SABABU: Ujio wa Obama na timu ya watu 700

SABABU: Ujio wa Obama na timu ya watu 700

Kwa kuwa ni wazungu wanakuja hakuna tabu,ingekua ni dege la mfalme wa uarabuni anakuja na umati wote huo pangechimbika kwa matusi

Kitu gani kinakupa amani juu ya wazungu. Natumai umesoma historia na unakumbuka nani alikuwa mkoloni wa taifa lako na majirani zako. Pia ni matumaini yangu ulipata kusikia kuhusu biashara moja iliyokuwa inalipa sana, na ilivuma mno miaka ya nyuma, biasharar hiyo ilifaamika kama biashara ya WATUMWA. Wadau wakubwa wa biashara hiyo walikuwa ni WAZUNGU na WAARABU.

Sasa tafakari kama unao unafuu wowote kwa ujio wa mmoja wao badala ya mwingine.
 
Umesomeka mkuu!! Hapa kwa mwenye macho haambiwi tazama,,, ni kweli haya Mabepari huwa hayaendi kwa hasara!
 
Katika mwaka 2013; hii ni makala namba moja yenye maana iliobeba nadharia na historia kuhusiana wapi dunia ipo na inapoelekea.
 
Hakuna kizuri kinakuja na nchi ya magharibi kama siyo kuweka base ya kijeshi,kutafuta sehemu ya kutupa uchafu wao wa nyuklia au kutaka tukubali tukubali sera zao za ndoa za mashoga na kuwaunga mkono pale wanapotaka kuvamia nchi.
 
Kitu gani kinakupa amani juu ya wazungu. Natumai umesoma historia na unakumbuka nani alikuwa mkoloni wa taifa lako na majirani zako. Pia ni matumaini yangu ulipata kusikia kuhusu biashara moja iliyokuwa inalipa sana, na ilivuma mno miaka ya nyuma, biasharar hiyo ilifaamika kama biashara ya WATUMWA. Wadau wakubwa wa biashara hiyo walikuwa ni WAZUNGU na WAARABU.

Sasa tafakari kama unao unafuu wowote kwa ujio wa mmoja wao badala ya mwingine.

Wazungu wametuaminisha kuwachukia waarabu,huko uchumi wa wazungu wote unategemea soko la uarabuni
 
Lakini kama kaOBAMA alichaguliwa maalumu kwa lengo hilo kwanini hakuja kipindi chake cha kwanza?.
 
Huo ni mtizamo wako tu, Rais wa mataifa yaliyoendelea wakisema waje kufanya ziara huku mnafikiria kunyang'anywa ardhi na rasilimali zingine ila nyie Rais wenu akienda huko mnaona poa tu eti anaenda kutafuta masoko na fulsa za uwekezaji...SAWA lakini mara nyingi tuwe tunaangalia mambo (hizi ziara) kwa mtazamo CHANYA na kujitengenezea fulsa za kupata chochote potential kupitia ziara hizo na sio daily kulalamika kama MAHAYAWANI. utajiri wa china au marekani haunihusu mimi maana hata TZ yetu ina mazuri yake na mabaya yake.

Mara ngapi watu wanamdiscredit jakaya na safari zake zisizo za msingi kwenda kuombaomba na kusababisha deni la taifa likue??!!
Cha ajabu anaomba msaada hadi wajamaica juu ya walimu wa sayansi na michezo..
this is a serious disaster!
juu ya obama kuja hapa mpaka siku ukija kushtuka upo nchi ya watu yaani umeshauzwa bila kujua usishangae!
come forward with cogently arguments kama mwenzako alivyofanya sio personal attack!
 
Umesomeka mkuu!! Hapa kwa mwenye macho haambiwi tazama,,, ni kweli haya Mabepari huwa hayaendi kwa hasara!

Yaani huwa yanakuwa rafiki yako unapokuwa na kitu tu...
Aisee hii micapitalist....
Ni zaidi ya ukimwi!
 
Wazungu wametuaminisha kuwachukia waarabu,huko uchumi wa wazungu wote unategemea soko la uarabuni

What they all think about is permanet interest...
Ukikubali kuchunwa basi we unafuata haki za binadamu!
 
Lakini kama kaOBAMA alichaguliwa maalumu kwa lengo hilo kwanini hakuja kipindi chake cha kwanza?.

Wakoloni wetu walipanga kurejea tena Africa, lakini sio kwa kasi ila kwa utaratibu ambao hatutastuka kuwa wanarudi kututawala. Kwa makadirio yao na jinsi wanavyotuelewa walijua kuwa kamwe hatutaweza kujikomboa na tutafungua milango na kuwakaribisha tena.

Bahati mbaya katika nadharia ya kiuchumi hawakutaraji injini ya Jiefang(China)ingekuwa na kasi, waliiona ni dhaifu ukilinganisha na injini ya Rolly Royce (England), Ferarri(Italy),Benz(German), Toyota(Japan) na Ford(Marekani). Chumi za mataifa haya ziliisha paa zamani sana.

Pia ilikuwa haijawahi kutokea na haikutarajiwa taifa lililowahi kutawaliwa (koloni) likaweza kukua kiuchumi na kulipita taifa lilokuwa na makoloni. China ni nchi pekee iliyowahi kutawaliwa na sasa ni taifa kubwa kiuchumi. Wajapani waliitawala china kwa muda mrefu mno.
 
sijawahi kukutana na uchambuzi na fikra za hali ya juu kama hizi, hakika mtoa mada umenikosha sana kwa kweli
 
Liganga, huu ni uchambuzi mzuri na makini "think out of the box"

Ni rejee kwenye TAFAKARI hapo juu ambapo kinadharia naona mwamuzi wa kati ndio amebeba hatma ya mchezo huu. Kwa hakika mechi hii inahitaji mchezo wa kiu-ungwana (fair play) ili mashabiki wafurahie.

Obama na Rais XI: vituo vingi vya habari vimetangaza ni mkutano utakaojadili mambo ya Cyber Protection na kuangalia namna nzuri ya kuzuia Udukuzi unaofanywa na Uchina kwa taifa la marekani kiasi cha kuhatarisha biashara kubwa za wawekezaji wa Kimarekani, kuna madai ya siri za kampuni ya GOOGLE kuingiliwa na makampuni ya Uchina kwa Masada wa jeshi la nchi hiyo, mfano mwingine anaolalamikia Marekani ni jinsi Uchina alivyoiba siri za ndege zake aina ya F-35 na sasa Uchina anatengeneza mwenyewe.

Yapo mambo kadha wa kadha Merekani anadai kuchezewa faulo na Uchina. Nami nimalizie kwa kusema Uchina ni Barcelona katika soka!

Copy kahtaan
#
Izz,
mwenye kuanzisha thread hii amesahau kitu kimoja ambacho tunakisoma na kukiskiliza kila siku kwenye tvs na radio, kuwa HISTORIA INATABIA YA KUJIRUDIA!, Siku zoote na miaka yote, tokea empire over 2000 yrs ago,
Taifa llt lililoko juu hofu yake kubwa ni ! lisitokee taifa lingine ambalo kwa namna moja au nyingine linaonekana kulishinda lingine,

wakati huo (romans and abisinians and pershians almost 2000 yrs ago) kesi zao zilikuwa hazina tofauti saana na hizi za leo baina ya hawa super powers,
Ukiangalia american na china, wote ni nyuklia power nation{ hapa sio nyuklia ya kutengeneza umeme, LA HASHA, HII NI YA KUUA KWA WINGI INAPOTUMIKA!} KWA HIVO hata mabishano yao hayawi makali kama vile america na cuba, au venezuela inapokuja kwenye threat,

Sasa taifa dogo linapoonekana kuwa tishio basi hawa mabeperiri kama americans and europeans huibana hiyo nchi kuanzia kwenye uchumi na biashara na ikishindikana huitafutia sababu yyt na kuitishia hata kuiingilia kivita, mifano ni mingi tu, north korea, iraq, iran n.k huutangazia ulimwengu ubaya wa kubumba ili kuinyamazisha ,

Lakini kwa nchi km china mbinu hizi haziwezi kufanya kazi, hata fujo inayotokea ndani ya china wamerekani hata comment hawatoi,

Sisi wanyonge ni watazamaji tu, tunaangalia nani atakae endelea kuelea kwenye ulimwengu huu wa ushindani??

Tamaa imeponza mataifa mengi mmno! sisi yetu macho na maji yakizidi unga Mi baba narudi kijijini nikaanze ufugaji tena,
 
  • Thanks
Reactions: Izz
sijawahi kukutana na uchambuzi na fikra za hali ya juu kama hizi, hakika mtoa mada umenikosha sana kwa kweli

Nashukuru.

Natumai nafungua ukurasa mpya wa ile JamiiForum tuliyoifahamu zamani (2006-2008) kama "Home of the Great thinkers". Nimerejea tena kwenye jahazi la Great Thinkers nikiamini mwaka huu tunaanza historia mpya.
 
Liganga

Hakika umejitahidi kwa kadiri ulivyona ujio wa hawa mapapa hapa Nchini.
Mi naona kama Tanzania yetu ni kama Mwanamke mzuri wa sifa zote na sasa kila Mwanaume anatamani awe mkewe na hata ikiwezeka aolewe kabisa.
Utumwa inaweza isiwe mbali kwa wanainchi serikali legelege isipokuwa makini!
 
Last edited by a moderator:
Katika mwaka 2013; hii ni makala namba moja yenye maana iliobeba nadharia na historia kuhusiana wapi dunia ipo na inapoelekea.

Nashukuru,

Ni imani yangu kuwa kuna mengi mazuri tunaweza kuyafanya na kuboresha ustawi wetu na bara letu iwapo tutaamini kuwa tunaweza, kuthamini na kuheshimu michango ya watu wetu na kuifanyia kazi pasipo kuogopa.
 
#
Izz,
mwenye kuanzisha thread hii amesahau kitu kimoja ambacho tunakisoma na kukiskiliza kila siku kwenye tvs na radio, kuwa HISTORIA INATABIA YA KUJIRUDIA!, Siku zoote na miaka yote, tokea empire over 2000 yrs ago,
Taifa llt lililoko juu hofu yake kubwa ni ! lisitokee taifa lingine ambalo kwa namna moja au nyingine linaonekana kulishinda lingine,

wakati huo (romans and abisinians and pershians almost 2000 yrs ago) kesi zao zilikuwa hazina tofauti saana na hizi za leo baina ya hawa super powers,
Ukiangalia american na china, wote ni nyuklia power nation{ hapa sio nyuklia ya kutengeneza umeme, LA HASHA, HII NI YA KUUA KWA WINGI INAPOTUMIKA!} KWA HIVO hata mabishano yao hayawi makali kama vile america na cuba, au venezuela inapokuja kwenye threat,

Sasa taifa dogo linapoonekana kuwa tishio basi hawa mabeperiri kama americans and europeans huibana hiyo nchi kuanzia kwenye uchumi na biashara na ikishindikana huitafutia sababu yyt na kuitishia hata kuiingilia kivita, mifano ni mingi tu, north korea, iraq, iran n.k huutangazia ulimwengu ubaya wa kubumba ili kuinyamazisha ,

Lakini kwa nchi km china mbinu hizi haziwezi kufanya kazi, hata fujo inayotokea ndani ya china wamerekani hata comment hawatoi,

Sisi wanyonge ni watazamaji tu, tunaangalia nani atakae endelea kuelea kwenye ulimwengu huu wa ushindani??

Tamaa imeponza mataifa mengi mmno! sisi yetu macho na maji yakizidi unga Mi baba narudi kijijini nikaanze ufugaji tena,
kahtaan, ahsante kwa kuturejesha kwenye history kidogo, ni vema kukumbuka nyuma wakati ukielekea mbele.

Ni wakati wa kusema kupitia hapa namna nzuri ya kuzitumia rasilimali zetu ambazo hao "super powers " wanazitolea macho, sio tu ziwafaidishe wao pindi wanapokuja nchini bali sisi tuliopo na kizazi kijacho.
 
Last edited by a moderator:
Kutokusikilizwa na kuupuzwa kwa ‘wanasystem’ wetu kumesababisha hadi mambo nyeti na makubwa kama haya yaletwe kujadiliwa hapa ili kupata public sympathy badala ya kupelekwa kwa ‘wakubwa’ wayafanyie kazi. Nimestuka sana kusoma mambo kama haya mtandaoni, kimsingi hayakupaswa kuwa hapa ingawa ni faraja sana kuyaona hapa pia.
 
kahtaan, ahsante kwa kuturejesha kwenye history kidogo, ni vema kukumbuka nyuma wakati ukielekea mbele.

Ni wakati wa kusema kupitia hapa namna nzuri ya kuzitumia rasilimali zetu ambazo hao "super powers " wanazitolea macho, sio tu ziwafaidishe wao pindi wanapokuja nchini bali sisi tuliopo na kizazi kijacho.

Raslimali bora na yenye thamani kuu ni WATU. Tuanze kwa kuwajenga watu wetu kuwa
-wazalendo,
-wenye mtazamo wa mbali (Vision),
-wanaojitegemea na si wale wanaosubiri serikali iwafanyie vitu
-wenye mipango ya mda mrefu inayooana na mahitaji ya nchi
-wenye elimu bora na ya kisasa inayoendana na mahitaji ya mazingira yaliyowazunguka na si KKK tu.
-watafiti na wagunduzi
-wenyekuthubutu na kupenda kuona matokeo na si kuridhika na maneno matupu

Tukimudu apo basi mengine yanayohusu raslimali kama miundombinuni, usimamizi, uongozi na uwekezaji yatafuata.
 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: Izz
Raslimali bora na yenye thamani kuu ni WATU. Tuanze kwa kuwajenga watu wetu kuwa
-wazalendo,
-wenye mtazamo wa mbali (Vision),
-wanaojitegemea na si wale wanaosubiri serikali iwafanyie vitu
-wenye mipango ya mda mrefu inayooana na mahitaji ya nchi
-wenye elimu bora na ya kisasa inayoendana na mahitaji ya mazingira yaliyowazunguka na si KKK tu.
-watafiti na wagunduzi
-wenyekuthubutu na kupenda kuona matokeo na si kuridhika na maneno matupu

Tukimudu apo basi mengine yanayohusu miundombinuni, usimamizi, uongozi na uwekezaji yatafuata.
Liganga, nakubaliana na wewe mkuu. Pia tunatakiwa kuondoa mawazo mgando ya baadhi ya watu kuamini kila jambo ni lazima lifanywe na serikali, wakisahau kua mimi na wewe ndio serikali na tunaweza kuleta maendeleo tukiwa na UZALENDO
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom