Nyanidume
JF-Expert Member
- Oct 24, 2012
- 2,411
- 1,153
Mtoto wa aliyekuwa kiongozi wa Libya, kanali Muammar Gaddaf, Saad amekamatwa na maofisa usalama huko nchini Nigeria, habari nilizozipata hivi punde kupitia redio RFA zinasema kwamba, Saad amekamatwa pamoja na baadhi ya maofisa waliokuwa katika serikali ya baba yake, kati ya maofisa hao ni aliyekuwa mkuu wa televisheni ya nchi hiyo. Saad alikimbilia nchini Niger ambako alihifadhiwa huku serikali ya nchi hiyo ikikataa kumkabidhi Tripol. Utawala wa Tripol umetuma ujumbe wake nchini Nigeria ili kuzungumza na serikali ya nchi hiyo ili wakabidhiwe watu hao.