Umejuaje nimesoma chuo kikuu, na sekondari? Na hutakiwi kuamini nitakachokwambia. Nenda kafanye utafiti kuhusu mimi. Ukishindwa njoo tutafute muda muafaka kufanya usaili na mimi, na mada ya siku hiyo itakuwa mahsusi, wasifu wangu mimi Rostam Aziz, kama unataka kuandika biography. Swali lingine tafadhali.
Umiliki wa makampuni ya biashara, ukitakata kuongelea umiliki wa makampuni, unaweza kuanzia yanarekodiwa, BRELA. Huo ndio uandishi wa kichunguzi. Ukishindwa, again, nitakuwa na zaidi ya furaha kukaa na wewe unifanyie usaili kuongelea biashara zangu na yatokanayo. Nikupe upande wangu wa hadithi, nitakuwa na zaidi ya furaha kufanya hilo. Mwingine?
Gen. Adawi ana hisa ngapi wapi ilibidi umbane yeye siku hiyo hiyo akwambie ana ngapi wapi alipokiri kunifahamu.
Isitoshe, ndugu mwandishi, umiliki wa Dowans na yote yatokanayo yalichunguzwa na Bunge, na Tukukuru, yameongelewa magazetini, na mitandaoni na mabarazani. Unatakiwa ndugu mwandishi, kuwa na msingi wa yaliyosemwa na wachunguzi binafsi kwanza, kabla ya kuja kuniuliza mimi. Huanzii kwangu. Swali lingine?
Kuhusu ya Dowans, nitakachokisema nimekisema.
Ndugu mwandishi, inabidi uzatiti hisia yako, substantiate the presumption, the premise, of your question, kwamba nilimsaidia, halafu ndio uulize nilimsaidia kiasa gani. Vinginevyo swali lako ni la kufikirika, hypothetical. Si busara kujibu ya kufikirika, hypotheticals. Swali linatofuata tafadhali.
Tuko kwenye press conference ya shutuma za Mzee Mengi, wewe unaongelea nitawaambia nini wananchi kuhusu kampeni za Kikwete. Watu wa Igunga wamesha move forward kutoka katika campaign mode na sasa wanatathmini uongozi, na sio kampeni, uongozi wa Kikwete. Ninapima the pulse of the voter, hicho sio kilio cha watu wa Igunga. Nina ulukuki, a laundry list, ya kero za wa Igunga. Kampeni za 2005 halimo. Next.
Ndugu mwandishi umesema "mfuko binafsi"? Ya mfuko binafsi yanawahusu watu binafsi, kutokana na watu binafsi, kwa ajili ya watu binafsi. Maongezi ya binafsi tutafutane kwa kahawa, kwa faragha. Umesema mwenyewe "mfuko binafsi," huulizi ya binafsi, ndugu mwandishi, huulizi ya binafsi kwenye mdahalo wa umma. Mwingine mwenye swali tafadhali.
Kuhusu ya kampeni ya Kikwete, nitakachokisema nimekisema.
Sina ruhusa ya Yusuph Manji au yeyote yule niliye na mahusiano nae kuongelea mahusiano yetu hadharani. Baadhi ya mahusiana ya kibiashara huwa ni trade secrets anyway. Swali lingine.
Ndio wafikishwe, ndugu mwandishi, naamini siku zote kwamba anaeshukiwa kuvunja sheria anatakiwa apelekwe mbele ya vyombo vya sheria. Ahsanteni sana.
Ndugu wananchi, sasa tunawarudisha studio zetu kujiunga na Professor Jay akisema:
Piga makofi, Piga Makofi, Piga Makofi tafadhali...
Piga makofi, Piga Makofi, Piga Makofi tafadhali...