Mkalukungone Mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 2,437
- 5,235
Mwanasiasa mwandamizi aliyewahi kuwa Mbunge wa Viti Maalumu CCM mkoa wa Simiyu, Mkuu wa Wilaya ya Meatu na pia Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake wa CHADEMA (BAWACHA) Kanda ya Serengeti, Rosemary Kirigini amejiunga na chama cha ACT Wazalendo.
Kirigini amejiunga na Chama hicho na kutangazwa mbele ya wananchi wa Mwandoya Jimbo la Kisesa, Mkoani Simiyu siku ya Jumamosi Agosti 16, 2025.
Akizungumza baada ya kutangazwa kujiunga, Kirigini amesema wananchi watarajie mambo makubwa kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025 kwani chama hicho kimejipambanua vya kutosha.
Kirigini amejiunga na Chama hicho na kutangazwa mbele ya wananchi wa Mwandoya Jimbo la Kisesa, Mkoani Simiyu siku ya Jumamosi Agosti 16, 2025.
Akizungumza baada ya kutangazwa kujiunga, Kirigini amesema wananchi watarajie mambo makubwa kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025 kwani chama hicho kimejipambanua vya kutosha.