Watanzania bwana hakuna hata mtu anaeshauri kwanini serikari inunue ndege kutokana na argument ya business opportunity iliyopo. Kitu tunachojua Kenya iliyo invest kwenye viwanja vya ndege kadhaa vyenye hadhi, inayopokea wageni wengi annually kushinda Tanzania na ilipojaribu kusema ifanye investment kwenye ndege imeshia kutafuta madeni makubwa tu.
Leo hii Tanzania ambayo mashirika makubwa kama BA inayofuta hizo route kwa sababu hakuna commercial benefit, KLM ambayo ndege nyingi uishia Kenya kuliko zinazokuja Tanzania direct. Katika mazingira hayo ya kibiashara sisi tunataka serikari ifanye investment ya ndege kubwa kwa kukopa unazipeleka wapi au kuna gap gani ya kushindana kwa ATCL?
Serikari ya Kagame inajulikana kwa kukopa na bunge lake limeshaonyesha huo wasiwasi wao na kwa Kagame wala sio swala linalomsumbua, nadhani kabla auja iga kilakitu tunatakiwa tujiulize kukopa $160+interest hizo ndege zinalipaje hilo deni kwanza na deni lenyewe ni la muda gani.
Mashirika ya ndege yaliyo jaribu tu kufanya strategies za lower prices to lure volume yameishia kufa hao wateja wako wapi wa kuwakopea ndege mpya in the first place, watu awakurupuki nadhani ajira ni tatizo linaloitaji investment zaidi kuliko hili tatizo la kutokuwa na ndege.