RPC Ahmed Msangi awaagiza polisi waue jambazi yeyote kabla hawajaua raia

maramia

JF-Expert Member
Jul 17, 2015
2,030
1,345
Kamanda wa polisi wa mkoa wa Mwanza Ahmed Msangi amewapa amri polisi wa mkoa wa Mwanza kumuua mtu yeyote atakayetajwa au kudaiwa kwamba ni jambazi.

Kama Msangi ana uwezo na mamlaka haya kwa nini asitoe amri hii wauawe wote wanaopatikana na hatia hii pale pale mahakama kuu ya Mwanza kabla hawajatoka nje kuliko hawa ambao hata hawajafikishwa mahakamani?

Kama polisi wanaweza kuua kwa nini kila siku wanatuomba sisi raia tusijichukulie hatua mikononi? Heri nasi tuendelee kuua maana ndio tunaowakamata wezi live.

Hivi huyu Ahmed Msangi siyo yule aliyetajwa tajwa kuhusika kwenye sakata la kumtesa Dk Ulimboka wakati wa mgomo wa madaktari MNH?


======================

Jeshi la Polisi limeamriwa kuua mtu yeyote ataedaiwa kuwa jambazi.Ruhusa hiyo imetolewa leo na Ahmed Msangi, kamanda mpya wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza ambaye pia ni Kamishna Msaidizi Mwandamizi (SACP).

Msangi ambaye amehamia mkoani humo akitokea Mbeya, ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na maofisa usalama na polisi wa vyeo mbalimbali baada ya kukabidhiwa rasmi ofisi hiyo na SACP, Justus Kamugisha.

Msangi ametoa kauli hio siku chache baada ya John Mongella, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kusema kwamba, Kamugisha alikuwa mzigo kwenye jiji hilo kutokana na kushindwa kukabiliana na ujambazi.

Katika kipindi cha miezi miwili ya Machi na Aprili mwaka huu, matukio saba ya uhalifu wa kutumia silaha za moto umeripotiwa na katika matukio hayo watu sita walipoteza maisha.

Msangi amesema kuwa, anawashangaa polisi wanaoshindwa kutumia silaha zao kuwaua watu wanaodaiwa kuwa majambazi na kusababisha vitendo vya uhalifu kuendelea kushamiri jijini humo.

“Tumieni na nyie bunduki zenu kuua watu ambao ni majambazi, haiwezekana uwe na silaha halafu unaacha kuchukua hatua za haraka za watu ambao wanasababisha mauaji na uporaji wa mara za raia,” amesema Msangi.

Msangi amesema, Jiji la Mwanza miezi michache iliyopita limetikiswa na matukio ya unyang’anyi wa kutumia silaha yanayoambatana na mauaji ya raia, kujeruhi na uporaji wa mali zao.

Amesema kuwa, polisi wanapaswa kufanya kazi zao kwa kujiamini na kuacha kufanya kazi kwa mazoea.

Kamanda Kamugisha akikabidhi ofisi hiyo aliwahimiza polisi kufanya kazi kwa weledi na kwa kuzingatia maadili ya jeshi hilo bila kumuonea mtu yeyote yule.


Chanzo: Mwanahalisionline
 
Majambazi ni kweli wanarudisha nyuma. Ila kuua tu eti kwa kutajwa au kuhusiwa! Hii hapana. Maana inawezekana mtu akamtaja mbaya wake ili tu kumkomoa auawe
 
Alikua hana adabu kabla hajaenda Mbeya...maana yeye anasifika kuwa ndiye alikua Killing machine ndani ya Jeshi la Polisi na sifa hiyo ndiyo ilimbeba na kumfanya maarufu ikiwemo kupanda vyeo.
Alipofika Mbeya akaongoza kiungwana sana, sasa amepekekwa Mwanza naona anataka kurudia tabia zake za zamani ambazo zilishaanza kujipatia wafuasi kama akina Sabasita.
 
Kamanda wa polisi wa mkoa wa Mwanza Ahmed Msangi amewapa amri polisi wa mkoa wa Mwanza kumuua mtu yeyote atakayetajwa au kudaiwa kwamba ni jambazi.

Kama Msangi ana uwezo na mamlaka haya kwa nini asitoe amri hii wauawe wote wanaopatikana na hatia hii pale pale mahakama kuu ya Mwanza kabla hawajatoka nje kuliko hawa ambao hata hawajafikishwa mahakamani?

Kama polisi wanaweza kuua kwa nini kila siku wanatuomba sisi raia tusijichukulie hatua mikononi? Heri nasi tuendelee kuua maana ndio tunaowakamata wezi live.

Chanzo: Radio Ukombozi Fm.

Kama Taarifa hii ni ya kweli basi huyo RPC akae chini atafakari. Yawezekana akili yake imeruka na hayuko sawa. Kama siyo basi anatumia ule mumea ambayo huko kwetu ni mboga. Nadhani kwa sasa Jeshi letu lina wasomi wengi ambao wanaweza kuchallenge orders kama hizi kabla ya kuzitekeleza. Japo wapo ambao kila amri inayotolewa na Mkubwa wao ni kutekeleza tu bila kujali athari zinazoweza kujitokeza. Kutoa Amri ya Kuuwa kila anayehisiwa na kutajwa kuwa ni jambazi kunaweza kuleta ufa mkubwa kati ya jeshi la polisi na wananchi wa Kawaida hivyo huyu anawachonganisha polisi wa kawaida na wananchi. Kitendo cha kutoa amri hiyo ni kukiri kuwa JESHI LA POLISI limeshindwa kazi. Kamanda Msangi Yawezekana umekaa jeshini muda mrefu bila kupitia tena sheria ya uanzishwaji wa jeshi la polisi na Madhumuni yake.
Kama ni kweli umetoa AMRI hiyo basi unatengeneza ufa mkubwa ambao hutoweza kuuziba. Mwishowe utaitwa jipu na utatumbuliwa.
 
Ahmed Msangi hana shule si kosa lake ni mfumo mbovu ndio umemfikisha hapo alipo.
 
Tulionywa sana na wahenga kutosahau akili wakati tukitumia mioyo kunena yaliyotujaza kifuani...ni vyema sana viongozi na watawala kwa ujumla wao wakahariri matamko wanayoyatoa kabla ya kuyatamka ili kuepusha migogoro na sintofahamu kwenye jamii kutokana na matamko husika!
 
Amesema hivi "majambazi wakikataa kujisalimisha na kuanza kuwafyatulia risasi polisi, basi nao wawajibu hata wakiwaua." Hapa naona wewe umeleta habari kiupotoshaji, sijui ni kwa makusudi au una lengo gani. Au una ushirika na hawa majambazi?

now u are talking


we mleta uzi wacha kuleta habari nusunusu kuleta hisia tofauti na maana halisi ya alichokisema kamanda ... ninyi ndo mnafanya jf iwe kama kijiwe samli...... ........idharauliwe ionekane kama instagram



NONESENSE
 
Kamanda wa polisi wa mkoa wa Mwanza Ahmed Msangi amewapa amri polisi wa mkoa wa Mwanza kumuua mtu yeyote atakayetajwa au kudaiwa kwamba ni jambazi.

Kama Msangi ana uwezo na mamlaka haya kwa nini asitoe amri hii wauawe wote wanaopatikana na hatia hii pale pale mahakama kuu ya Mwanza kabla hawajatoka nje kuliko hawa ambao hata hawajafikishwa mahakamani?

Kama polisi wanaweza kuua kwa nini kila siku wanatuomba sisi raia tusijichukulie hatua mikononi? Heri nasi tuendelee kuua maana ndio tunaowakamata wezi live.

Hivi huyu Ahmed Msangi siyo yule aliyetajwa tajwa kuhusika kwenye sakata la kumtesa Dk Ulimboka wakati wa mgomo wa madaktari MNH?

Chanzo: Radio Ukombozi Fm.
Wewe unaepinga utakuwa na sifa mbili kuu
1) Mwana UKAWA
2) JAMBAZI
 
Alikua hana adabu kabla hajaenda Mbeya...maana yeye anasifika kuwa ndiye alikua Killing machine ndani ya Jeshi la Polisi na sifa hiyo ndiyo ilimbeba na kumfanya maarufu ikiwemo kupanda vyeo.
Alipofika Mbeya akaongoza kiungwana sana, sasa amepekekwa Mwanza naona anataka kurudia tabia zake za zamani ambazo zilishaanza kujipatia wafuasi kama akina Sabasita.
Mkuu kumbe unamfahamu sabasita, huyu jamaa ni muuaji sana
 
Amesema hivi "majambazi wakikataa kujisalimisha na kuanza kuwafyatulia risasi polisi, basi nao wawajibu hata wakiwaua." Hapa naona wewe umeleta habari kiupotoshaji, sijui ni kwa makusudi au una lengo gani. Au una ushirika na hawa majambazi?
Mkuu, wala usihangaike. wengine wapo humu Jf ila ni majambazi ya kutupwa.
 
Naiona The Hague haiko mbali kama ni kweli, hakuna aliye juu ya sheria afanye kazi zake kwa weledi.
 
Tulionywa sana na wahenga kutosahau akili wakati tukitumia mioyo kunena yaliyotujaza kifuani...ni vyema sana viongozi na watawala kwa ujumla wao wakahariri matamko wanayoyatoa kabla ya kuyatamka ili kuepusha migogoro na sintofahamu kwenye jamii kutokana na matamko husika!
Majambazi yamekuwa yakisababisha mauaji ya watu wengi wasio na hatia. wengine wamebaki vilema. sasa kama wao wanaua, kwa nini wasiuawe? sheria ni msumeno
 
Amesema hivi "majambazi wakikataa kujisalimisha na kuanza kuwafyatulia risasi polisi, basi nao wawajibu hata wakiwaua." Hapa naona wewe umeleta habari kiupotoshaji, sijui ni kwa makusudi au una lengo gani. Au una ushirika na hawa majambazi?
Kamanda hakuyasema hayo, hayo unamsemea wewe.
 
Kamanda wa polisi wa mkoa wa Mwanza Ahmed Msangi amewapa amri polisi wa mkoa wa Mwanza kumuua mtu yeyote atakayetajwa au kudaiwa kwamba ni jambazi.

Kama Msangi ana uwezo na mamlaka haya kwa nini asitoe amri hii wauawe wote wanaopatikana na hatia hii pale pale mahakama kuu ya Mwanza kabla hawajatoka nje kuliko hawa ambao hata hawajafikishwa mahakamani?

Kama polisi wanaweza kuua kwa nini kila siku wanatuomba sisi raia tusijichukulie hatua mikononi? Heri nasi tuendelee kuua maana ndio tunaowakamata wezi live.

Hivi huyu Ahmed Msangi siyo yule aliyetajwa tajwa kuhusika kwenye sakata la kumtesa Dk Ulimboka wakati wa mgomo wa madaktari MNH?

Chanzo: Radio Ukombozi Fm.
SAHIHISHO: Mkuu hii taarifa niliisikia live alipokuwa anazungumza na si kama unavyoiripoti[ hapo kwenye buluu] alichosema ni kuwa kwa kuwa majambazi yanaua raia wasio na hatia kwa kuwapiga risasi basi jeshi la polisi liwaue majambazi vivyo hivyo kwa kuwapiga risasi ila wawe makini wasidhuru raia. Hajasema mtu atakaetajwa kuwa ni jambazi auawe, upotoshaji wa taarifa ni hatari kwa maslahi ya nchi
 
Naiona The Hague haiko mbali kama ni kweli, hakuna aliye juu ya sheria afanye kazi zake kwa weledi.
Sidhani kama kuna kiongozi anapelekwa The Hague kwa kuua majambazi. Kagame kanyonga Majambazi wengi sana na ndo maana kwa sasa Rwanda hakuna ujambazi
 
Back
Top Bottom