Ruto: Uwanja wa Talanta tutaupa jina la Raila Odinga

Ruto: Uwanja wa Talanta tutaupa jina la Raila Odinga

DuaZaMama

JF-Expert Member
Joined
Jun 2, 2025
Posts
1,882
Reaction score
4,129
RAIS WA KENYA, Dr William Samoei Ruto amethibitisha rasmi kuwa uwanja mpya wa Talanta Sports City unaojengwa eneo la Jamhuri pale Nairobi utakapokamilika utapewa jina la RAILA AMOLLO ODINGA STADIUM kwa heshima ya Nguli wa siasa za Kenya na Ziwa Victoria aliyekuwa Kiongozi wa Upinzani nchini humo.
 
Unafiki tu,kwani hakuwa hai majuzi tu hapo kwanini msingempa hiyo heshima akafa akijua kwamba na yeye alikuwa mtu ktk watu?
 
Vizuri.
Mara nyingi wafu hukumbukwa kwa mazuri yao.
 
Unafiki tu,kwani hakuwa hai majuzi tu hapo kwanini msingempa hiyo heshima akafa akijua kwamba na yeye alikuwa mtu ktk watu?
Monuments hupewa majina ya watu walikwishafariki, siyo kama Nobel prize kuwa itolewe kwa watu walio hai tu. Ni ujing na aibu sana kutumia jina la mtu aliye hai kwenye monument yoyote ile. Enzi za Nyerere, hakutaka jina lake litumike kwenye monument yoyote, ingawa Shinyanga walipiga chenga kidogo wakauita uwanja wao kuwa wa Kambarage (siyo Nyerere).
 
Monuments hupewa majina ya watu walikwishafariki, siyo kama Nobel prize kuwa itolewe kwa watu walio hai tu. Ni ujing na aibu sana kutumia jina la mtu aliye hai kwenye monument yoyote ile. Enzi za Nyerere, hakutaka jina lake litumike kwenye monument yoyote, ingawa Shinyanga walipiga chenga kidogo wakauita uwanja wao kuwa wa Kambarage (siyo Nyerere).
Huu ndio ukweli.
 
Watanzania hasa wana siasa uchwara wa ccm wanapenda sana vitu viitwe kwa majina yao wakiwa hai japo hawana sifa hiyo, hawana chochote walichoifanyia hii nchi lakini wanalazimisha barabara ziitwe kwa majina yao.

Inatakiwa mtu uwafanyie wananchi wako mema ili ufae hiyo sifa ukishatoka duniani, sio mtu labda umeua watu wako na bado unataka barabara liitwe kwa jina lako ikija serikali nyingine jina lako linafutwa kabisa.
 
Back
Top Bottom