Rukwa: Ndege yanusurika kugonga Bajaji iliyokuwa ikikatisha uwanja wa ndege

Ghazwat

JF-Expert Member
Oct 4, 2015
23,718
66,262
86d23cffe76af0cea904b0a8b0f56c50.jpg
Katika hali isiyokuwa ya kawaida watu watatu wamenusurika kugongwa na ndege walipokuwa wakisafiri kwa bajaji iliyokuwa ikikatisha uwanja wa ndege wa Sumbawanga mkoani Rukwa ambapo rubani wa ndege hiyo alifanikiwa kuepusha ajali kwa kuipaisha ndege juu upepo wa ndege ukasababisha bajaji hiyo kupinduka na kujeruhi abiria waliokuwemo.

Kukosekana kwa uzio imara katika uwanja wa ndege wa Sumbawanga kunaweza kusababisha ajali mbaya kutokana na mazoea ya kukatisha katikati ya uwanja wa ndege kwa watembea kwa miguu, baiskeli, pikipiki, magari na hata mabasi madogo ya wanafunzi na abiria kama ambavyo mwishoni mwa wiki imetokea sintofahamu baada ya ndege moja kunusurika kupata ajali ya kugonga Bajaji iliyokuwa ikikatisha uwanja wa ndege hiyo ikitaka kutua.

Mashuhuda wa tukio hilo wamesema ilikuwa majira ya saa nne na dakika ishirini asubuhi ndege ilipokuwa ikitaka kutua uwanjani hapo, rubani alibaini kuwepo kwa bajaji na kupaisha ndege lakini upepo mkali uliweza kupindua bajaji ambayo ilisamasoti mara kadhaa na kuwajeruhi waliokuwa ndani.

Chanzo: Channelten
 
Mashuhuda wa tukio hilo wamesema ilikuwa majira ya saa nne na dakika ishirini asubuhi ndege ilipokuwa ikitaka kutua uwanjani hapo, rubani alibaini kuwepo kwa bajaji na kupaisha ndege lakini upepo mkali uliweza kupindua bajaji ambayo ilisamasoti mara kadhaa na kuwajeruhi waliokuwa ndani.
 
Katika hali isiyokuwa ya kawaida watu watatu wamenusurika kugongwa na ndege walipokuwa wakisafiri kwa bajaji iliyokuwa ikikatisha uwanja wa ndege wa Sumbawanga mkoani Rukwa ambapo rubani wa ndege hiyo alifanikiwa kuepusha ajali kwa kuipaisha ndege juu upepo wa ndege ukasababisha bajaji hiyo kupinduka na kujeruhi abiria waliokuwemo.

Kukosekana kwa uzio imara katika uwanja wa ndege wa Sumbawanga kunaweza kusababisha ajali mbaya kutokana na mazoea ya kukatisha katikati ya uwanja wa ndege kwa watembea kwa miguu, baiskeli, pikipiki, magari na hata mabasi madogo ya wanafunzi na abiria kama ambavyo mwishoni mwa wiki imetokea sintofahamu baada ya ndege moja kunusurika kupata ajali ya kugonga Bajaji iliyokuwa ikikatisha uwanja wa ndege hiyo ikitaka kutua.

Mashuhuda wa tukio hilo wamesema ilikuwa majira ya saa nne na dakika ishirini asubuhi ndege ilipokuwa ikitaka kutua uwanjani hapo, rubani alibaini kuwepo kwa bajaji na kupaisha ndege lakini upepo mkali uliweza kupindua bajaji ambayo ilisamasoti mara kadhaa na kuwajeruhi waliokuwa ndani.

Chanzo: Channelten
Picha Mkuu
 
Back
Top Bottom