Sababu ya Gazeti la Jambo leo kuingia vitani na RC Makonda ni Manji kutajwa kwenye dawa za kulevya

Biyani

Member
Aug 7, 2016
76
144
Sababu ya Jambo Leo kuingia vitani na RC Makonda ni Manji kutajwa kwenye biashara ya Dawa za kulevya.

Toka RC wa jiji la Dsm amtaje Mfanya biashara Manji kuwa anahusika na Dawa za kulevya gazeti la Jambo Leo toka siku hiyo limeingia kwenye vita kali na RC Makonda.

Kutokana na uandishi wa gazeti hili, kila siku kuandika habari za mtu mmoja tu, ni dhahiri sasa gazeti hilo limepoteza maadili ya uandishi wa habari na sasa kujikita kumtetea bosi wao Manji.

Ni muda muafaka kwa Waziri wa Habari kuwa makini na uanzishwaji wa haya magazeti kwani mengi yanaanzishwa ili kutetea maslahi ya watu wachache.

Ushauri: Watanzania wa mitandaoni tusitumie nguvu kubwa kupotosha ukweli kuwa wengi wa wafanyabiashara kubwa wanatumia na kuuza dawa za kulevya, na kuanza kupotosha ukweli kwa kuleta habari za uongo kuhusu Makonda.

Kama tungekuwa great thinkers kweli tungekuwa tunaongelea suala la Manji kuhusika na dawa za kulevya lakini tunaongelea suala la uzushi kwa RC Makonda.

Hii maana yake ni kuwa suala la dawa za kulevya linagusa maisha ya wengi humu JF na wengi wanafaidika nazo kwa njia moja au nyingine.

Pia ningependa kumshauri mhariri wa gazeti la Jambo Leo kuwa kumshambulia RC Makonda ni sawa na kuipinga serikali kwenye suala la dawa za kulevya. Hii ni kwa sababu RC Makonda anaiwakilisha serikali kutimiza wajibu wake.

Unapomzushia habari nyingi za uongo ni eti kwa sababu amemtaja Manji kwenye dawa ni sawa na kutetea wauza unga.

Naona future yako katika hiyo kazi huko mbeleni inapotea kabisa.
 
Hayo ya Jambo Leo yatakuwia magumu kuelezea kwani utakuwa na dhana tu.
Lakini kwa kuwa inaelekea upo karibu sana na RC Makonda, tuelezee uhusiano wake na CLOUDS FM kwani utakuwa na habari kutoka kwenye chanzo.

RC ameitwa na Bunge (lenye jukumu la kuisimamia serikali) amekaidi
RC ameitwa mahakamani, sijui kama aliitikia wito, sasa tunasikia RC anakwenda CLOUDS FM alikoitwa.
 
10 Reactions
Reply
Back
Top Bottom