X-PASTER
JF-Expert Member
- Feb 12, 2007
- 11,604
- 1,858
Rwanda yajiunga rasmi na Jumuiya ya Madola
Bendera ya Rwanda inatarajiwa kupeperushwa kwa mara ya kwanza mjini London, katika makao makuu ya jumuiya ya madola.
Rwanda ambayo ilikuwa koloni ya Ubelgiji, ilijiunga kama mwanachama wa hamsini na nne wa jumuiya hiyo ambayo hutumia kiingereza kama lugha rasmi Novemba mwaka uliopita.
Waandamanaji wamesema watafanya wataandamana kulalamikia rekodi mbovu ya haki za kibinadam ya Rwanda.
Lakini akiongea na BBC, waziri wa masuala ya nchi za kigeni wa Rwanda Louise Mushikiwabo amesema raia wenzake wa Rwanda wana haki zote wanazohitaji.