SABABU: Ujio wa Obama na timu ya watu 700

Hizi ziara ni nzuri kwa tz kama tuko makini lakini na wasiwasi na aina ya viongozi tulionao kama watakuwa makini ni zoezi tosha kucheza na barca na real kwani tukija kucheza na vibonde tayari sisi tuna muelekeo
 
Sioni tofauti kati ya kipindi Living stone via Carls peter vs Mangungo na wakati uliopo,ubinafs umeanza mda mrefu
 
Liganga Nimefurahishwa na uchambuzi wako.Isipokuwa nataka nikuulize kuwa mbona sasa ni zaidi ya miaka 55 miongo mingi sana , Tangu wakoloni waanze kuondoka kwenye hili bara la africa na kuwaacha waafrica wajitawale na kujiendeshea mambo yao wenyewe, kwa masikitiko makubwa hakuna walichokibadilisha, hata ile miondo mbinu kidogo waliyotuachia, na baadhi ya viwanda na pamoja na rasilimali nyingi walizotubakishia havijatuongezea kasi yeyote ya maendeleo kwa kasi ukilinganisha na walivyokuwepo wakoloni.(sio kwamba naunga mkono ukoloni).

Kama Tanzania walishindwa kujiendeleza wenyewe takriban miaka zaidi ya 50 tangu uhuru 1961, itawezekana lini kujitambua na kujiendeleza yenyewe bila kutumia haya mataifa makubwa ya nje? Tanzania ya leo yenye watu milioni 46 wanashindwa kujitosheleza chakula kwa mwaka mmoja, achilia mbali kuwa na uwezo wa technolojia kubwa ya kuchimba mafuta, madini na gesi..?
 
Last edited by a moderator:
Raslimali bora na yenye thamani kuu ni WATU. Tuanze kwa kuwajenga watu wetu kuwa
-wazalendo,
-wenye mtazamo wa mbali (Vision),
-wanaojitegemea na si wale wanaosubiri serikali iwafanyie vitu
-wenye mipango ya mda mrefu inayooana na mahitaji ya nchi
-wenye elimu bora na ya kisasa inayoendana na mahitaji ya mazingira yaliyowazunguka na si KKK tu.
-watafiti na wagunduzi
-wenyekuthubutu na kupenda kuona matokeo na si kuridhika na maneno matupu

Tukimudu apo basi mengine yanayohusu raslimali kama miundombinuni, usimamizi, uongozi na uwekezaji yatafuata.

Unazunguka sana, In Short ni ELIMU BORA na AFYA vinatosha Vingine vitakuja vyenyewe, sijuhi kilimo kwanza, Utawala bora, uwekezaji, Mitaji vyote vitapatikana tu, Endapo tutasomesha watu wetu vizuri.
 
Kwani Tz kuna nini cha ajabu mpaka uhisi unaibiwa? watanzania tuna roho nyembamba sana inayofanana kabisa na hali yetu ya umaskini kiasi cha kuhisi umaskini wetu ni kwa sababu ya watu fulani wanatuibia, jambo ambalo ni ushezi na ni kutokana na uwezo mdogo tulionao wa kufikiria.
 
Liganga, nakubaliana na wewe mkuu. Pia tunatakiwa kuondoa mawazo mgando ya baadhi ya watu kuamini kila jambo ni lazima lifanywe na serikali, wakisahau kua mimi na wewe ndio serikali na tunaweza kuleta maendeleo tukiwa na UZALENDO

Ukibahatika kufika nchi kama Japan na German, utaelewa uzalendo ni nini na jinsi watu wanavyojiskia kwa kutumia vitu vya nyumbani na kulinda vitu vyote ambavyo ni kwa ajili ya maendeleo yao.

Mfano pale Yokohama, karibu kila mtu anaiona ile bandari kama mboni ya jicho lake, na kila siku wanapambana kuhakikisha inaweka rekodi ya ufanisi. Hii pia niliona kwenye TV kuhusu ile bandari kubwa kule china, inafahamika kama Yangshan.

Ujerumani ndio usiseme, mwaka 2000 walitoa Greencard kwa ajili ya wataalam wa IT toka nje lakini bunge lilipitisha kwa mbinde na likataka atua kali zichukuliwe kufidia nakisi ya nguvu kazi iliyojitokeza. Wahindi wengi walichukua zile kazi kwa muda huo wa miaka mitano baada ya apo walirejea nyumbani maana vyuo vya kijerumani viliishazalisha wahitim wakutosha kuziba pengo.
 
Last edited by a moderator:
You need to look at their approaches to realize who is on top of their game now,EUropeans + the US or China.
with trillions in surplus and uncanny ability to hoard resource China has at its disposal a population of very hard working 1B+ strong while the US is barely functioning with majority lazy 300M+ population,with china you have a nation that is extremely hunger for more,from the villager to the president,with the US you have a former champion in his heyday.

Xijinping promised over $20B+ in economic aid, while the entire G8 is struggling to offer just over $4B in 7 years.

while the western world is busy giving us "clean" AID with zero corruption tolerance,which is a great way to keep AID low,as they are sure as hell African leaders and corruption is like "chanda na pete", China is showering our leaders with billions of AID and investment projects worth even more in quick succession,

All i can say is its never been a greater time to be an African Leader.Mangungos and Kimweris of the past aint got nothing on the Kikwetes and such of our current generation.our leaders have all the swag to not listen to us.why would they when they have the US and China all willing to keep the status quo?
 
Kwani Tz kuna nini cha ajabu mpaka uhisi unaibiwa? watanzania tuna roho nyembamba sana inayofanana kabisa na hali yetu ya umaskini kiasi cha kuhisi umaskini wetu ni kwa sababu ya watu fulani wanatuibia, jambo ambalo ni ushezi na ni kutokana na uwezo mdogo tulionao wa kufikiria.

Nikushukuru kwa mchango wako, lakini pia ungewaomba radhi watanzania wenzako kwa kudai wana uwezo mdogo wa kufikiri. Naamini wewe pia ni mtanzania, na kwa kunyambua hiyo sentensi yako inakujumlisha na wewe.

Uwezo mdogo wa kufikiri huonekana pale mtu anapopewa fursa ya kuzungumza na kuja na majibu mepesi katika maswali magumu.

Hoja ndio kipimo cha uwezo wa mtu kufikiri. Kuna kitu kinaitwa effective communication, hii hujumuisha kusikiliza, kuchambua na kuzungumza. Hapa ndio watu wengi ufeli.

Naomba urejee kwenye kipengere cha TAFAKARI na utaelewa mada hii inalengo gani.
 
Duh hongera kaka kwa uchambuzi wa kitafiti kweli Tanzania sasa tumegeuka uwanja wa mapambano wa Mataifa haya yenye nguvu kubwa ya kijeshi na kiuchumi duniani.

Kwanini mwalimu Nyerere alivyotutoka tu, Tanzania imekuwa kimbilio la wawekezaji kwa kasi ya ajabu? Mimi najiulizaga sipati jibu.
 
Mheshimiwa umefanya uchambuzi wa kisayansi.

Historia hujirudia yenyewe. Sababu kubwa ya utumwa, ukoloni na hata utandawazi ni manufaa ya kiuchumi kwa mbinu mbali mbali.

Tanzania tupo loosers siku zote. Nchi zote kubwa zinawekeza kwenye tafiti katika nyanja zote, lakini nitolee mfano wa watafiti tunaowadharau sana, yaani anthropologists, hawa hujifunza mila na desturi ya jami, mara nyingi hawa watafiti huishi miongoni mwa watu wanao wajufunza na hasa vijijini. Utafiti huu hutumika kupata wanachotaka kwa jamii kwa kutumia mila na desturi zao. Enzi za Livingstone wa sasa. Inaaminika kila anthropologist ni agenti wa shirika la kijasusi la nchi yake.

Tafiti nyingine ambayo zinafanywa na hawa watu ni Ethnography, hapa mtafiti humjifunza mtu binafsi, kitugani anakipenda, asichopenda, namna nzuri ya kumshawishi nk. labda ili mnielewe ni vizuri niweke mfano wa rais Mkapa. Mkapa kabla ya kuingia kwenye madaraka alikuwa inocent, kwa kweli hakuwa mla rushwa na labda hata yeye anashangaa aliingiaje humo. lakini kwa wanaomfahamu Mkapa ni mtu mwenye kupenda kusifiwa, kutambuliwa na kuthaminiwa. Ni mtu ambaye akikuamini hatasikia ya wenginena hapendi kuwa critisied. Lakini pia ni mtu wa kupenda sana maendeleo na aaonekane amefanya kazi nzuri inayopimika. Sasa angalia jinsi gani walivyoweza kutumia weakness na strength zake ili kufanikisha malengo yao. Makamu mwenyekiti wa globalisation! Misaada waliyo mimina na yeye alivyofunguka. ------,wanamsaidia sana kwa kwendana na interest zake hawa ndio wanatumia mbinu za Carl petro wa leo kwa mangungo wetu Ze mkapa na Mr fast jet
 
Uchambuzi umetulia sana, ila kiukweli sisi hatuna jinsi maana hawa jamaa wana visa vingi, hawakawii kuhamishia vita huku. loh
 
Kwanini mwalimu Nyerere alivyotutoka tu, Tanzania imekuwa kimbilio la wawekezaji kwa kasi ya ajabu? Mimi najiulizaga sipati jibu.

Usitafute jibu ya yaliyokwishajili, jikite kuangalia ni fursa zipi zipo mezani, upande gani uelekee au uelekeze nguvu kama nchi na pia kama mwananchi mmoja mmoja.

Kuja watakuja na hawazuiliki, ndio sababu nakuuliza tumeipangaje Taifa Stars na mechi hizi?? Kocha wetu ana mikakati ipi? Anakinoa kikosi vipi? Amepeleka timu kambini? Au vijana wanapiga nyama choma na moja moto moja baridi.

Mashabiki nao wanahali gani?? wako tayari kushangilia timu kwa sauti na wingi hadi ushindi upatikane au wataungana na wapinzani wetu kuivunja nguvu Taifa Stars sababu wanapenda mchezo wa Messi, Puyol, Pique? Au wanapenda kasi ya Ronaldo, Kaka, Ramos, Alonso?
 
Mheshimiwa umefanya uchambuzi wa kisayansi.

Historia hujirudia yenyewe. Sababu kubwa ya utumwa, ukoloni na hata utandawazi ni manufaa ya kiuchumi kwa mbinu mbali mbali.

Tanzania tupo loosers siku zote. Nchi zote kubwa zinawekeza kwenye tafiti katika nyanja zote, lakini nitolee mfano wa watafiti tunaowadharau sana, yaani anthropologists, hawa hujifunza mila na desturi ya jami, mara nyingi hawa watafiti huishi miongoni mwa watu wanao wajufunza na hasa vijijini. Utafiti huu hutumika kupata wanachotaka kwa jamii kwa kutumia mila na desturi zao. Enzi za Livingstone wa sasa. Inaaminika kila anthropologist ni agenti wa shirika la kijasusi la nchi yake.

Tafiti nyingine ambayo zinafanywa na hawa watu ni Ethnography, hapa mtafiti humjifunza mtu binafsi, kitugani anakipenda, asichopenda, namna nzuri ya kumshawishi nk. labda ili mnielewe ni vizuri niweke mfano wa rais Mkapa. Mkapa kabla ya kuingia kwenye madaraka alikuwa inocent, kwa kweli hakuwa mla rushwa na labda hata yeye anashangaa aliingiaje humo. lakini kwa wanaomfahamu Mkapa ni mtu mwenye kupenda kusifiwa, kutambuliwa na kuthaminiwa. Ni mtu ambaye akikuamini hatasikia ya wenginena hapendi kuwa critisied. Lakini pia ni mtu wa kupenda sana maendeleo na aaonekane amefanya kazi nzuri inayopimika. Sasa angalia jinsi gani walivyoweza kutumia weakness na strength zake ili kufanikisha malengo yao. Makamu mwenyekiti wa globalisation! Misaada waliyo mimina na yeye alivyofunguka. ------,wanamsaidia sana kwa kwendana na interest zake hawa ndio wanatumia mbinu za Carl petro wa leo kwa mangungo wetu Ze mkapa na Mr fast jet

Kwa ufupi kabisa, maendeleo uja pale mwanadamu anapotambua mazingira yake na changamoto zinazomzunguka. Kisha baada ya apo utumia yale yanayopatikana kwenye mazingira yake kupata ufumbuzi wa hizo changamoto.

Norway ndio vinara wa kuvuna gesi bahari kuu na kutengeneza mitambo na vyombo vinayoweza pasua kwenye bahari kuu na hata barafu. Wanataasisi yao ya utafiti wa mambo ya baharin inaitwa Aker Actic Research.

Visiwa vya Japan vvimelala katika ufa mpana sana unaojulikana kama Pacific rim of fire. Hili ndilo jiko la matetemeko, kutokana na changamoto hiyo wao wameweza kujenga ghorofa zinazonepa kulingana na mtikisiko utokanao na tetemeko.

Netherland ni nchi yenye ardhi ndogo lakini inamahitaj makubwa, kwa iyo wamewekeza katika teknolojia ya kukomboa na kutanua maneneo ya pwani ilikupata ardhi ya kujenga. Singapore pia wanachangamoto hizo hizo, ni nchi yenye ukubwa sawa na jiji la Dar es Salaam lakini ina wakaaz wengi. Hivyo wao wamekeza katika ujenzi wa maghorofa marefu kwa ofis na makazi huku wakijitahid kupeleka shughuli nying underground kama vile reserve yao ya mafuta na maji.
 
Kwani Tz kuna nini cha ajabu mpaka uhisi unaibiwa? watanzania tuna roho nyembamba sana inayofanana kabisa na hali yetu ya umaskini kiasi cha kuhisi umaskini wetu ni kwa sababu ya watu fulani wanatuibia, jambo ambalo ni ushezi na ni kutokana na uwezo mdogo tulionao wa kufikiria.
we lazma ni mwana ccm
 
. Ningependa kidogo muelewe
na ntaweka baadhi ya
vithibitisho kutoka vyanzoa mbalimbali
nini hasa ni sababu ya safari hii.


KWANZA:.
.Hapa chini
nimeweka linki ya dokumentari ya Aljazeera ambayo inaongelea uporaji ardhi mkubwa na pia naweka
na video ya taarifa za kiintelijensi za mikakati ya mataifa makubwa:

Uporaji ardh
i: Our Man in Sudan - Witness - Al Jazeera English
Intelijensia: imeambatanishwa




HITIMISHO:
Kwa waliomudu kutazama taarifa ya habari juu ya mkutano wa Obama na Xi, utaona jinsi Obama
alivyojawa na wasiwasi hata sauti yake ilikuwa kama inatetemeka
. Pili mkutano ule haukuwa pale
Washington kama vile viongozi wengine wanapokuwa wameenda USA kukutana na raisi wa Marekani,
mkutano huu unafanyika California, eneo lilipendekezwa na Xi na watu wake. Obama na timu yake
wameitwa kukutana na Xi, na si vinginevyo,
Tazama Aljazeera na utaona hata maelezo ya habari hiyo
leo yanaandikwa tofauti. Nimeambatanisha screenshot. China sasa ndio SUPER POWER!!!
View attachment 96829

TAFAKARI:
Kwa kutumia mfano wa timu za mpira (wengi wetu ni wadau)
China = Barcelona (Young, inteligent players, financially sound and ambitious)
USA = Real Madrid (Ageing giant, talented players, financially fit, has lost bearings)
Tanzania = Taifa Stars (Rookie, money-hungry players,ambitious coach -> JK and highly hopeful fans)


.

kwa kifupi ni kwamba wewe ni mpiga debe wa wachina, sioni kama unakemea kwa dhati uporaji wa maliasi za afrika kama ulivyolenga, umefikia hatua kutuaminisha haya Nakunukuu
PHP:
Pili mkutano ule haukuwa pale 
Washington kama vile viongozi wengine wanapokuwa wameenda USA kukutana na raisi wa Marekani, 
mkutano huu unafanyika California, eneo lilipendekezwa na Xi na watu wake. Obama na timu yake 
wameitwa kukutana na Xi, na si vinginevyo,
REALLY? kwa nini asingemuita huko china kabisa? mbona ujaweka nukuu ya hiyo maana ulidokeza mwanzo kwamba utaweka marejeo.
Kuna sehemu umegusia kwamba vijana wengi wa kiafrika/Tanzania sio wachunguzi kwamba tunasikiliza kwamba kinachosemwa kwenye media mfano blogs etc etc kwamba hivyo ni vyombo vya propadanga kisha na wewe ukaweka propaganda ya waarabu kupitia ALJAZEERA,!!!!
Mkuu huna moral authority wa assumption uliyotoa maana una bepari mfukoni mwako pia
 
Liganga Nimefurahishwa na uchambuzi wako.Isipokuwa nataka nikuulize kuwa mbona sasa ni zaidi ya miaka 55 miongo mingi sana , Tangu wakoloni waanze kuondoka kwenye hili bara la africa na kuwaacha waafrica wajitawale na kujiendeshea mambo yao wenyewe, kwa masikitiko makubwa hakuna walichokibadilisha, hata ile miondo mbinu kidogo waliyotuachia, na baadhi ya viwanda na pamoja na rasilimali nyingi walizotubakishia havijatuongezea kasi yeyote ya maendeleo kwa kasi ukilinganisha na walivyokuwepo wakoloni.(sio kwamba naunga mkono ukoloni).

Kama Tanzania walishindwa kujiendeleza wenyewe takriban miaka zaidi ya 50 tangu uhuru 1961, itawezekana lini kujitambua na kujiendeleza yenyewe bila kutumia haya mataifa makubwa ya nje? Tanzania ya leo yenye watu milioni 46 wanashindwa kujitosheleza chakula kwa mwaka mmoja, achilia mbali kuwa na uwezo wa technolojia kubwa ya kuchimba mafuta, madini na gesi..?

Tunatatizo kubwa kama taifa, nalo ni kusimamia na kuheshim taratibu na miiko. Baada ya uhuru tulianzisha viwanda zaidi ya 340 na vyote vilikuwa ni vinatumia malighafi ya ndani kwa asilimia zaid ya 50%. Kama vile vya nguo, ngozi, kusindika kahawa na chai. Hii ilikuwa ni hatua kubwa kuelekea mbele. Nakumbuka tulimudu kununu meli kadhaa kutoa huduma baharini na kwenye maziwa. Tuliiboresha bandari ya Dar kuwa na teknolojia ya kisasa kwa wakati huo, kuanzia kwenye tugs na gantry cranes.

Vile vile tuliwekeza kwenye uwanja wa kisasa wa ndege pale terminal II. Bado naamini tulikuwa na mwanzo mzurim tulijenga maofisi ya ghorofa kwa wizara mbalimbali na mengineyo. Hizi zote zilikuwa ni peasa za ndani. Wakulima nao walikazana na waliona matunda ya bidiii yao, walivuna pamba, kahawa na chai kwa wingi. Nakumbuka mkulima mzalendo wa pamba na kahawa walimuhudu kununua malori mapya ya bedford na trekta. Leo sijui kama kuna mkulima mzalendo wa mazao haya anayemudu kununua hata fuso used achilia Scania. Mambo haya yaliwezekana kutokana na usimamizi na mipango.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom