Ben Zen Tarot
JF-Expert Member
- Dec 13, 2014
- 3,910
- 6,706
MAHITAJI
1.Viazi mbatata kilo moja
2.Nyama ya ng'ombe kilo moja
3.Nyanya maji kubwa nane
4.Tomato paste vijiko viwili vya chakula
5.Vitunguu maji viwili
6.Karoti kubwa moja
7.Kitunguu saum kilichosagwa kijiko kimoja cha chakula
8.Binzari nyembamba ya unga nusu kijiko cha chai
9.Tangawizi iliyosagwa kijiko kimoja cha chakula
10.Pilipilimanga ya unga nusu kijiko cha chai
11.Paprika kijiko kimoja cha chai
12.Pilipili mbichi iliyosagwa kiasi
13.Mchuzi mix au garam masala kijiko kimoja cha chakula
14.Limao moja
15.Mafuta ya kupikia
16.Chumvi
MAPISHI
1.Katakata nyama katika vipande tia tangawizi na chumvi kamulia kipande cha limao changanya, ichemshe hadi iive bakisha supu kiasi
2.Saga nyanya kupata rojo
3.Kataka vitunguu maji na karoti katika vipande vipande
4.Tia mafuta katika sufuria, acha yapate moto tia vitunguu maji koroga hadi vibadirike rangi viwe kama vya kijani mpauko, kisha tia vitunguu saum koroga kidogo hadi usikie harufu, visiungue, tia binzari ya nyembamba koroga vyema.
5.Tia rojo la nyanya na chumvi kiasi kisha koroga na funika, acha hadi nyanya ziive vizuri
6.Tia humo nyama,viazi na vipande vya karoti na tomato paste koroga vyema
7.Funika acha vichemke kiasi, funua nyunyuzia mchuzi mix au garam masala, unga wa pilipilimanga, paprika,pilipili mbichi,kamulia kipande cha limao kilichobaki,tia supu iliyobaki kidogo kisha koroga, punguza moto acha chakula kichemke taratibu hadi maji yapungue na ibakie rosti zito.
8.Epua chakula kipo tayari
Andaa juisi au soda baridii na chakula hiki kisha jenga mwili
1.Viazi mbatata kilo moja
2.Nyama ya ng'ombe kilo moja
3.Nyanya maji kubwa nane
4.Tomato paste vijiko viwili vya chakula
5.Vitunguu maji viwili
6.Karoti kubwa moja
7.Kitunguu saum kilichosagwa kijiko kimoja cha chakula
8.Binzari nyembamba ya unga nusu kijiko cha chai
9.Tangawizi iliyosagwa kijiko kimoja cha chakula
10.Pilipilimanga ya unga nusu kijiko cha chai
11.Paprika kijiko kimoja cha chai
12.Pilipili mbichi iliyosagwa kiasi
13.Mchuzi mix au garam masala kijiko kimoja cha chakula
14.Limao moja
15.Mafuta ya kupikia
16.Chumvi
MAPISHI
1.Katakata nyama katika vipande tia tangawizi na chumvi kamulia kipande cha limao changanya, ichemshe hadi iive bakisha supu kiasi
2.Saga nyanya kupata rojo
3.Kataka vitunguu maji na karoti katika vipande vipande
4.Tia mafuta katika sufuria, acha yapate moto tia vitunguu maji koroga hadi vibadirike rangi viwe kama vya kijani mpauko, kisha tia vitunguu saum koroga kidogo hadi usikie harufu, visiungue, tia binzari ya nyembamba koroga vyema.
5.Tia rojo la nyanya na chumvi kiasi kisha koroga na funika, acha hadi nyanya ziive vizuri
6.Tia humo nyama,viazi na vipande vya karoti na tomato paste koroga vyema
7.Funika acha vichemke kiasi, funua nyunyuzia mchuzi mix au garam masala, unga wa pilipilimanga, paprika,pilipili mbichi,kamulia kipande cha limao kilichobaki,tia supu iliyobaki kidogo kisha koroga, punguza moto acha chakula kichemke taratibu hadi maji yapungue na ibakie rosti zito.
8.Epua chakula kipo tayari
Andaa juisi au soda baridii na chakula hiki kisha jenga mwili