Rostam kukutana na waandishi wa habari

Status
Not open for further replies.
Mkutano huu wa waandishi wa habari inabidi uwe ni juu ya Rostam. Asiachwe na ajenda yake bali waandishi ndio waamue muelekeo wa ajenda ya mazungumzo. Baadhi tu ya maswali ambayo itakuwa vizuri kupata majibu yake ni haya:

Mhe. Rostam:

a. Ulizaliwa wapi, mwaka gani, ulisoma shule ya msingi wapi, sekondari wapi na Chuo Kikuu wapi na mwaka gani?

b. Una umiliki wa makampuni mangapi ya biashara (aidha ukiwa mmiliki au mwenye hisa)?

c. Mmiliki wa Dowans Gen. Aladawi amekiri kukufahamu na kuwa mna urafiki wa karibu; je una hisa yoyote kwenye kampuni yake au yeye ana hisa zozote kwenye mojawapo ya makampuni yako?

d. Ni kwa kiasi gani ulimsaidia Gen. Al-Adawi kuweza kuanzisha kampuni ya Dowans Tanzania Ltd? Unamfahamu mmiliki wa Dowans Holdings SA ya Costa Rica?

e. Ni kwa kiasi gani ulimsaidia Salva Rweyemamu mwandishi wa mojawapo ya vyombo vyako vya habari kupata kazi Ikulu?

f. Ukiwa Meneja wa Kampuni wa Kikwete bila ya shaka ulisimamia kiasi kikubwa cha fedha na mgawanyo wa matumizi yake, (a) je unaweza kuwaambia wananchi ni kiasi gani kilitumika katika kampeni ya Kikwete (b)Je fedha za kampeni ya Kikwete zilitoka wapi?

g. Ni wabunge wangapi ambao umewasaidia kifedha katika kampeni kutoka katika mfuko wako binafsi katika uchaguzi wa 2005, unaweza kuwataja baadhi yao?

h. Kuna kiasi chochote cha fedha ambacho kampeni ya Kikwete ilipokea aidha kutoka Iran au nchi nyingine yoyote ya nje au wafanyabiashara wa nje akiwemo Gen. Al-Adawi?

i. Je una uhusiano wowote wa kibiashara na Yusuph Manji na ni uhusiano upi?

j. Je, msimamo wako kuhusu wizi mkubwa kabisa wa fedha za Watanzania kutoka akaunti ya EPA ni upi na unasema nini kuhusu kutokujulikana kwa watu waliochota fedha za Kagoda na kuzirudisha taslimu. Je wafikishwe mahakamani hata baada ya kurudisha?
 
"Hiyo ni strategy yake tu ambayo kaanza toka juzi nadhani anafikiri watanzania ni wajinga unaweza ukawaibia na ukawanunua baadhi ukawatumia kuwadanganya wengine,kawalipia wenyeviti wa UVCCM ticket za kuja Dar kusoma waraka alioandikiwa na Lowasa,by the way baadhi wamekusudia kusema ukweli na kulaumu wenzao kuwasukuma kufanya wasiyo yajua,kwa mfano mmoja wa wenyeviti niliyeongea nae kaniambia walilipwa shs laki 3 kila mmoja na wamelipiwa ticket na gharama za kuishi Dar na wakapelekwa Maelezo kusoma waraka ambao hawajui nani aliyeuandiaka"

*******************************

Ndanda to Lomwe:

Nami nimeyasikia hayo unayosema kuhusu UVCCM Tabora walionunuliwa na kulipwa nauli ya ndege (mmoja alitolewa Mwanza alikokuwapo). Inasemekana halmashauri Kuu ya UVCCM mkoani Tabora hawakutoa baraka zao kwa hilo na wanakuja na taarifa kali ya kulani -- ingawa RA anaweza kuwawahi wasifanye hivyo kwa kuwamwagia mapesa.

Mimi nadhani kwa mara ya kwanza RA ataaibika kesho!!! Ngojeni tu.
 
Mkutano huu wa waandishi wa habari inabidi uwe ni juu ya Rostam. Asiachwe na ajenda yake bali waandishi ndio waamue muelekeo wa ajenda ya mazungumzo. Baadhi tu ya maswali ambayo itakuwa vizuri kupata majibu yake ni haya:

Mhe. Rostam:

a. Ulizaliwa wapi, mwaka gani, ulisoma shule ya msingi wapi, sekondari wapi na Chuo Kikuu wapi na mwaka gani?

b. Una umiliki wa makampuni mangapi ya biashara (aidha ukiwa mmiliki au mwenye hisa)?

c. Mmiliki wa Dowans Gen. Aladawi amekiri kukufahamu na kuwa mna urafiki wa karibu; je una hisa yoyote kwenye kampuni yake au yeye ana hisa zozote kwenye mojawapo ya makampuni yako?

d. Ni kwa kiasi gani ulimsaidia Gen. Al-Adawi kuweza kuanzisha kampuni ya Dowans Tanzania Ltd? Unamfahamu mmiliki wa Dowans Holdings SA ya Costa Rica?

e. Ni kwa kiasi gani ulimsaidia Salva Rweyemamu mwandishi wa mojawapo ya vyombo vyako vya habari kupata kazi Ikulu?

f. Ukiwa Meneja wa Kampuni wa Kikwete bila ya shaka ulisimamia kiasi kikubwa cha fedha na mgawanyo wa matumizi yake, (a) je unaweza kuwaambia wananchi ni kiasi gani kilitumika katika kampeni ya Kikwete (b)Je fedha za kampeni ya Kikwete zilitoka wapi?

g. Ni wabunge wangapi ambao umewasaidia kifedha katika kampeni kutoka katika mfuko wako binafsi katika uchaguzi wa 2005, unaweza kuwataja baadhi yao?

h. Kuna kiasi chochote cha fedha ambacho kampeni ya Kikwete ilipokea aidha kutoka Iran au nchi nyingine yoyote ya nje au wafanyabiashara wa nje akiwemo Gen. Al-Adawi?

i. Je una uhusiano wowote wa kibiashara na Yusuph Manji na ni uhusiano upi?

j. Je, msimamo wako kuhusu wizi mkubwa kabisa wa fedha za Watanzania kutoka akaunti ya EPA ni upi na unasema nini kuhusu kutokujulikana kwa watu waliochota fedha za Kagoda na kuzirudisha taslimu. Je wafikishwe mahakamani hata baada ya kurudisha?

k. kila mwezi Mhe. Kuna mtu kafanana kama wewe anayefika personally Hazina kuchukua cheques za Dowans, Je ni Ndugu?
 
Waandishi wa habari wa bongo bwana, sijui taaluma yao wameipatia wapi ?........samahanini waungwana.......lakini ndio ukweli huo............
Jamaa anaitisha conference utasiki .......sema tu uayotaka kusema muungwana........kamaliza hapo.
Hamna swali hamna cha nini......

Kwa maoni yangu, Waandishi wenye ujasiri wa kuweza kumuuliza RA maswali kama aliyoyaorodhesha Mwanakijiji, ni Mwanakijiji mwenyewe na Gurumo (kama wangelikuwepo nchini), Kubenea, Mzee Ndimara, Mzee Mbwambo, Sakina, Mayega, Nyenyembe, Kulwa, Kevin Makyao, Jerry, Kibonde, Hapiness na wengine wachache.

Baadhi ya waandishi kwa mfano wa gazeti la Tanzania Daima wakati mwingine hawaeleweki wana msimamo gani, Kibanda akiongoza! Mwigamba alikuwa kwenye orodha ya waandishi wanaothubutu 'kumfunga paka kengele' lakini naye makala yake ya Jumatano 29 April 2009 imetia mashaka. Alifanya kosa lilelile alilofanya Manyerere kuanza kujihami kwa kusema: "Napenda nieleweke wazi mapema kabisa kwamba, katu katika makala hii silengi kuwatetea mafisadi wa aina yoyote ile. Wasomaji wanaonifuatilia sana ni mashahidi. Nimetumia nguvu nyingi mno kupiga vita ufisadi wa aina yoyote......." Aliendelea kuelezea kwamba wapo watu ambao wanajidai wanapiga vita ufisadi kumbe wana agenda zao za siri zinazotokana na chuki binafsi na kutaka kuwafix wagomvi wao.

Watanzania wenye uchungu na nchi yao wanapigana vita dhidi ya Ufisadi. Kama wapo wenye chuki binafsi wanaojiingiza kwenye vita hiyo si wanasaidia katika mapigano? Mtu mwenye agenda yake ya siri ama Fisadi anaposaidia kumuumbua Fisadi mwingine, wakiumbuana wao kwa wao kuna tatizo gani, si wanasaidia katika kufichua ama kupatikana kwa ushahidi dhidi ya ufisadi?

Waandishi makini, Good luck!
 
Mhe. Rostam:

a. Ulizaliwa wapi, mwaka gani, ulisoma shule ya msingi wapi, sekondari wapi na Chuo Kikuu wapi na mwaka gani?

Umejuaje nimesoma chuo kikuu, na sekondari? Na hutakiwi kuamini nitakachokwambia. Nenda kafanye utafiti kuhusu mimi. Ukishindwa njoo tutafute muda muafaka kufanya usaili na mimi, na mada ya siku hiyo itakuwa mahsusi, wasifu wangu mimi Rostam Aziz, kama unataka kuandika biography. Swali lingine tafadhali.

b. Una umiliki wa makampuni mangapi ya biashara (aidha ukiwa mmiliki au mwenye hisa)?
Umiliki wa makampuni ya biashara, ukitakata kuongelea umiliki wa makampuni, unaweza kuanzia yanarekodiwa, BRELA. Huo ndio uandishi wa kichunguzi. Ukishindwa, again, nitakuwa na zaidi ya furaha kukaa na wewe unifanyie usaili kuongelea biashara zangu na yatokanayo. Nikupe upande wangu wa hadithi, nitakuwa na zaidi ya furaha kufanya hilo. Mwingine?

c. Mmiliki wa Dowans Gen. Aladawi amekiri kukufahamu na kuwa mna urafiki wa karibu; je una hisa yoyote kwenye kampuni yake au yeye ana hisa zozote kwenye mojawapo ya makampuni yako?
Gen. Adawi ana hisa ngapi wapi ilibidi umbane yeye siku hiyo hiyo akwambie ana ngapi wapi alipokiri kunifahamu.

Isitoshe, ndugu mwandishi, umiliki wa Dowans na yote yatokanayo yalichunguzwa na Bunge, na Tukukuru, yameongelewa magazetini, na mitandaoni na mabarazani. Unatakiwa ndugu mwandishi, kuwa na msingi wa yaliyosemwa na wachunguzi binafsi kwanza, kabla ya kuja kuniuliza mimi. Huanzii kwangu. Swali lingine?

d. Ni kwa kiasi gani ulimsaidia Gen. Al-Adawi kuweza kuanzisha kampuni ya Dowans Tanzania Ltd? Unamfahamu mmiliki wa Dowans Holdings SA ya Costa Rica?
Kuhusu ya Dowans, nitakachokisema nimekisema.

e. Ni kwa kiasi gani ulimsaidia Salva Rweyemamu mwandishi wa mojawapo ya vyombo vyako vya habari kupata kazi Ikulu?
Ndugu mwandishi, inabidi uzatiti hisia yako, substantiate the presumption, the premise, of your question, kwamba nilimsaidia, halafu ndio uulize nilimsaidia kiasa gani. Vinginevyo swali lako ni la kufikirika, hypothetical. Si busara kujibu ya kufikirika, hypotheticals. Swali linatofuata tafadhali.

f. Ukiwa Meneja wa Kampuni wa Kikwete bila ya shaka ulisimamia kiasi kikubwa cha fedha na mgawanyo wa matumizi yake, (a) je unaweza kuwaambia wananchi ni kiasi gani kilitumika katika kampeni ya Kikwete (b)Je fedha za kampeni ya Kikwete zilitoka wapi?
Tuko kwenye press conference ya shutuma za Mzee Mengi, wewe unaongelea nitawaambia nini wananchi kuhusu kampeni za Kikwete. Watu wa Igunga wamesha move forward kutoka katika campaign mode na sasa wanatathmini uongozi, na sio kampeni, uongozi wa Kikwete. Ninapima the pulse of the voter, hicho sio kilio cha watu wa Igunga. Nina ulukuki, a laundry list, ya kero za wa Igunga. Kampeni za 2005 halimo. Next.

g. Ni wabunge wangapi ambao umewasaidia kifedha katika kampeni kutoka katika mfuko wako binafsi katika uchaguzi wa 2005, unaweza kuwataja baadhi yao?
Ndugu mwandishi umesema "mfuko binafsi"? Ya mfuko binafsi yanawahusu watu binafsi, kutokana na watu binafsi, kwa ajili ya watu binafsi. Maongezi ya binafsi tutafutane kwa kahawa, kwa faragha. Umesema mwenyewe "mfuko binafsi," huulizi ya binafsi, ndugu mwandishi, huulizi ya binafsi kwenye mdahalo wa umma. Mwingine mwenye swali tafadhali.

h. Kuna kiasi chochote cha fedha ambacho kampeni ya Kikwete ilipokea aidha kutoka Iran au nchi nyingine yoyote ya nje au wafanyabiashara wa nje akiwemo Gen. Al-Adawi?
Kuhusu ya kampeni ya Kikwete, nitakachokisema nimekisema.

i. Je una uhusiano wowote wa kibiashara na Yusuph Manji na ni uhusiano upi?
Sina ruhusa ya Yusuph Manji au yeyote yule niliye na mahusiano nae kuongelea mahusiano yetu hadharani. Baadhi ya mahusiana ya kibiashara huwa ni trade secrets anyway. Swali lingine.

j. Je, msimamo wako kuhusu wizi mkubwa kabisa wa fedha za Watanzania kutoka akaunti ya EPA ni upi na unasema nini kuhusu kutokujulikana kwa watu waliochota fedha za Kagoda na kuzirudisha taslimu. Je wafikishwe mahakamani hata baada ya kurudisha?
Ndio wafikishwe, ndugu mwandishi, naamini siku zote kwamba anaeshukiwa kuvunja sheria anatakiwa apelekwe mbele ya vyombo vya sheria. Ahsanteni sana.

Ndugu wananchi, sasa tunawarudisha studio zetu kujiunga na Professor Jay akisema:
Piga makofi, Piga Makofi, Piga Makofi tafadhali...
Piga makofi, Piga Makofi, Piga Makofi tafadhali...
 
i feel to wear an explosive vest.... and be somewhere of course....natania tu mjomba,ila nikipewa bunduki!!
 
Hayo masuala hamuwezi kuyauliza maana aliyeandaa ndie mwenye mpangilio wake na amekusudia kusema ya kwake tu ,kama mnataka kumuuliza hayo andaeni kongamano lenu na kumualika ,sio mnasubiri mtu aandae kitu chake halafu mzuke na mikakati yenu ,hilo halikubaliki ,maana anayo hata haki ya kukusanya masuali na kuyajibu yale ayapendayo.

Kwa nini ninyi kama waandishi musiwaandalie mkutano wa pamoja wahusika wote wa ufisadi na kuwaweka kwenye round table na hapo kuwatupia masuala ,pengine masuala kwa idadi sawa bila ya kuonekana mpo hapo kama mmekodiwa kumkandamiza mtu kwa sababu ya utajiri wake na nyio mna njaa zenu mnataka kumfisidi ,hivi waTz mna choyo sana ,na tamaa na shida zimewafanya muanze kupoteza imani kwa matajiri wachache tulio nao. Mnaacha kupambana na adui wa nchi hii ambae ni Sultani CCM mnaenda kuvamia watu majumbani mwao ,sasa usione hapo Rostamu ameshawanunua waandishi wote ,kila mwandishi apewe bahasha iliyonona muone mtakavyo umbuka ,kuna waandishi hawajawahi kuona milioni moja toka wazaliwe na nafasi ndio hiyo ,dogo lazima amsifu Rostam na kuona inafaa apewe na uraisi kabisa.

Let us stand for the uprising against CCM & not inviduals.
 
Ndugu wananchi, sasa tunawarudisha studio zetu kujiunga na Professor Jay akisema:
Piga makofi, Piga Makofi, Piga Makofi tafadhali...
Piga makofi, Piga Makofi, Piga Makofi tafadhali...

kudandia treni kwa mbele huko. Mhe. Rostam.
 
Rostam kukutana na waandishi wa habari

Kuna habari kwamba kesho (Jumapili) saa 5 mchana Rostam Aziz atakuwa na mkutano na waandishi wa habari katika hoteli ya Kempinski.

Huyu alistahili kuwa keko huku akiisaidia polisi katika uchunguzi wa ufisadi wa Kagoda wa shilingi bilioni 40 na ufisadi wa Richmond/Dowans wa shilingi bilioni 200. Anafahamu fika kwamba Kikwete yuko mifukoni mwake na hawezi kufurukuta maana anayajua madhambi yote yaliyofanyika hadi kumuwezesha Kikwete kuingia Ikulu. Sasa kapata jeuri na anataka kuanza kuonyesha ufalme aliokuwa nao katika serikali iliyopo madarakani. Inatia kinyaa na kuchefua roho vibaya sana kumuona huyu jamaa akifanya atakavyo bila kuguswa na vyombo vya dola.
 
Umejuaje nimesoma chuo kikuu, na sekondari? Na hutakiwi kuamini nitakachokwambia. Nenda kafanye utafiti kuhusu mimi. Ukishindwa njoo tutafute muda muafaka kufanya usaili na mimi, na mada ya siku hiyo itakuwa mahsusi, wasifu wangu mimi Rostam Aziz, kama unataka kuandika biography. Swali lingine tafadhali.

Umiliki wa makampuni ya biashara, ukitakata kuongelea umiliki wa makampuni, unaweza kuanzia yanarekodiwa, BRELA. Huo ndio uandishi wa kichunguzi. Ukishindwa, again, nitakuwa na zaidi ya furaha kukaa na wewe unifanyie usaili kuongelea biashara zangu na yatokanayo. Nikupe upande wangu wa hadithi, nitakuwa na zaidi ya furaha kufanya hilo. Mwingine?

Gen. Adawi ana hisa ngapi wapi ilibidi umbane yeye siku hiyo hiyo akwambie ana ngapi wapi alipokiri kunifahamu.

Isitoshe, ndugu mwandishi, umiliki wa Dowans na yote yatokanayo yalichunguzwa na Bunge, na Tukukuru, yameongelewa magazetini, na mitandaoni na mabarazani. Unatakiwa ndugu mwandishi, kuwa na msingi wa yaliyosemwa na wachunguzi binafsi kwanza, kabla ya kuja kuniuliza mimi. Huanzii kwangu. Swali lingine?

Kuhusu ya Dowans, nitakachokisema nimekisema.

Ndugu mwandishi, inabidi uzatiti hisia yako, substantiate the presumption, the premise, of your question, kwamba nilimsaidia, halafu ndio uulize nilimsaidia kiasa gani. Vinginevyo swali lako ni la kufikirika, hypothetical. Si busara kujibu ya kufikirika, hypotheticals. Swali linatofuata tafadhali.

Tuko kwenye press conference ya shutuma za Mzee Mengi, wewe unaongelea nitawaambia nini wananchi kuhusu kampeni za Kikwete. Watu wa Igunga wamesha move forward kutoka katika campaign mode na sasa wanatathmini uongozi, na sio kampeni, uongozi wa Kikwete. Ninapima the pulse of the voter, hicho sio kilio cha watu wa Igunga. Nina ulukuki, a laundry list, ya kero za wa Igunga. Kampeni za 2005 halimo. Next.

Ndugu mwandishi umesema "mfuko binafsi"? Ya mfuko binafsi yanawahusu watu binafsi, kutokana na watu binafsi, kwa ajili ya watu binafsi. Maongezi ya binafsi tutafutane kwa kahawa, kwa faragha. Umesema mwenyewe "mfuko binafsi," huulizi ya binafsi, ndugu mwandishi, huulizi ya binafsi kwenye mdahalo wa umma. Mwingine mwenye swali tafadhali.

Kuhusu ya kampeni ya Kikwete, nitakachokisema nimekisema.

Sina ruhusa ya Yusuph Manji au yeyote yule niliye na mahusiano nae kuongelea mahusiano yetu hadharani. Baadhi ya mahusiana ya kibiashara huwa ni trade secrets anyway. Swali lingine.

Ndio wafikishwe, ndugu mwandishi, naamini siku zote kwamba anaeshukiwa kuvunja sheria anatakiwa apelekwe mbele ya vyombo vya sheria. Ahsanteni sana.

Ndugu wananchi, sasa tunawarudisha studio zetu kujiunga na Professor Jay akisema:
Piga makofi, Piga Makofi, Piga Makofi tafadhali...
Piga makofi, Piga Makofi, Piga Makofi tafadhali...

- Kumbe ndio maana watu humu husema kwenye huu msafara tunao makenge pia, maana ninaamini kwamba maswali ya Mkulu Mwanakijiji yanatuwakilisha sisi wananchi wengi walalahoi,

- Sasa hapo juu mkuu anamjibia nani hasa kama sio Makamba na Rostam? duh!

Respect.

FMES!
 
1. Re: Rostam kukutana na waandishi wa habari

Tuko kwenye press conference ya shutuma za Mzee Mengi, wewe unaongelea nitawaambia nini wananchi kuhusu kampeni za Kikwete...


- Duh! Mkuu ya press conference kuwa ya shutuma za Mengi umeyatoa wapi? Mbona kichwa cha hii mada kiko wazi kwamba atakutana tu na waandishi tu? au?

FMES!
 
- Kumbe ndio maana watu humu husema kwenye huu msafara tunao makenge pia, maana ninaamini kwamba maswali ya Mkulu Mwanakijiji yanatuwakilisha sisi wananchi wengi walalahoi;

- Sasa hapo juu mkuu anamjibia nani hasa kama sio Makamba na Rostam? duh!

Respect.

FMES!

FMES i think you misunderstood Dilunga; that was speculative response to the questions posed by MMM; sasa kama unataka aandike utakacho basi na wewe andaa majibu-- That is democracy/freedom of speech lets give Dilunga similar representative role kwa upande wa pili

He is just spinning and no need to hit back... Lets share openness
 
Mkutano huu wa waandishi wa habari inabidi uwe ni juu ya Rostam. Asiachwe na ajenda yake bali waandishi ndio waamue muelekeo wa ajenda ya mazungumzo. Baadhi tu ya maswali ambayo itakuwa vizuri kupata majibu yake ni haya:

Mhe. Rostam:

a. Ulizaliwa wapi, mwaka gani, ulisoma shule ya msingi wapi, sekondari wapi na Chuo Kikuu wapi na mwaka gani?

b. Una umiliki wa makampuni mangapi ya biashara (aidha ukiwa mmiliki au mwenye hisa)?

c. Mmiliki wa Dowans Gen. Aladawi amekiri kukufahamu na kuwa mna urafiki wa karibu; je una hisa yoyote kwenye kampuni yake au yeye ana hisa zozote kwenye mojawapo ya makampuni yako?

d. Ni kwa kiasi gani ulimsaidia Gen. Al-Adawi kuweza kuanzisha kampuni ya Dowans Tanzania Ltd? Unamfahamu mmiliki wa Dowans Holdings SA ya Costa Rica?

e. Ni kwa kiasi gani ulimsaidia Salva Rweyemamu mwandishi wa mojawapo ya vyombo vyako vya habari kupata kazi Ikulu?

f. Ukiwa Meneja wa Kampuni wa Kikwete bila ya shaka ulisimamia kiasi kikubwa cha fedha na mgawanyo wa matumizi yake, (a) je unaweza kuwaambia wananchi ni kiasi gani kilitumika katika kampeni ya Kikwete (b)Je fedha za kampeni ya Kikwete zilitoka wapi?

g. Ni wabunge wangapi ambao umewasaidia kifedha katika kampeni kutoka katika mfuko wako binafsi katika uchaguzi wa 2005, unaweza kuwataja baadhi yao?

h. Kuna kiasi chochote cha fedha ambacho kampeni ya Kikwete ilipokea aidha kutoka Iran au nchi nyingine yoyote ya nje au wafanyabiashara wa nje akiwemo Gen. Al-Adawi?

i. Je una uhusiano wowote wa kibiashara na Yusuph Manji na ni uhusiano upi?

j. Je, msimamo wako kuhusu wizi mkubwa kabisa wa fedha za Watanzania kutoka akaunti ya EPA ni upi na unasema nini kuhusu kutokujulikana kwa watu waliochota fedha za Kagoda na kuzirudisha taslimu. Je wafikishwe mahakamani hata baada ya kurudisha?
Mkuu MMKJJ, pamoja na maswali yako kuwa very relevant huku yakiwakilisha mawazo ya wengi, aliyeitisha press conference ni RA, yeye ndie anayejua anataka kusema nini?. miongoni mwa hayo, zikiwemo issues zinazohusiana na mswali haya its well and good akiulizwa.
Kwa mtazamo wangu, hakuna sababu ya kuisubiri press conference ya RA ndipo tuulize maswali haya, maswali kama haya yalibidi RA ualizwe man to man ama waandishi ndio waandae press conference ndipo wajimwage watakavyo.
Kwa kumbukumbu zangu, hata press conferences za Mengi enzi hizo, alikuwa hakubali kuulizwa maswali yoyote. Ni press release na press statement anayeisoma mwenyewe, mwisho wa statement is the end, period.
Hivi ndivyo alivyo RA, unless na yeye sasa awe amebadilika maana last press conf. ya Mengi, alikubali maswali.
Hata RA akikubali maswali, bado maswali haya ni mengi mno kuulizwa yote bila organized media.
Hata hivyo nakushukuru MMKJJ kwa kuibua issues nzito za kumuuliza RA. Natumaini watatokea baadhi ya waandishi wetu watakaoyatumia maswali yako kuulizwa maswali ya maana.
Pia sitashangaa kama waandishi wengi watakaa kimya kuwahi awaiting 'sunday lunch at kempinsky' na kutokana na kuhofia waandishi mamluki wa Mengi wasije chafua hali ya hewa, kama ambavyo waandishi mamluki wa RA walivyotaka kuchafua hali ya hewa press conference ya Dr. Mwakiembe, nadhani hata ile session inayopendwa sana sana na waandishi wetu ya 'brown envelopes' inaweza isiwepo!.
 
1. Re: Rostam kukutana na waandishi wa habari




- Duh! Mkuu ya press conference kuwa ya shutuma za Mengi umeyatoa wapi? Mbona kichwa cha hii mada kiko wazi kwamba atakutana tu na waandishi tu? au?

FMES!
Si kila mtu hanauhakikika kama wewe wengine tayari wanajua anakwenda kuongea nini..kimsingi anakwenda kumchamba vilivyo Mengi na mambo yake na pia atatoa ushuhuda jinsi alivyopata kufisadi makampuni kadhaa hapa nchini.kimsingi itakuwa ni aibu kwa Mengi na kila mtu
 
Si kila mtu hanauhakikika kama wewe wengine tayari wanajua anakwenda kuongea nini..kimsingi anakwenda kumchamba vilivyo Mengi na mambo yake na pia atatoa ushuhuda jinsi alivyopata kufisadi makampuni kadhaa hapa nchini.kimsingi itakuwa ni aibu kwa Mengi na kila mtu[/QUOTE]

Haya mkuu kula refreshment ya maana ya aibu hapa chini:-



Mheshimiwa Spika, hadi kufikia tarehe 31 Disemba 2007 siku ilipowasilisha taarifa yake kwako, Kamati Teule ilikuwa imewahoji jumla ya mashahidi 75 na kuuliza maswali 2717 na kuzipitia nyaraka na kumbukumbu 104. Mashahidi 4 kati ya hao walikuja kwa hiari yao bila kupelekewa hati za kuitwa. Mashahidi 7 waliitwa mara mbili. Mashahidi wawili, Ndugu Daniel Yona na Mhe. Rostam Aziz, (Mb) walipelekewa hati za kuitwa mbele ya Kamati Teule lakini hawakufika kwa maelezo kwamba walikuwa nje ya nchi.

Mheshimiwa Spika, Ndugu Daniel Yona alitakiwa na Kamati Teule atoe maelezo kuhusu msingi wa uamuzi wake wa kuipa Richmond Development Company LLC, haki maalum ya kipekee (exclusive right) ya miezi 18 kuhusu mradi wa Bomba la Mafuta kutoka Dar es Salaam hadi Mwanza mwaka 2004 wakati huo akiwa Waziri wa Nishati na Madini. Maelezo ya ziada ya mradi huu nitayatoa baadaye.

Mheshimiwa Spika, vilevile Mhe. Rostam Aziz alitakiwa atoe maelezo kuhusu uhusiano wake na Kampuni za Richmond Development Company LLC na Dowans Holdings S.A baada ya mashahidi kadhaa kudai kuwa ana uhusiano nazo. Aidha, alitakiwa na Kamati Teule aeleze kwa nini anwani ya barua pepe ya kampuni yake ya Caspian Construction Ltd ilitumiwa na Dowans. Kamati Teule ilitaka vilevile kupata ufafanuzi kutoka kwake kuhusu baadhi ya wafanyakazi wa kampuni yake wanaosemekana kuwa ni watumishi vilevile wa Dowans Holdings S.A.

Mheshimiwa Spika, leo tunapowasilisha taarifa hii mbele ya Bunge lako tukufu, tunajisikia kuutua mzigo mzito sana ulioanza kutuelemea kutokana na kuzongwa kila kukicha na kila aina ya uzushi, uchochezi, uchonganishi na hata vitisho. Tumezushiwa kuhongwa magari ya kifahari na fedha taslimu; tumetuhumiwa kuendesha vita dhidi ya Waislamu na mara nyingine tuhuma hiyo ikageuka kuwa vita dhidi ya Wakristo ndani ya Serikali; tumesingiziwa kuibadilisha taarifa yetu mara mbili, baadhi wakisema kwa ushawishi wa fedha, wengine wakidai kwa shinikizo la Mhe. Spika na wengine kwa shinikizo la Waziri Mkuu; tumeshuhudia pilikapilika za usiku na mchana za kujipanga na kuwashawishi baadhi ya Mawaziri na Wabunge kuikana taarifa hii na mapendekezo yake kiasi cha wengine wetu kujiuliza: kulikoni mtu asiye na hatia kuweweseka?

Mheshimiwa Spika, naomba kwa niaba ya wajumbe wenzangu wa Kamati Teule, kukuhakikishia wewe binafsi na Bunge lako tukufu kuwa tumekamilisha kazi tuliyopewa kwa uaminifu na ujasiri mkubwa, dhamira safi, moyo wa uzalendo na kwa kumtanguliza mbele Mwenyezi Mungu katika kila tulilolifanya. Tulichukua kila tahadhari tusibanwe na mgongano wowote wa kimaslahi kiasi kwamba mjumbe mwenzetu, Mhe. Eng. Stella Manyanya, mwajiriwa wa muda mrefu wa TANESCO ambaye alikuwa kwenye likizo isiyo na malipo, akaamua kukatisha ajira yake kwa kujiuzuru. Aidha, tunakuhakikishia Mheshimiwa Spika kuwa hatukupokea senti tano ya mtu wala baiskeli yake. Mwenye ushahidi tofauti, basi alithibitishie Bunge hili tukufu. Mimi na wajumbe wenzangu wa Kamati Teule tuko tayari kuwajibika kisiasa.
 
FMES i think you misunderstood Dilunga; that was speculative response to the questions posed by MMM; sasa kama unataka aandike utakacho basi na wewe andaa majibu-- That is democracy/freedom of speech lets give Dilunga similar representative role kwa upande wa pili

He is just spinning and no need to hit back... Lets share openness

- Ooooh! he is just spinning kwa ajili ya fisadi papa Rostam, wakati wananchi tuna uchungu na taifa letu? it is strange no?



William.
 
Si kila mtu hanauhakikika kama wewe wengine tayari wanajua anakwenda kuongea nini..kimsingi anakwenda kumchamba vilivyo Mengi na mambo yake na pia atatoa ushuhuda jinsi alivyopata kufisadi makampuni kadhaa hapa nchini.kimsingi itakuwa ni aibu kwa Mengi na kila mtu
Mzee Mengi ni briliant bussness man ila watu wenye IQ ya juu, pia wanamuona Mzee Mengi kama mjinga fulani.
Hakuna ubishi RA pia ni mfanya biashara tajiri iwe ni kwa kufisidi, magendo na halali, the botom line ana pesa ila pia ana IQ ndogo compared na Mengi.
Kama ni kweli RA ataanika uchafu wa Mengi, kwa kuamini, kumchafua Mengi ndio kutamsafisha, RA ndio atazidi kuonekana kituko.
Kwenye list ya mafisadi papa, Mengi amentaja Jeethu. Hii ni habari ingine, kama kuna Mafia Bongo, Jeethu ni 'Don', jamaa hatafanya press conference wala mahakamani haendi, Watanzania tusubiri tuu kitakacho mkuta Mzee wetu huyu and there will be no one who 'will live to tell'
Tumwache RA naye amwage pumba zake, waandishi wapate cha kuandika.
Mzee Mengi aliitaja list ili kuwaprovoke apate mass rally behind him to fight them. Wapiga kelele kama RA hawatamuumiza kichwa, ila wale watakao kaa kimya, ndio watamnyima usingizi.
lets sit and watch the movie...
 
- Ooooh! he is just spinning kwa ajili ya fisadi papa Rostam, wakati wananchi tuna uchungu na taifa letu? it is strange no?

William.
Bill, its not strange, ni kweli wananchi tuna uchungu na taifa letu, ila kuna wenye uchungu na taifa letu wanaowachukia mafisadi huku wakiwaimbia nyimbo za sifa na mapambio kwa walezi wa mafisadi, kwangu mimi huu ni unafiki.
Hakuna ubishi kuhusu ufisadi wa RA. Lakini kwa mujibu wa sheria taratibu na kanuni, he is crystal clean before the eyes of the law, so do Mkapa and the entire CCM as well ambayo ndiyo ilitegemea fungu la RA kama mweka hazina wake, mkuu wa kampeni, mfadhili mkuu, mbunge, kamanda wa UVCCM, mwanaCCM damu, mjumbe wa NEC na Mjumbe wa CC!.
Mimi ni mmoja wa wanaomini Mengi ana uchungu sana na taifa lake ndio maana akafikia point of 'calling a spade a spade' and not as a big spoon as others do, but its very unfortunately, he is fighting a loosing battle.
Alichofanya is not right but he has the guts and will bear the consequences.
Hakuna ubishi Tanzania kama taifa, limekumbwa na adui ufisadi who is very powerfull ana ameshika mpaka kwenye the axis of which our nation hangs.
Kutokana na nguvu za adui huyu, ili kumtokomeza we must wage war from within. Mengi knows who is the realy enemy, wewe unamjua na mimi pia namjua. kumpungeza Mengi kwa kuwataja mafisadi papa huku akimsifu JK, kwangu mimi ni unafiki wa hali ya juu ambao uko shared wengi tuu.
Kwa vile adui huyu, yuko ndani kwetu, tena sio sebuleni, bali chumbani tena kwenye jiwe kuu, hivyo namna pekee ya kushinda vita hii ya ufisadi kwa kwa kupigana from within na sio kwa kupiga kelele, kunyoosheana vidole na vilio vya public sympathy huku tukivunja sheria za nchi.
Nausisitiza ule msemo, if you can't beat them, join them, mimi nilijigunduliaga zamani kuwa I can't beat them, I have now joined them na kujikalia kimya nikikusanya nguvu kusubiri the most aportune moment to support war.
2010 is too near, ni ushind wa kishindo ila tujipange vizuri 2015 tusafishe nyumba sio kwa kuwanyooshea vodole mafisadi, bali kwa kufanya fatiki ya usafi, ambayo its very unfortunately inaweza kuwakumba hata wasafi wanaowakumbatia mafisadi.
 
Bill, achana na huyo pasco, asikusumbue your brain. yeye ni miongoni mwa 0.1 per cent ya wana-JF wanaojaribu kuwashabikia mafisadi kwa kubuni sababu mbali mbali kama vile "unafiki wa Mengi" n.k. hawa kwa kuwa idadi yao ni ndogo, wanajaribu kuwa vocal minority. Hawana lolooooooooooooote!!!!!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom