RPC Liberatus Sabas na Kashfa ya Leopard Tours

RPC Liberatus Sabas na Kashfa ya Leopard Tours

Kuna harufu isiyo sahihi waleta hoja naona wanakata kulitumia Jukwaa kwa vita ya kimasilahi hii ni thread sijui ya pili kuhusu Leopard Tours na mahusiano na Watumishi wa Umma.
Hahaha..kwa maslahi yapi watakayopata ikiwa hao wanaosemwa watarekebishwa?.
 
Kwa jeshi letu la polisi, maneno yenu ni sawa na kulima kwenye Lami.Uozo upo Tanzania nzima.
 
Ninaona umejitoa mhanga kupost habari za wakubwa, shauri yako yasijekukuta ya mawazo
 
Graduate anayeanza kazi basic salary ni 860,000.

Huyu hata cheo kimoja hana, jinyonge tu.
 
Last edited by a moderator:
Mdau hili linajulikana miaka mingi lakini hakuna hata hatua yoyote inayochukuliwa. Nchi hii bado tuna safari ndefu ya kuondoa utawala mbovu, sijui kama JPM ataweza.
 
Usalama wa Taifa, wafanye kazi yao wataupata...!
Kwani usalama wa taifa hawapo kwenye malipo ya haya majizi? CCM nzima iko mifukoni mwa wafanya biashara. Muombeeni Magufuli maana hii ni vita yake binafsi
 
Kuna askari Pale Maeneo ya Raskazonii Kama unaelekea Ngaramtoni, kwa kweli wamekua keroo..
Sijui ni gari langu tuu(kirikuu) au ni kwa magari yote..???Nikupigwa mkono nakutafutiwa kosa..
Ukitoka hapo wapo Technico/TripleA...

Embu tokeni nje ya mji huko ndiko makosa kibao mtayapata..cc traffic police Arusha
 
Hahaha..kwa maslahi yapi watakayopata ikiwa hao wanaosemwa watarekebishwa?.

Mara nyingi biashara au maisha kwa ujumla wake si kila mmoja anapenda ufanikiwe -marekebisho mengine ndiyo kama zile operation za wale ndugu walikumbwa na balaa la Mwaka-unakumbuka tukio la mgonjwa wa Kichwa kupasuliwa mguu na mguu kupasuliwa kichwa?
 
Swala la kuwa na gari sio ishu maana wengine wasomi mishahara yao iko juu na kuna mikopo, tatizo labda ni hiyo rushwa.
Hatuzungumzii usomi wala nini tunataka kujua askari polisi wa kawaida hana miaka mitano kazini, ana nyumba self, ana nyumba za wapangaji, ana magari ya abiria tunaita vifodi ana gari yake ya kuembelea je mshahara wake na mikopo vinatosheleza kuwa na vitu vyote hivi??? Kuna watumishi wanafanya kazi miaka 40 wanakuja kujenga kibanda na hela za mafao, tuwe serious kwenye kuchangia hii mada.
 
Kuna askari Pale Maeneo ya Raskazonii Kama unaelekea Ngaramtoni, kwa kweli wamekua keroo..
Sijui ni gari langu tuu(kirikuu) au ni kwa magari yote..???Nikupigwa mkono nakutafutiwa kosa..
Ukitoka hapo wapo Technico/TripleA...

Embu tokeni nje ya mji huko ndiko makosa kibao mtayapata..cc traffic police Arusha
Ati wana pita speed limit isizidi 50km/h hakuna kibao cha speed limit RTO yote hayo anajua ila kwa vile ni kimaslahi hakemei hii hali Jamani tutafikaaa????
 
pamoja na yote hayo hivi nyinyi watu wa arusha kila mara mnaugomvi na polisi? simtetei kamanda lakini
ukiona hivyo watu wa Arusha ni waelewa wa mambo na wasema kweli ndio maana yote hayo yanafahamika mapema sio kama mikoa mingine mpaka mambo yanaharibika kabisa
 
Ati wana pita speed limit isizidi 50km/h hakuna kibao cha speed limit RTO yote hayo anajua ila kwa vile ni kimaslahi hakemei hii hali Jamani tutafikaaa????
kwanza haya mambo ya speed llimit yanatakiwa yaangaliwe upya maana kwa wakati huo magari mengi yalikuwa na speed mwisho 180 lakini sasa hivi kuna magari mpaka speed ya 300 kwa saa
 
kwanza haya mambo ya speed llimit yanatakiwa yaangaliwe upya maana kwa wakati huo magari mengi yalikuwa na speed mwisho 180 lakini sasa hivi kuna magari mpaka speed ya 300 kwa saa
Brother silalamikii mwendo najiuliza kwanini watege watu sehemu ambazo hakuna onyo la kibao?? Kwamba wanataka tuendeshe magari kwa hisia na sio kwa taratibu za barabara?? Pale Madiira Tengeru utakuta wako pia na touch ya mwendo wanataka speed 50 lakini hakuna kibao wala makazi ya watu, tunakwenda wapi na hawa trafic wa Arusha?? Pale kinachotakiwa ni hakuna kupita gari jingine kwa sababu ya daraja na sio mwendo kasi.
Naomba sana RTO Arusha na Ocs wake wote wachunguzwe hizi tochi ziko kwa manufaa ya nani??
Lah ni hivyo basi waongee na Tanroads waweke vibao ili tufuate sheria.
 
Swala la kuwa na gari sio ishu maana wengine wasomi mishahara yao iko juu na kuna mikopo, tatizo labda ni hiyo rushwa.

sawa ila jua kuwa kuna police pale anamagari kama utitili uliza mafundi Garage watawaambieni magari yao mjue sasa na ujiulize yeye mshahara wake ni kiasi gani biashara mtu ana gari 15 khaaa alafu bado yuko Jeshi la police anataka nini sasa au hapo ndipo anajificha kwenye kichaka na maovu yao?


My Take;
Ilikuwa zamu ya TPA TRA TAKUKURU NA SERIKALINI sasa inakuja TISS na POLICE ndiko kuna wala rushwa wa kulazimishia
 
Na sasa barabara ya kwenda Tengeru - USA inajengwa sasa watahamia vichochoroni mara wako Njia ya themi hill sikummoja nikawakuta njiro kwa msola hahahahaha

kazi nzuri hiii hulali njaaaa kabisaaaa unachukuwa pesa za mtu kwanguvu tena bila uwoga. Fani zao tizama kitabu ni cha mwaka 2011 unatozewa fini siku niliona kwa mtu nikamwambia usilipe kitabu cha mwaka gani hata ukienda mahakamani watakushinda records zao za miaka 4 nyuma unakutoza fani mwaka 2016
hii ni kali ya mwaka.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom