Rubani auchapa usingizi ndani ya ndege

Rubani auchapa usingizi ndani ya ndege

2efdd2acdaa5d3c2448b4c5c6f296e35.jpg
😀😀😀
 
Huu usafiri natumia kwa sababu tu nakuwa sina namna, ila mimi sijawahi kabisa kuizoea ndege, ningekuwa mimi humo nafikiri hali yangu ingekuwa mbaya mno

Na ndio maana kabla ya kuruka tahadhari hutolewa ki utu uzima. Ila ni usafiri salama kuliko yote.
 
Hakuna ndege inayobeba abiria ikiwa na rubani mwanafunzi.Huyo ni co-pilot ambaye nayeye ni rubani certified sema ana masaa machache..

Hawa wapakistan nao ni ushamba unawasumbua ndege ikishafika cruising altitude wanaweka autopilot kila rubani na kitanda chake wanadozi
 
Kuna kesi moja ilikua ndege ya warusi ilikua inaenda Japan i think basi kuna pilot alikua likizo akawa anasafili na watoto wake sasa ile kupenda sifa akawapeleka watoto wake kwenye cockpit akawaomba wale ma pilot wenzie coz walikua wanafahamiana kuwa mwanangu anataka ku experience ku endesha ndege jamaa wakakubali da wakaweka auto pilot ngoma iko hewani na abiria wa kutosha kama 200 hivi dogo si akauchezesha usukani dege likayumba akauludisha ikakaa sawa wote wakafurai badae wazee wakawa wanapiga story wamejisahau dogo akauchezesha usukani akapiliza limit ya ile auto pilot ku handle ndege ikageuka kilichowapata mungu anajua hakutoka hata mtu mmoja tangu kipindi hicho ikapitishwa sheria watoto hawaluhusiwi kwenye cockpit so nilichoka kusema sometimes auto pilot huwa zina fail
hiyo ni ajali ya ndege ya Aeroflot Flight 593 ikitokea moscow kwenda hong kong ambapo rubani aliwaalika watoto wake waje cockpit ili waone jinsi ndege inavyoendeshwa. both first officer na mwenzake walikuwa wazembe kuruhusu hali hiyo kutokea. unfortunately wote waliangamia.

 
Kwa ufupi,

Ndege hiyo ilikuwa na abiria zaidi ya 305 ikisafiri kutoka mji mkuu wa Pakistan, Islamabad kuelekea London, Uingereza.

Rubani auchapa usingizi ndani ya ndege, azua tafrani
Islamabad, Pakistan. Abiria waliokuwa wakisafiri na ndege ya Shirika la Ndege la Pakistan (Pia) waliingiwa taharuki baada ya kugundua kuwa rubani wa ndege hiyo alikuwa ametoka katika chumba chake na kuelekea sehemu nyingine kulala.
Ndege hiyo ilikuwa na abiria zaidi ya 305 ikisafiri kutoka mji mkuu wa Pakistan, Islamabad kuelekea London, Uingereza.

Rubani huyo, Amir Akhtar Hashmi anadaiwa kumwacha rubani mwanafunzi katika chumba cha kuongezea ndege na kwenda katika moja ya sehemu za abiria ambako alijifunika blanketi na kulala.

Tukio hilo lilitokea muda mchache baada ya ndege hiyo kuanza kuruka.

SOURCE:MWANANCHI
Islamabad to london ni parefu sana so ni obvious aliiweka ndege ktk auto pilot na huyu mwanafunzi ni mwanafunzi kwa jina tu ila atakuwa vizuri kabisa!
 
Nauliza hivi hizi bajaji/pangaboi(bomberdia) zetu zina hiyo auto-piloting?
 
Habari nyengine zinavotiwa chumvi! Rubai mwanafunzi kaachiwa arushe ndege? Tangu lini mwanafunzi akaachiwa arushe ndege yenye abiria ndani? Hao abiria walijuaje kama huyo mwanafunzi? Halafu pilot kulala ni kawaida mbona huku akimuachia first officer aenselee na kazi. Hili gazeti limekosa habari nini?
 
Hyo ya dege kubwa hvo kuwa na marubani wawil tu nalo geni masikioni mwangu.. hata ikitokea ameenda chooni lazima abaki mtu wa kusoma alert system, na inategemea huyu mwanafunzi ni wa level gan, Kama ni junior au sinior trainee
 
Huu usafiri natumia kwa sababu tu nakuwa sina namna, ila mimi sijawahi kabisa kuizoea ndege, ningekuwa mimi humo nafikiri hali yangu ingekuwa mbaya mno
Aiseee!! Kumbe tuko wengi

Nkipandaga huo usafir na meli
Hua naanza kutubu thambi zang
Mapemaaa
 
Back
Top Bottom