Damaso
JF-Expert Member
- Jul 18, 2018
- 6,132
- 10,514
Dunia ya muziki wa Tanzania imekuwa ikipitia mageuzi makubwa kwa miongo kadhaa. Kila zama imezaa nyota zake – kuanzia wasanii, watunzi, waimbaji, hadi watayarishaji muziki (producers). Katika zama hizi za mitandao ya kijamii, kumekuwa na tabia ya baadhi ya watu kujianika hadharani na kujinadi kuwa wao ndio number one kwenye sekta fulani.
Hivi karibuni, jina la Salmin Kasimu Maengo maarufu kama S2KIZZY limekuwa gumzo baada ya kujinasibu hadharani kuwa ndiye producer namba moja wa muda wote ndani ya muziki wa Tanzania, akifanya hivyo kwenye vituo kadhaa vya habari.
Kauli hii imeibua mjadala mzito, ikizingatiwa kuwa Tanzania imewahi na bado ina watayarishaji waliopiga hatua kubwa, wakatengeneza alama zisizofutika kwenye historia ya muziki wa kizazi kipya (Bongo Flava).
Kabla S2kizzy hujazaliwa, Paul Matthysse maarufu kama P Funk Majani alikuwa akitikisa anga ya muziki. Huyu ndiye aliyebatizwa jina Mkono wa Mungu, kutokana na uwezo wake wa kutoa kazi bora ambazo hadi leo zinasalia kuwa alama za muziki.
Majani ndiye aliyekuwa nyuma ya nyimbo nyingi za TMK Wanaume Family, Juma Nature, Gangwe Mobb, na Dogo Janja wa miaka ile. Fikiria wimbo "Mzee wa Busara" wa Juma Nature au "Msela" – nyimbo zilizoweka msingi wa Bongo Flava na kubaki kwenye kumbukumbu za kila mpenzi wa muziki.
Kwa upande mwingine, Miika Mwamba lilikuwa jina linalotikisa sana katika miaka ya 2000. Alisifika kwa ubunifu na ubora wa utayarishaji uliosababisha nyimbo kadhaa kukua kimataifa. Wimbo kama "Darubini Kali" wa Afande Sele si tu ulikuwa wa kijamii, bali pia ulikuwa na ubora wa kipekee wa production.
Hii ilikuwa kazi ya producer mwenye upeo mkubwa, aliyeweka uzito kwenye sound na ujumbe wa nyimbo. Mzungu ambaye hakutaka umaarufu kabsa ndio maana kuna picha zake chache sana mitandaoni, kazi zake zinaishi mpaka kesho.
Producer bora huwa hafanyi kazi kwa kutafuta sifa, bali kazi zake hujieleza zenyewe. Fikiria nyimbo hizi:
Nyimbo hizi ni mifano hai kuwa Tanzania imebarikiwa na producers wenye vipaji vikubwa ambao walitengeneza miziki ya thamani isiyopimika.
Bwana mkubwa S2kizzy pasipo shaka ana mchango mkubwa sana, kwani amekuwa nyuma ya hits kama "Tetema" na "Amaboko" za wasanii Rayvanny na Diamond Platnumz, nyimbo zilizoitikisa Afrika na dunia.
Lakini je, kufanikisha nyimbo mbili tatu kubwa kunatosha kumfanya awe producer bora wa muda wote? Historia ya muziki wa Tanzania ni ndefu, na majina kama P Funk Majani, Mesen Selekta, Lamar, Maroza, Tudd Thomas na wengineo yameshafanya kazi ambazo zinaishi vizazi baada ya vizazi.
Producer bora hahitaji kujisifu. Ni jamii na historia ndizo zinazomvika taji. Sauti za muziki zinazodumu vizazi ndivyo ushahidi wa ubora wa kweli. Ubora wa kazi husika na heshima ya kazi yake vitaongea.
Kwa hiyo, badala ya kuanzisha majigambo na mabishano yasiyokuwa na faida, S2kizzy anapaswa kuacha kazi zake ziongee. Historia ya muziki wa Tanzania imeshaandikwa kwa wino usiofutika – na huenda siku moja, kama ataendelea kwa ubunifu na nidhamu, jina lake litaunganishwa rasmi na orodha ya vigogo.
Lakini kwa sasa, kofia ya dhahabu ya producer namba moja wa muda wote bado inabaki mikononi mwa wale waliopanda mlima huu mapema na kusimamisha bendera ya muziki wa Tanzania. Kama haujasikia majigambo kutoka kwa watu kama Tudd Thomas na wahenga wengine, kaa kwa kutulia brother.
Hivi karibuni, jina la Salmin Kasimu Maengo maarufu kama S2KIZZY limekuwa gumzo baada ya kujinasibu hadharani kuwa ndiye producer namba moja wa muda wote ndani ya muziki wa Tanzania, akifanya hivyo kwenye vituo kadhaa vya habari.
Kauli hii imeibua mjadala mzito, ikizingatiwa kuwa Tanzania imewahi na bado ina watayarishaji waliopiga hatua kubwa, wakatengeneza alama zisizofutika kwenye historia ya muziki wa kizazi kipya (Bongo Flava).
Kabla S2kizzy hujazaliwa, Paul Matthysse maarufu kama P Funk Majani alikuwa akitikisa anga ya muziki. Huyu ndiye aliyebatizwa jina Mkono wa Mungu, kutokana na uwezo wake wa kutoa kazi bora ambazo hadi leo zinasalia kuwa alama za muziki.
Majani ndiye aliyekuwa nyuma ya nyimbo nyingi za TMK Wanaume Family, Juma Nature, Gangwe Mobb, na Dogo Janja wa miaka ile. Fikiria wimbo "Mzee wa Busara" wa Juma Nature au "Msela" – nyimbo zilizoweka msingi wa Bongo Flava na kubaki kwenye kumbukumbu za kila mpenzi wa muziki.
Kwa upande mwingine, Miika Mwamba lilikuwa jina linalotikisa sana katika miaka ya 2000. Alisifika kwa ubunifu na ubora wa utayarishaji uliosababisha nyimbo kadhaa kukua kimataifa. Wimbo kama "Darubini Kali" wa Afande Sele si tu ulikuwa wa kijamii, bali pia ulikuwa na ubora wa kipekee wa production.
Hii ilikuwa kazi ya producer mwenye upeo mkubwa, aliyeweka uzito kwenye sound na ujumbe wa nyimbo. Mzungu ambaye hakutaka umaarufu kabsa ndio maana kuna picha zake chache sana mitandaoni, kazi zake zinaishi mpaka kesho.
Producer bora huwa hafanyi kazi kwa kutafuta sifa, bali kazi zake hujieleza zenyewe. Fikiria nyimbo hizi:
- "Barua" – Daz Nundaz, production ya Miika Mwamba, nyimbo ambayo ilimwinua kundi la Daz Nundaz kuwa kundi lililopendwa sana ndani ya Tanzania.
- "Nikusaidiaje" – TID, production ya P Funk, nyimbo ambayo ilimwinua TID kuwa superstar.
- "Eno Maiki" – Ziggy Dee, production ya Miika Mwamba, nyimbo ambayo ilimwinua na kumfanya Ziggy kuwa superstar ndani ya Tanzania.
- "Ndio Mzee" – Professor Jay ft. Juma Nature, production bora sana ambayo ilitengeneza anthem ya vijana wa Tanzania miaka ya 2000.
- "Kamanda" – Daz Nundaz, kazi nyingine ya Miika Mwmba.
- "Chuki" – Gangwe Mobb, mojawapo ya nyimbo za kwanza kupeleka street rap mainstream.
- "Tamala" – Hardmad, mojawapo ya nyimbo bora sana ya mapenzi, wimbo ambao mdundo wake tu ni unique.
Nyimbo hizi ni mifano hai kuwa Tanzania imebarikiwa na producers wenye vipaji vikubwa ambao walitengeneza miziki ya thamani isiyopimika.
Bwana mkubwa S2kizzy pasipo shaka ana mchango mkubwa sana, kwani amekuwa nyuma ya hits kama "Tetema" na "Amaboko" za wasanii Rayvanny na Diamond Platnumz, nyimbo zilizoitikisa Afrika na dunia.
Lakini je, kufanikisha nyimbo mbili tatu kubwa kunatosha kumfanya awe producer bora wa muda wote? Historia ya muziki wa Tanzania ni ndefu, na majina kama P Funk Majani, Mesen Selekta, Lamar, Maroza, Tudd Thomas na wengineo yameshafanya kazi ambazo zinaishi vizazi baada ya vizazi.
Producer bora hahitaji kujisifu. Ni jamii na historia ndizo zinazomvika taji. Sauti za muziki zinazodumu vizazi ndivyo ushahidi wa ubora wa kweli. Ubora wa kazi husika na heshima ya kazi yake vitaongea.
Kwa hiyo, badala ya kuanzisha majigambo na mabishano yasiyokuwa na faida, S2kizzy anapaswa kuacha kazi zake ziongee. Historia ya muziki wa Tanzania imeshaandikwa kwa wino usiofutika – na huenda siku moja, kama ataendelea kwa ubunifu na nidhamu, jina lake litaunganishwa rasmi na orodha ya vigogo.
Lakini kwa sasa, kofia ya dhahabu ya producer namba moja wa muda wote bado inabaki mikononi mwa wale waliopanda mlima huu mapema na kusimamisha bendera ya muziki wa Tanzania. Kama haujasikia majigambo kutoka kwa watu kama Tudd Thomas na wahenga wengine, kaa kwa kutulia brother.