Sababu ya mambo kubaki 'Kama kawaida' pamoja na teua/tengua, maelekezo, maelezo na 'mikwara' ya Rais Magufuli

K.umamake wabongo hamna jema,maanina,..ndomana skuhiz nmeamua kuwapuuza watu kama mtoa mada..

Tho leo nmeshindwa
 
Juz badala Ampongeze Msaidiz wake kwa kufanikisha Marufuku ya mifuko ya plastiki kwa ustadi mkubwa.....
Akaanza kujisifia kua alitoa maelekezo tangu mwaka jana tena akalaumu na kukosoa kua wizara wamechelewa sana....!
Atakuwa na gubu huyu mtu sio bure
 
Ni kweli... LEO UKIMTENGUA ULIYEMTEUA JANA, unachofanya ni kutuonyesha HOW MUCH jana ulikosea.... na watenguliwaji wanapozidi kuwa wengi, unatuonyesha umekosea mara ngapi na ukubwa makosa upoje....

SI kila aliyetenguliwa alikosea, wengine walikuwa wanatekereza maagizo yake, lakini alipoona yanaleta NEGATIVE IMPACT akaamua kuwatoa SADAKA YA KUTENGULIWA
NI KWELI ALISHAWAHI kumtengua athuman diwani then akamteua tena cheo kingine
 
Ni kweli... LEO UKIMTENGUA ULIYEMTEUA JANA, unachofanya ni kutuonyesha HOW MUCH jana ulikosea.... na watenguliwaji wanapozidi kuwa wengi, unatuonyesha umekosea mara ngapi na ukubwa makosa upoje....

SI kila aliyetenguliwa alikosea, wengine walikuwa wanatekereza maagizo yake, lakini alipoona yanaleta NEGATIVE IMPACT akaamua kuwatoa SADAKA YA KUTENGULIWA
Ingekuwa Marekani tayari walishamtaka apimwe akili(sanity) kama Trump
 
Naweza kusema kuwa bado tu hawajamjua anataka nini, Rais anataka kiongozi mzarendo na aliyejikana kwa masrahi mapana ya taifa na si mtu anayewaza masrahi yake huku akijua yeye ni kiongozi wa umma

Kuwa kiongozi wa umma ni kujitoa kwa ajili ya wananchi na si kuwaza utakuwa umemiliki nini baada ya kustaafu au kumaliza muda wako wa uongozi.

Kuwa kiongozi si kupata fursa ya kukufanya uwe tajili baali uwe daraja la kuwavusha wananchi na taifa kwa ujumla kufikia malengo
ACHA UPUUZI WEWE NANI MALENDO KTK UTAWAL HUU?
 
Ni kweli... LEO UKIMTENGUA ULIYEMTEUA JANA, unachofanya ni kutuonyesha HOW MUCH jana ulikosea.... na watenguliwaji wanapozidi kuwa wengi, unatuonyesha umekosea mara ngapi na ukubwa makosa upoje....

SI kila aliyetenguliwa alikosea, wengine walikuwa wanatekereza maagizo yake, lakini alipoona yanaleta NEGATIVE IMPACT akaamua kuwatoa SADAKA YA KUTENGULIWA
Brother, hizi ndo akili ambazo zinahitajika humu jamii forum. Simply "THE GREAT THINKERS"
 
Unapojenga jengo kubwa la TRA kwenye makusanyo madogo ya kodi si maslahi ya eneo lako?

Unapojenga uwanja wa ndege ambao hakutatua ndege "YA MAANA" si maslahi ya eneo utokalo?

By the way, HATA TAA ZA BARABARANI zilizojengwa enzi za uwazili, haina tofauti na hayo hapo juu
Jengo ni la umma na lipo kwa maslahi ya umma na taifa kwa ujumla.

Uwanja ni wa umma na upo kwa maslahi ya umma na taifa kwa ujumla

Kutua ndege za maana siyo hoja ya msingi, hata Musoma uwanja upo lakin hakuna ndege za maana zinazotua pale.

Vivyo hivyo taa si za mtu binafsi.
 
Kila kiumbe hujitofautisha kwa sifa zake. Vipo vunavyofahamika na kujitanabaisha kwa kutaga mayai, kuzaa, kuruka, kutambaa, kutembea na kadhalika. Sifa hutofautisha.

Alipoingia madarakani Rais Magufuli, wananchi na wasaidizi/wateule wake walikuwa wakisubiri Rais ajitanabaishe. Sasa wameshamjua. Wanafuata kadiri atakavyo.

Wanamjua kuwa anapenda YEYE NA NI YEYE TU ABUNI JAMBO. Wao wanasubiri ubunifu wake. Wanamjua kuwa HACHELEWI KUKUGEUKA UKITHUBUTU KUBUNI AU KUAMUA. wasaidizi wanamngoja aseme wafanye nini.

Wasaidizi HAWAJUI KINACHOMFURAHISHA WALA KINACHOMKWAZA KATIKA UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU YAO. Wanamsubiri atoe maelekezo. Wanamsubiri kila wakati aseme. Ndiyo maana makongamano hayaishi.

Wasaidizi wanamjua KUWA HASHINDWI GHAFLA NA TENA HADHARANI KUKUPANDISHA CHEO, KUKUTUMBUA/KUKUTEUA,KUKUSHUSHA AU HATA KUSEMA KWANINI AMEFANYA HIVYO. Daima wanasubiri muongozo.

Kutokana na hayo, wakubadilisha Ni YEYE. Aruhusu wasaidizi wake wabuni, waamue, waseme na watende bila kusubiri maelekezo. Wasaidizi wataenendelea kumsikiliza, kuandika maagizo na kuendelea na 'kawaida' iliyopo.

Dawa Ni kutoka kwa muundaji mwenyewe!

Mzee Tupatupa wa Lumumba(kwasasa Kilosa, Morogoro)
Mbona husemi kitu kuhusu baadhi watendaji wa TRA wenye tabia za kijinga kubambikizia watu mizigo isiyobebeka?

Sema neno kuhusu waomba rushwa wanaotusumbua ili kutupatia huduma ambazo ni haki yetu kisheria.

Wakati mwingine hua nasimama na Magufuli na akinikera hua sifichi hua nasema na kumuombea asiteleze tena. Kwa hili la TRA namuunga mkono Magufuli
 
Kila kiumbe hujitofautisha kwa sifa zake. Vipo vunavyofahamika na kujitanabaisha kwa kutaga mayai, kuzaa, kuruka, kutambaa, kutembea na kadhalika. Sifa hutofautisha.

Alipoingia madarakani Rais Magufuli, wananchi na wasaidizi/wateule wake walikuwa wakisubiri Rais ajitanabaishe. Sasa wameshamjua. Wanafuata kadiri atakavyo.

Wanamjua kuwa anapenda YEYE NA NI YEYE TU ABUNI JAMBO. Wao wanasubiri ubunifu wake. Wanamjua kuwa HACHELEWI KUKUGEUKA UKITHUBUTU KUBUNI AU KUAMUA. wasaidizi wanamngoja aseme wafanye nini.

Wasaidizi HAWAJUI KINACHOMFURAHISHA WALA KINACHOMKWAZA KATIKA UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU YAO. Wanamsubiri atoe maelekezo. Wanamsubiri kila wakati aseme. Ndiyo maana makongamano hayaishi.

Wasaidizi wanamjua KUWA HASHINDWI GHAFLA NA TENA HADHARANI KUKUPANDISHA CHEO, KUKUTUMBUA/KUKUTEUA,KUKUSHUSHA AU HATA KUSEMA KWANINI AMEFANYA HIVYO. Daima wanasubiri muongozo.

Kutokana na hayo, wakubadilisha Ni YEYE. Aruhusu wasaidizi wake wabuni, waamue, waseme na watende bila kusubiri maelekezo. Wasaidizi wataenendelea kumsikiliza, kuandika maagizo na kuendelea na 'kawaida' iliyopo.

Dawa Ni kutoka kwa muundaji mwenyewe!

Mzee Tupatupa wa Lumumba(kwasasa Kilosa, Morogoro)
Upo sawa mkuu umenena
 
Naweza kusema kuwa bado tu hawajamjua anataka nini, Rais anataka kiongozi mzarendo na aliyejikana kwa masrahi mapana ya taifa na si mtu anayewaza masrahi yake huku akijua yeye ni kiongozi wa umma

Kuwa kiongozi wa umma ni kujitoa kwa ajili ya wananchi na si kuwaza utakuwa umemiliki nini baada ya kustaafu au kumaliza muda wako wa uongozi.

Kuwa kiongozi si kupata fursa ya kukufanya uwe tajili baali uwe daraja la kuwavusha wananchi na taifa kwa ujumla kufikia malengo.
Yeye ana sifa hizo? Mbona ushahidi wa yeye kulitia hasara taiifa upo kila mahali?
 
Mnamlaumu Magufuli bure tu. Tanzania hii hata atawale malaika bado watu watalalamika tu.
Sisi Watanzania/waafrika wengi wao ni wabinafsi na wazembe sana. Hatujali kazi, Hatufanyi kazi kwa weledi. Mtu akipata nafasi flani anaitumia kuiba ama kunyanyasa wengine. Tunapenda sana kulalamika sometimes with no reasons. Pia ni wanafiki sana. Mtu anaweza kufanya kosa ila akiazibiwa kelele zinapigwa kila kona. Tuna wivu Uliopitiliza. Viongozi wakipewa nafasi hawawi wabunifu katika kuboresha kazi zaidi ya kusubiri mshahara mwisho wa mwezi na Kuplani jinsi ya kupiga allowance.
Kwa kifupi hii nchi hata apewe Mbowe, Zito, Maalimu ama Lipumba bado watu watalalamika tu.
Japo Magu ana mapungufu kidogo ila kwa upande wangu namkubali sana. Maana nlishabahatika kuwa kiongozi kwenye taasisi ya Serikali so Watanzania nawajua. Magu anajitahidi kuwapatia. Maana nlishangaa hata PM alivyowaacha wale jamaa wa TRA waliozuia mzigo wa mfanyabiashara wa Kariakoo unreasonably.
“In Magufuli I Trust”.
“Magufuli again 2020”.
 
Back
Top Bottom