Grader
JF-Expert Member
- Feb 23, 2009
- 445
- 65
WanaJF tujadiliane sababu za msingi za kuongezeka kwa migomo hapa Tanzania na suluhisho zake mana kila kukicha hapiti bila kusikia neno mgomo. Najua humu kuna watumishi wataguswa na hizo sababu na masuluhisho yake wayachukue na kuyafanyia kazi. Baadhi ya migomo tulishawahi kusikia, migomo ya walimu kudai haki zao, madereva, wafanyabiashara, wanafunzi shuleni na vyuoni, wabunge, madiwani, watumishi wa kada mbalimbali n.k.
Nawasilisha
Nawasilisha