Umetisha Mama la Mamaa, sisi Wazee kazi yetu ni kutulia zetu kwenye Mkeka huku tumefunga Msuli wakati tukipeluzi Ubuyu wa moto moto kutoka kwa the Queen herself Nifah 🤗Unakumbuka nilikuahidi? Ndio natekeleza kwa vitendo sasa.
Nikileta ubuyu sasa hivi ni exclusive tu, huwezi kuupata kokote!
Mwenzangu ana madeni na maisha ya wasanii si unayajua tena?Kama ndiivyo basi RJ kazingua sababu hali yake kifedha haikuwa nzuri ndio maana akaanza kujiongeza. Anatakiwa akumbuke kwanini aliitafuta hiyo kazi.
Pale kwa kaka Mondi mambo ya fedha si rahisi kwa kila mtu.
Tatizo ameshazingua sana Lamata amechoka na wasanii wenzie pia hawamtaki.Watengeneze scene RJ awe kama ameenda kusoma Marekani tena ingenoga kweli maana inge waacha watazamaji kwenye suspense kujua kama jamaa atarudi na cheti ama laaaaaaah director ana kwama wapi
Kwa hili nasimama na RJ..DJ maarufu nchini, Romeo George ‘Romy Jones’ ameingia katika bifu zito na bosi wake katika tasnia ya filamu mwanamama Leah Mwendamseke ’Lamata’ kwa kile kinachodhaniwa kuwa vita ya kimaslahi.
Wawili hao wamefanya kazi kwa mafanikio katika tamthilia maarufu nchini ya Jua Kali, kabla ya kuibuka kwa majukumu mapya yaliyomzidia Romy Jones kutimiza wajibu wake wa kushiriki ktk tamthilia hiyo.
CHANZO NI WASAFI FESTIVAL!
Ikumbukwe kuwa, licha ya Romy Jones kuwa ndugu wa damu wa Diamond Platinumz, ndiye DJ wake rasmi katika kila tamasha la muziki atakaloshiriki.
Hiyo imepelekea Romy Jones kuwa busy kutokana na utitiri wa shows nyingi ndani ya tamasha hilo ambalo Diamond kama muasisi na mmiliki amewekeza nguvu zake nyingi huko kwa kushiriki binafsi katika kila mkoa ambao kuna ratiba ya kufanyika kwa Wasafi Festival.
Romy Jones baada ya kutingwa na matamasha, akakosa kushiriki kwa ukamilifu na pengine kutokushiriki kabisa kwa sehemu kubwa katika tamthilia hiyo.
Kitendo hiki kilimuumiza sana Lamata ambaye ndiye aliyempa nafasi ya kuigiza kwa mara ya kwanza kupitia tamthilia hiyo kubwa na ilikuwa bahati tu kwa mujibu wake mwenyewe Romy Jones kutokana na mahojiano kadhaa aliyowahi kuyafanya juu ya ushiriki wake katika tamthilia hiyo na nyingine za Kiswahili.
Balaa baina yao lilizuka pale Romy Jones alipokwama kwenye mambo yake, huku akitaka kupewa malipo kutoka kwa uongozi wa Jua Kali ambako hakuwa ameonekana katika shooting kadha wa kadha.
Lamata kama bosi wa tamthilia hiyo hivi sasa amepumzika kwa kiasi kikubwa majukumu kutokana na ujauzito wake kufikia ukingoni karibuni na kujifungua, aliingilia kuweka sawa baada ya mzozo mkubwa kuibuka kati ya mhasibu wake na Romy Jones juu ya malipo.
Alimpigia simu RJ na kuzozana nae kwa kumpa ukweli wa mambo jinsi gani anavyokwamisha shooting, na kutoa maagizo RJ atumiwe laki moja katika simu kwa ajili ya mafuta ya gari kwa RJ kisha amfuate Lamata alipo wakajadili kwa kina, na ikiwa ni pamoja na kulipwa stahiki zake zote.
RJ hakukubaliana na hilo, punde laki moja ilipoingia kupitia simu yake na mhasibu kupiga simu kuthibitisha, RJ akagombana na mhasibu kisha akaurudisha muamala.
Yeye RJ alitaka kuongea wayaweke sawa na sivyo Lamata alivyotaka ‘kumalizana’ nae.
Hadi ninavyoandika hapa, kuna uwezekano mkubwa wa Billy Jr. kutokuonekana tena katika tamthilia ya Jua Kali baada ya kuchokwa na kila mmoja hadi wasanii wenzie kwa ‘uzinguaji’ wake.
RJ mwenyewe anahaha huku na huko kuomba kikao na Lamata bila mafanikio…
Ndimi,
Nifah
View attachment 2844179View attachment 2844182
Si ndio uzinguaji wemyewe au?Kwakweli sio mzinguaji itakuwa ratiba tu zimembana
Basi watakuwa wamesha mpata mtu mwingineTatizo ameshazingua sana Lamata amechoka na wasanii wenzie pia hawamtaki.
Hapo kazi kufanyika ni vigumu.
Sasa kosa la Lamata ni nini? Mtu hajatokea kutimiza wajibu wake, anaibuka anataka hela.Kwa hili nasimama na RJ..
Lamata Sasa kazidi mara ya kwanza alikuwa Neila..Akabadilishwa sasa Bill Jr hapana aisee
Lete facts dokta..ushaambiwa mtu haonekan site na maananyake hakuna official information prior the incidence, je huu sio uzinguaj?Kwa hili nasimama na RJ..
Lamata Sasa kazidi mara ya kwanza alikuwa Neila..Akabadilishwa sasa Bill Jr hapana aisee
Nifah mwaka huu kwenye ubuyu hutaki utani.DJ maarufu nchini, Romeo George ‘Romy Jones’ ameingia katika bifu zito na bosi wake katika tasnia ya filamu mwanamama Leah Mwendamseke ’Lamata’ kwa kile kinachodhaniwa kuwa vita ya kimaslahi.
Wawili hao wamefanya kazi kwa mafanikio katika tamthilia maarufu nchini ya Jua Kali, kabla ya kuibuka kwa majukumu mapya yaliyomzidia Romy Jones kutimiza wajibu wake wa kushiriki ktk tamthilia hiyo.
CHANZO NI WASAFI FESTIVAL!
Ikumbukwe kuwa, licha ya Romy Jones kuwa ndugu wa damu wa Diamond Platinumz, ndiye DJ wake rasmi katika kila tamasha la muziki atakaloshiriki.
Hiyo imepelekea Romy Jones kuwa busy kutokana na utitiri wa shows nyingi ndani ya tamasha hilo ambalo Diamond kama muasisi na mmiliki amewekeza nguvu zake nyingi huko kwa kushiriki binafsi katika kila mkoa ambao kuna ratiba ya kufanyika kwa Wasafi Festival.
Romy Jones baada ya kutingwa na matamasha, akakosa kushiriki kwa ukamilifu na pengine kutokushiriki kabisa kwa sehemu kubwa katika tamthilia hiyo.
Kitendo hiki kilimuumiza sana Lamata ambaye ndiye aliyempa nafasi ya kuigiza kwa mara ya kwanza kupitia tamthilia hiyo kubwa na ilikuwa bahati tu kwa mujibu wake mwenyewe Romy Jones kutokana na mahojiano kadhaa aliyowahi kuyafanya juu ya ushiriki wake katika tamthilia hiyo na nyingine za Kiswahili.
Balaa baina yao lilizuka pale Romy Jones alipokwama kwenye mambo yake, huku akitaka kupewa malipo kutoka kwa uongozi wa Jua Kali ambako hakuwa ameonekana katika shooting kadha wa kadha.
Lamata kama bosi wa tamthilia hiyo hivi sasa amepumzika kwa kiasi kikubwa majukumu kutokana na ujauzito wake kufikia ukingoni karibuni na kujifungua, aliingilia kuweka sawa baada ya mzozo mkubwa kuibuka kati ya mhasibu wake na Romy Jones juu ya malipo.
Alimpigia simu RJ na kuzozana nae kwa kumpa ukweli wa mambo jinsi gani anavyokwamisha shooting, na kutoa maagizo RJ atumiwe laki moja katika simu kwa ajili ya mafuta ya gari kwa RJ kisha amfuate Lamata alipo wakajadili kwa kina, na ikiwa ni pamoja na kulipwa stahiki zake zote.
RJ hakukubaliana na hilo, punde laki moja ilipoingia kupitia simu yake na mhasibu kupiga simu kuthibitisha, RJ akagombana na mhasibu kisha akaurudisha muamala.
Yeye RJ alitaka kuongea wayaweke sawa na sivyo Lamata alivyotaka ‘kumalizana’ nae.
Hadi ninavyoandika hapa, kuna uwezekano mkubwa wa Billy Jr. kutokuonekana tena katika tamthilia ya Jua Kali baada ya kuchokwa na kila mmoja hadi wasanii wenzie kwa ‘uzinguaji’ wake.
RJ mwenyewe anahaha huku na huko kuomba kikao na Lamata bila mafanikio…
Ndimi,
Nifah
View attachment 2844179View attachment 2844182
Lols!Nifah mwaka huu kwenye ubuyu hutaki utani.
Wakianzisha nyuzi za mwisho wa mwaka za wachangiaji walioshinda JF idara ya ubuyu nakupigia kura.
Weka weka ubuyu.Lols!
Asante Mkuu…
Kama umenishawishi kesho niwape ubuyu mwingine hiviiiiii, ninao tele kabatini mwangu.
Ni mimi kuchagua upi wa kuweka na upi wa kusubiri.
Ngojea na mimi nisikilizie kutoka kwako maana sio mtazamaji wa hiyo makitu 😃Ngoja tuone itakuwaje.
Ni kweli mkuu. Mwaka 2018 nilimpa kazi ya kunitangazia biashara yangu alinifanyia kwa uaminifu wa hali ya juu kama tulivyokubaliana. Pia aliniunganisha na dogo mmoja wa Graphics ambaye naye ni mtu makini na ninafanya nae kazi hadi leo. Romy Jones ni mtu mwema sana. Katika hili siko upande wowote ila ninawasihi wakae chini na kuliweka hili jambo sawa kwa maslahi mapana ya pande zote.Kwa lolote lile nasimama upande wa RJ.
RJ ni mtu poa sana.
Sababu zake zinaelezeka mbona ila lamata sio msikiliza wa Sababu za wenzake anajali kazi kuliko utu..Sasa kosa la Lamata ni nini? Mtu hajatokea kutimiza wajibu wake, anaibuka anataka hela.
Tena kwenye igizo ambalo linaendelea…
Huko Wasafi wanalipana Tsh ngapi? Nahisi pesa wanazolipana ni haba.Mimi pia namkubali mno RJ, ila katika hili kazingua.
Ile ni kazi, kukosekana kwa RJ kama moja ya wahusika wakuu katika tamthilia kuna gharama hadi ya kubadili mtiririko mzima wa story.
Usimtetee sababu ya Wasafi Festival, ana makosa kweli.