi ya kuwajengea uwanja wa mpira.

Leo hii kwa mara ya kwanza uongozi wa mgodi kaachiwa mzawa tangu waanze kuchimba, wametamka bayana baadaya mazungumzo wataendesha kwa faida na hapo bado mazungumzo hayajakamilisha.

Hebu tuacheni ramli chonganishi.
 
Umenisoma vizuri ama na wewe una utindia ubongo. Nimeweka list ya wezi ambao unawaita makamanda. Wezi wa ccm wakiletewa figisu wanakwenda ccm B Chadema maana huko ndiko kimbilio lao. Kwasasa hata wezi waliobaki ccm wana kazi ya ziada. Mimi ni timu Magu2015/25 ukitaka kuwa na akili nzuri achana na vyama jiunge na timu ya ushindi na uzalendo Timu Magu2015/25
Ndio mkuu nina utindio.
Ila sijawazidi nyie wadumavu wa akili wa Lumumba

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tumeshafika nusu ya safari, bado nusu yake kufikia 2020. Kwa hali inavyokwenda inaanza kuwa rahisi kutabiri kitakachotokea wakati huo ujao. Watu tumechoka mno, hali haileti matumaini hata kidg. nyumbo za labda kesho zimechosha sana. Ninaamini penye giza nuru itaanza kung'aa
 
Wakwepaji kodi Bandarini walisamehewa kinyume na sheria..

.
Serikali inaweza kuwa ilipima mzani nakuona makosa yao yanasameheka.ii


Kosa la Manji ni lipi kwani? Sijasikia kama amefikishwa Mahakamani kwa tax evasion ama wizi!! Ebu nielezee.

.
Ni kweli kisheria Manji hana makosa na huwezi kumpata kwa njia hiyo lakini sheria na haki ni vitu viwili tofauti. Unaweza ukamtetea mwizi kisheria na akashinda, lakini vile vile ukawa hujatenda haki kwa yule aliyeibiwa.

Sheria si uhalisia wa jambo bali tafsiri.

Ndiyo hapo madaraka ya Rais yanapokuja ili aweze kunyoosha pale sheria inapokoma. Sasa unamwachiaje mtu anaehonga mpaka majaji? Sikatai kunaweza kuwa na matumizi mabaya ya madaraka lakini kwa Manji ni sawa kabisa.

Ana tofauti gani na Bwana Dhaifu aliyefunga watu jela maisha kisa ugomvi wao binafsi juu ya wanawake?
.
Kusema utawala huu na ule unafanana katika visasi si kweli na hasa linapokuja suala la ufisadi. Awamu hii ina matatizo yake lakini kwenye kuminya mirija ya wezi wanajitahidi sana.

Kwa kelele zake juu ya wakwepa kodi, nilitaraji mahakama ya ufisadi ingekuwa imeelemewa na kesi. Ila ajabu, ati mahakama inakosa wateja.
.
Hapa nakubaliana na wewe tuendelee kulipigia kelele, lakini pia tukumbuke serikali ina mkono mrefu. kupelekwa mahakamani siyo njia pekee ya kuhukumiwa. Mtu akinyang'anywa mashamba yake kwa kushindwa kuyaendeleza, si ndiyo kuhukumiwa huko?
 
1. Kwenye Sheria ya Madini hakuna kifungu kinachoipa Mamlaka Kamati ya Rais

2. Kwenye mkataba hakuna kipengele kinachoipa mamlaka Kamati ya Rais

3. Sheria inamtambua Kamishna wa Madini na sio Rais, hivyo mwenye Mamlaka ya kutengua kibali ni Kamishna wa madini na sio Rais.
Na kwamba kama kuna udanganyifu mwenye Mamlaka ya kutengua ni Kamishna wa madini na sio Rais na Kamati yake. Kwa hiyo Rais angemuita Kamishna akamulekeza atengue maamuzi kwa maandishi

The Whole Issue is null and void

Sent using Jamii Forums mobile app

Ila kuna vipengele vinavyoruhusu upande ule mwingine kutuibia au kuidanganya serikali kuhusu mapato si ndiyo?
 
Back
Top Bottom